Ghasia kwenye kura ya maamuzi Misri


Jeshi linawataka watu kupiga rasimu ya katiba kura ya ndio
Kulikuwa na ghasia katika siku ya kwanza ya kupigia kura ya maamuzi rasimu ya katiba mpya ambayo huenda ikatoa nafasi ya kuandaliwa kwa uchaguzi mpya nchini humo.

Wafuasi wa Rais aliyeondolewa mamlakani Mohammed Morsi walizua vurugu na hata kusababisha vifo kadhaa.

Katiba mpya itaondolea mbali wamisri katiba aliyoipitisha Morsi na iliyokuwa serikali yake kabla ya jeshi kuwaondoa mamlakani.

Jeshi linataka watu waipigie katiba hiyo kura ya ndio katika shughuli hiyo itakayaoendelea wa siku mbili.

Vuguvugu la Muslim Brotherhood ambalo limetajwa kuwa kundi la kigaidi limesusia kura huyo ya maamuzi.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company