Misaada yawasili kwa waathiriwa
Misaada ya kibinadamu imeanza kuwasili katika wilaya ya Dhading, karibu na kitovu cha tetemeko la ardhi lililotokea nchini Nepal na kusababisha vifo vya zaidi ya watu elfu tano.
Lakini pia vijiji vingi nchini humo bado havijafikiwa na misaada.
Katika mji mkuu Kathmandu, mvua kubwa iliyonyesha kote usiku wa kuamkia leo Jumatano, ilitatiza pakubwa shughuli za uokoaji.
Maelfu ya watu wanajaribu kuondoka kwenye mji huo mkuu na kukimbilia vijijini muao ili kuwatafuta jamaa zao.
Siku ya Jumanne, wakwea milima wote waliokuwa wamekwama juu ya mlima Everest waliondolewa huku serikali ikisitisha shughuli zote za kuukwea mlima huo.
TAIFA STARS HAZARANI
-
Kaimu kocha wa timu ya taifa ya Tanzania Etiene Ndairagije ametangaza
kikosi cha timu ya taifa chenye wachezaji 30 ambao wanajiaandaa na mchezo
wa kuwania ...
6 years ago

