HABARI KUU ZA LEO na OSCAR SAMBA
print this page
HABARI NA Oscar Samba
Showing posts with label INJILI. Show all posts
Showing posts with label INJILI. Show all posts

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

Mahali: TAG Ushiri Rombo: Tarehe 28:2:2019. Na Mwalimu Oscar Samba.
.

Mwanzo 2:18 Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.
Mwanamke ni msaidizi, andiko hilo lipo kabla ya dhambi kuingia ulimwenguni, hakukuwa na mfumo wa kanisa ama kuabudu kama leo, au kama baada ya dhambi, kusudio la ndoa, au familia ni ili liwe kanisa, yaani tuliumbwa kwa ajili ya ibada !

Kwa hiyo, kanisa, lina mukutadha wa ndoa, kwa hiyo, dhima ya mwanamke kindoa au kifamilia, ina mashabihiano na ile ya kikanisa !

Waefeso 5:23 Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili.
24 Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.

Kama ndivyo, mwanamke ameumbiwa kulichukulia kanisa kama anavyomchukulia mumewe, utendaji wa usaidizi kwa mume, ama kumuheshimu, uwe vivyo hivyo kwa kanisa, maana Kristo u kichwa huku.
Kumbuka hili Daima: Kuwa ni yule amchaye Mungu ndie asifiwaye: Mithali 31:30 Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; Bali mwanamke amchaye Bwana, ndiye atakayesifiwa.

Jambo hili, likupe kuhakikisha una sifa ya uchaji, kama kweli unadhamiria kusifiwa na Kristo ambaye ndie kanisa, na hakika ukijipatia kibali au sifa njema kutoka kwa Bwana Yesu, ni umejipatia kutoka kwa kila mtu, jifunze kwa wakina Debora,Dorkasi, na wengine akiwemo yule Mariamu aliyempaka yale mafuta, hadi leo tukio hilo lingali likikumbukwa, sasa utafahamu kuwa utendaji wao mwema uliotokana na uchaji ndio uliopeleke kujizolea sifa hizo.

Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili ! Kwa hiyo ni hatari mno kujisifia vya mwilini, ila sifa zitokane na uchaji, ambao huzaa kazi njema !
MAJUKUMU YAKE KATIKA NAFASI KWENYE KANISA:

1.  Ni Mueneza Habari Njema, sifa njema kuhusu Mchungaji wake, kanisa lake, huduma ya kanisani, watumishi wa kanisani, na kila wasifu mzuri kulihusu.

Ni jukumu lake pia kumuelezea Kristo Yesu kwa wasio mjua, huyu ni mjumbe mzuri sana, maana mwanamke amepewa kinywa chenye uwezo wa kuzalisha maneno mengi, adui amekuwa akiwahi hili na kulitumia vibaya kwa umbea na misuto, ukizingatia pia amepewa uwezo wa kutoka mji huu ama nyumba hii na kwenda kwa ile, nia ni ili aeneze mema, ila adui amewatumia vibaya.

Mfano wa dhima hii kibiblia ni mwanamke yuke wa kisima cha Yakobo Msamaria: ( Yoh 4:7-42.) 

Alipofahamu uzuri wa Yesu, moja kwa moja aliacha mtungi wake na kwenda kueneza wema wake!

Yohana 4:28 Basi yule mwanamke akauacha mtungi wake, akaenda zake mjini, akawaambia watu.

Kuna wakina mama au mabinti unakuta anafua nguo,au kukatakata kitunguu jikoni, ghafula huepua sufuria na kwenda mbio kwa jirani baada ya kusia umbea fulani, huku ni kukosa kujitambua ! Akisikia neno mbio ataaga na kutoka kanisani mapema utazani anawahi mtoto nyumbani, kumbe kuna sumu anaenda kumwaga kwa mpendwa ambaye hajaja kanisani. 

Huyu Msamaria, kaacha mtungi, na kwenda kueneza habari za Yesu, wewe je unaacha na kwenda kueneza nini? Aibu ya kanisa, udhaifu wa mama mchungaji wako, udhaifu wa kiongozi wako wa idara, ama unapeleka madhaifu ya kikanisa kwa wapendwa na mbaya zaidi hata kwa wasio wapendwa yaani kwa watu wa mataifa ! Ila huyu, hakufanya hivyo!

