Obama kukutana na viongozi 50 wa Afrika

Rais wa Marekani, Barack Obama
White House inasema Rais wa Marekani Barack Obama atawaalika viongozi takribani 50 wa serikali za barani Afrika kushiriki mkutano wa mwezi Agosti mjini Washington.
Naibu msemaji wa White House, Jonathan Lalley anasema bwana Obama atawajumuisha wakuu wote wa nchi au serikali za bara la Afrika ukiwatoa wale ambao hawana uhusiano mzuri na Marekani au waliosimamishwa kwa muda uanachama na Umoja wa Afrika-AU.

Lalley anasema mwenyekiti wa AU, Nkosazana Dlamini-Zuma pia ataalikwa kwenye mkutano ambao unafanyika Agosti tano hadi sita. White House ilitangaza mkutano huo jumanne ikisema Marekani itautumia kuimarisha ushirikiano wa biashara na uwekezaji na bara la Afrika.

Maafisa wanasema bwana Obama pia anamatumaini ya kujenga mafanikio yaliyopatikana tangu ziara yake ya mwezi Juni mwaka 2013 barani afrika. White House inasema nchi ambazo zitapokea mialiko ya mkutano wa Agosti ni pamoja na Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo-DRC, Ethiopia, Sudan Kusini, Mali na Nigeria.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company