Jokate na Lucci wanaileta documentary ya behind the scene ya “Kaka dada”


jokateVideo kali kama hii lazima utakuwa na hamu ya kuona jinsi ilivyotengenezwa… ‘Kaka dada’ video ya Lucci na Jokate ambayo imetoka ijumaa wiki iliyopita ina story nyingi sana nyuma yake ambazo wengi hawafahamu.
Kuna baadhi ya vipande havikurekodiwa kutokana na mambo yaliyotokea wakati wa kuandaa hii video mfano ukiangalia kwa makini,  kuna scene ya upande mmoja tu ambapo Jokate anaonekana kumuonea wivu Lucci akiwa na msichana mwingine wakati wimbo unasema pia Lucci anajua Jokate ana boyfriend na ana wivu juu ya hilo.
Plan za video ilitakiwa kuwe na scene ikimuonyesha Lucci anamuonea wivu Jokate, lakini haikuweza kurekodiwa.
kidotiLucci kaongea na millardayo.com na kusema fans wote wa music especially video hii watapata nafasi ya kuona documentary ikionyesha utengenezaji mzima wa video ya Kaka dada kuanzia wakitoka Tanzania kuelekea Kenya, mambo yote yaliyotokea nyuma ya pazia mpaka scene ambazo zilifutwa.
Unaambiwa kuna baadhi ya scene hazikuwekwa kwenye video ambazo Jokate alikuwa anacheza, scene hii ilifanyika usiku sana na Jokate alikuwa amechoka, producer akaamua wasiziweke kwenye video kwasababu hakuchangamka kama walivyotegemea.
Kauli ya Lucci ni kwamba kuna mambo mengi ambayo ni mazuri kuona hasa kutokana na ukali wa video yenyewe ndio maana wameamua kuitengenezea documentary, endelea kupita hapa millardayo.com kwa ajili ya info zaidiobama
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company