Nisikilize, hakuna mtumishi aliyekamilika, wapo mbinguni, hakuna kanisa lililokamilika, hoja ni pale unapoona madhaifu unafanya nini? Unapaswa kuomba, ukiona doa kwenye koti langu, kachukuwe sabuni na maji uliondowe, sio kulipiga picha na kusambaza doa langu, hujanisaidia, na ukitangaza aibu ya mtumishi ni umeanika aibu ya Yesu, huko ni kulivua nguo kanisa, na kanisa ni Kristo, uwe na uhakika adhabu inakuhusu siku ile ya mwisho ! Jifunze sana kwa huyu mwanamke, nawe uwe ni mueneza habari njema kwa majirani zako, marafiki, usikubali kukaa nao na kujadili yasiyofaa, bali mjadili mema, mkiongea kumi kuhusu VIKOBA, na VIBATI, au mchezo wa fedha,basi wewe weka hapo mawili ya Yesu, anza tu stori kuwa nilipokuwa sijaokoka jamani nilikuwa na sumbuliwa na hili au lile, ila toka nimeokoka, naona nimepokea mujiza, usishangae jirani yako akikwambia, jamani nipelekeni na mimi hapo !

Ama, mchungaji wetu akikuombea, Mungu aliyeko ndani yake atakufungua haraka sana, hapo unafahamu kuna mgonjwa, hata kama hatatoa jibu muda huo uwe na hakika kuwa punde, au baada ya muda, Kuna siku atakutafuta tu, maana ulipanda mbegu, maneno ni mbegu !
(Mithali 6:19 Shahidi wa uongo asemaye uongo; Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu.)

Sasa ikupe kujiuliza sana, huwa unapanda mbegu ipi uwapo kanisani, au na wapendwa, kama unamsema vibaya mchungaji, au kanisa, ama mpendwa, uwe na hakika, unapanda pando baya, na apandaye magugu ni mwana wa Ibilisi !

Tuendelee na utendaji wa mwanamke huyu, aliyemtengenezea Yesu mazingira mazuri ya kuifanya kazi yake !

Yohana 4:29 Njoni, mtazame mtu aliyeniambia mambo yote niliyoyatenda. Je! Haimkini huyu kuwa ndiye Kristo?
Na wewe tafuta ulilotendewa na Yesu, lipo, ( Kila aliye na Mwana hakosi ushuhuda, kama huna, tazama vyema kiroho chako kama kweli unaye Mwana !)

30 Basi wakatoka mjini, wakamwendea.
39 Na katika mji ule Wasamaria wengi walimwamini kwa sababu ya neno la yule mwanamke, aliyeshuhudia kwamba, Aliniambia mambo yote niliyoyatenda.

40 Basi wale Wasamaria walipomwendea, walimsihi akae kwao; naye akakaa huko siku mbili.
:41 Watu wengi zaidi wakaamini kwa sababu ya neno lake.
42 Wakamwambia yule mwanamke, Sasa tunaamini, wala si kwa sababu ya maneno yako tu; maana sisi tumesikia wenyewe, tena twajua ya kuwa hakika huyu ndiye Mwokozi wa ulimwengu.

Yesu alikuwa na kazi nyepesi sana huku, hakukuwa na haja ya kulipia matangazo ya mkutano, au kusambaza vipeperushi, maana kuna mtangazaji, na msemaji wake, alimtangulia, nawe una hiyo dhima, hakikisha unatumia vyema nafasi hii!

Kumbuka hili siku zote, kuwa Mungu asiponufaika na alichoweka ndani yako, basi adui atakitumia, huamini, acha kumsema Yesu, usipojikuta unawasema watu ! Kanisani utakuwa mkosoaji na kuchambua mabaya kana kwamba hakuna jema hata moja, kiongozi wa migomo baridi ni wewe, mbeba maneno utakuwa ni wewe, kwa nini, chai iliyopoa au supu, ndipo nzi hutua ! Kama kinywani mwako Yesu habebwi, Ibilisi atabebwa, utashangaa kila baada ya maneno yako unasema lakini tumuombee, lakini kiukweli huwa hauombi ! 

2. Ni Muombaji; Yohana 2:3 Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai.
4 Yesu akamwambia, Mama, tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia.
:5 Mamaye akawaambia watumishi, Lo lote atakalowaambia, fanyeni.

Sijajua ni kwa nini, ila wanawake wamepewa nafasi ya maombi yao kuwa na wepesi na kibali cha haraka sana, labla kwa kuwa ndani yao uombolezaji ni mwepesi zaidi, ila ninachonuia kukwambia hapa ni kwamba uonapo tatizo au upungugufu kanisani, sio muda wa vikao, na kuchambua, bali ni muda wa kufanya maombi, au dua, ama toba, lishike hili siku zote !

3. Ni Chanzo cha Utatuzi wa Migogoro au Matatizo Sugu maana amepewa Busara na Hekima; Mfano 1, Abigaeli; ( 1 Samweli 25:4-35.)
1 Samweli 25:23 Ndipo hapo Abigaili alipomwona Daudi, alifanya haraka kushuka juu ya punda wake, akamwangukia Daudi kifulifuli, akainama mpaka nchi.

24 Akamwangukia miguuni pake, akasema, Juu yangu, bwana wangu, juu yangu mimi na uwe uovu; tafadhali mjakazi wako na anene masikioni mwako, nawe uyasikilize maneno ya mjakazi wako.

25 Nakusihi, bwana wangu, wewe usimwangalie huyu mtu asiyefaa, yaani, Nabali; kwa maana kama lilivyo jina lake ndivyo alivyo yeye; jina lake ndilo Nabali, na upumbavu anao; lakini mimi, mjakazi wako, sikuwaona hao vijana wa bwana wangu aliowatuma.

32 Naye Daudi akamwambia Abigaili, Na ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye amekuleta hivi leo kunilaki;

33 na ibarikiwe busara yako, na ubarikiwe wewe, uliyenizuia hivi leo nisimwage damu, wala kujilipiza kisasi kwa mkono wangu mwenyewe.
Mfano 2, Kisa cha Seba aliyemuasi mfalme Daudi ! 

Baada ya tukio hili, Yoabu alinuia kuleta maangamizi makubwa kwa mji wao wote, na tayari alishaanza kuuvunja ukuta, nasi twafahamu huluka ya Yoabu, katika hiyo sura tu alikuwa ametoka kumuangamiza mtu kwa kukita upanga tumboni mwake, Abineli aliuawa naye, japo alikuwa ameshatengeneza, pia Absolum aliuawa, japo mfalme aliachilia rai ya kumtaka aishi ! Kwa hiyo, sio ajabu kuwa mji huo,ungedhuriwa !

Ila kwa hekima ya huyu mwanamke atwajaye kama mwenye akili, huku biblia nyingine za kingereza na zile za kiswahili rahisi kutumia neno mwenye busara,aliweza kuuokoa mji huo, sasa kanisa likiwa na mama mchungaji makini, na mumewe kujua kumtumia vyema, kwa kumsikiliza na kumpa nafasi, uwe na uhakika atafanikiwa kupindua maamuzi ambayo yangeweza kuleta madhara kwa kanisa, kama Abigaili na huyu waliweza, ni fika hata wewe wa weza !

Kuna ina fulani ya hekima, na busara, na uwezo wa ushawishi waliopewa wanawake, sasa adui akiuwahi, hapo huzalisha wakina Delila,ila Kristo kiuwahi, huzalisha wakina Abigaili, sijui wewe u wapi, au umempa nafasi adui au Kristo Yesu ! 
Tuuone mfano wetu : 

2 Samweli 20:15 Na hao wakaja wakamhusuru katika Abeli wa Bethmaaka, wakafanya chuguu mbele ya mji, nayo ikasimama kuielekea ngome; na watu wote waliokuwa pamoja na Yoabu wakavunja-vunja ukuta, wapate kuubomoa.

:16 Ndipo akalia mwanamke mmoja mwenye akili toka mjini, Sikieni, sikieni; mwambieni na Yoabu, aje hapa karibu, niseme naye.
:17 Basi akamkaribia; na yule mwanamke akasema, Ndiwe Yoabu? Akajibu, Ndimi. Ndipo akamwambia Sikia maneno ya mjakazi wako. Akajibu, Mimi nasikia.

18 Kisha akanena, akisema, Watu hunena zamani za kale, wakisema, Wasikose kuuliza huko Abeli; ndivyo walivyomaliza shauri.
:19 Mimi ni wa hao wenye amani, walio waaminifu katika Israeli; wewe unatafuta kuuharibu mji, na mama wa Israeli; mbona wataka kuumeza urithi wa Bwana?

:20 Yoabu akajibu, akasema, Isiwe, isiwe kwangu, niumeze wala kuuharibu.
21 Neno hili silo hivyo; lakini mtu mmoja wa milima ya Efraimu, Sheba, mwana wa Bikri, jina lake, ameinua mkono wake juu ya mfalme, naam, Daudi, basi mtoeni yeye tu, nami nitaondoka katika mji huu. Basi yule mwanamke akamwambia Yoabu, Tazama, kichwa chake utatupiwa juu ya ukuta.

:22 Ndipo yule mwanamke akawaendea watu wote katika akili zake. Nao wakamkata kichwa Sheba, mwana wa Bikri, wakamtupia Yoabu huko nje. Ndipo akapiga tarumbeta, nao wakatawanyika kutoka mjini kila mtu hemani kwake. Naye Yoabu akarudi mpaka Yerusalemu kwa mfalme.

Mwanamke ! Mumeo akiwa mkali, akiwa na hasira kama simba, ni hatari wewe ukiwa kama mbuzi, ila ukiwa kama kondoo, utafanikiwa kuituliza, huyu mwanamke kama naye angeinuka na kujibizana, hakika angechochea ghadhabu ya Yoabu, ila alitumia busara, sasa wanawake wengine, nao hupanda juu, hawajui Mithali 15:1 husemaje ? Kuwa jibu la upole hutuliza hasira, ila la kinyume chake huchochea !
Biblia nyingi za kingereza zimetumia neno ulimi laini, au mzuri, kwa hiyo, ukitaka kutenda vyema, dhidi ya mumeo mwenye hulika kama ya Yoabu, hakikisha unakuwa na ulimi laini, maana hata vyuma bila mafuta husagika.

Akikuudhi na wewe ukisema naenda kwetu, usishangae akiwa wa kwanza kukutolea begi nje!

Sio kwamba hakupendi, ila umechochea ghadhabu, ndio maana ukiondoka, baada ya siku mbili tatu, anakufuata, hapo uwe na hakika, hasira imeisha ! Sasa unaweza kuituliza kwa akili, sio kwa kushindana, huyu mwanamke na Abigaili wawe ni somo tosha kwako !

Muone Ambaye anatumiwa na Ibilisi, ni Mvunjaji, ni mbomoaji, nyundo, huweza kujenga ikitumiwa katika dhamira hiyo, ila ikitumiwa vibaya hubomoa pia, kwa hiyo chombo hakina shida, mtumiaji ndie mwenyewe shida: Kwa hiyo kama kuna mwanaume anaoma huu ujumbe, ajuwe sasa kumuombea mwenzie ! Na kama ni mtumishi, ukiwa na wanawake waharibifu, jifunze kuwabadili au kubadili nia zao kupitia maombi na mafundisho !

Mithali 14:1 Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.

Ona hapa: 

Mithali 27:15 Kutona-tona daima siku ya mvua nyingi, Na mwanamke mgomvi ni sawasawa;

Oanisha na : Mithali 19:13 Mwana mpumbavu ni msiba kwa babaye; Na ugomvi wa mke kama kutona-tona daima.

4. Hutunza Watumishi; 1. Yule Mshunami; 2 Wafalme 4:9 Yule mwanamke akamwambia mumewe, Tazama, mimi naona ya kuwa mtu huyu apitaye kwetu mara kwa mara ni mtu mtakatifu wa Mungu.

10 Nakuomba, tumfanyie chumba kidogo ukutani; na ndani yake tumwekee kitanda, na meza, na kiti, na kinara cha taa; na itakuwa, atujiapo, ataingia humo.

Kuna mzigo wa kipekee ambao Mungu ameweka kwa wanawake kuhusu kuwahudumia watumishi, na kanisa lenye wanawake wenye kujitambua kama hawa, moja kwa moja, hutimiza dhima hii vyema sana !

Mfano 2, Mwanamke wa Serepta, 1 Wafalme 17: 10-16. 

Mfano 3, Enzi za Yesu, japo hata kwa Paulo Mtume ama kqnisa la kwanza walikweo wakina Lidia, tumuone Yesu; 

Luka 8:2 na wanawake kadha wa kadha ambao walikuwa na pepo wabaya na magonjwa wakaponywa; nao ni Mariamu aitwaye Magdalene aliyetokwa na pepo saba,

3 na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, na wengine wengi, waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao.

Yesu alihudumiwa kwa mali zao, wewe jiulize, mtumishi wako unamuhudumia kwa mali zako ! Na Yesu wa leo ni huyo mlawi wako, ama mtumishi wake !

Na kama hujaokoka na unataka kufanya hivyo sasa tafadhli kwa imani kubwa nakuu kabisa fuatisha pamoja nami maneno haya, au sala hii ya toba ili uweze kuokoka, Sema;

BWANA YESU, NIMETAMBUA KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NATUBU MBELE ZAKO LEO, NISAMEHE NA NINAKUOMBA UFUTE JINA LANGU KWENYE KITABU CHA HUKUMU, TAFADHALI LIANDDIKE KWENYE KITABU CHA UZIMA, NINAKUKIRII NA KUKUPOKEA MOYONI MWANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, HAKIKA WEWE NI MUNGU NA ULIFUFUKA KATIKA WAFU, Amen.

Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo, kwa maombi, sadaka kwa njia ya M-Pesa, kupiga simu au Wasats App, ni +25559859287. Tupo Arusha Tanzania.
0 Toa maoni yako.

MAANA YA MBEGU ILIYODONDOKA KANDO YA NJIA

HABARI ZETU
Mahali: TAG Ushiri, Rombo:     Tarehe 27/2/2019, Na Mwalimu Oscar Samba

Mathayo 13:3 Akawaambia mambo mengi kwa mifano, akisema, Tazama, mpanzi alitoka kwenda kupanda.
4 Hata alipokuwa akipanda, mbegu nyingine zilianguka karibu na njia, ndege wakaja wakazila;
( Luka, zikakanyagwa:Luka 8:5 Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake; naye alipokuwa akizipanda, nyingine zilianguka karibu na njia, zikakanyagwa, ndege wa angani wakazila.)
19 Kila mtu alisikiapo neno la ufalme asielewe nalo, huja yule mwovu, akalinyakua lililopandwa moyoni mwake. Huyo ndiye aliyepandwa karibu na njia.
Kwa hiyo, kutokulielewa neno, huifanya mbegu hiyo kukosa makao mazuri moyoni mwa muhusika, maana hapo huambiwa yule asikiaye, lakini asielewe yu sawa ama ndie aliyepandwa kando au pembezoni mwa njia, ambapo adui huja na kulitwaa hilo neno, ama kukanyagwa na kuharibiwa.
Maana ya Mbegu: Mbegu ni Neno la Mungu, mpanzi ni Muhubiri, ama Roho Mtakatifu moja kwa moja, au kumpitia mjumbe wake aliye Mtumishi wake;
Luka 8:11 Na huo mfano, maana yake ni hii; Mbegu ni neno la Mungu.
Shamba ni Moyo: Luka 8:12 Wale wa karibu na njia ndio wasikiao, kisha huja Ibilisi akaliondoa hilo neno mioyoni mwao, wasije wakaamini na kuokoka.
Kama huondolewa moyoni, maana yake lilipandwa hapo, kwa hiyo, kama mbegu ni neno, na moyo ni shamba, kwa mantiki hiyo mahubiri, au mafundisho hupandwa moyoni mwa muhusika.
Zile aina za mahali mbegu zilidondokea, yaani njiani, penye udongo mchache, penye miiba, na udongo mzuri, maana yake ni aina ya mioyo ya watu wanaolisikia neno la Mungu.
Mpanzi au mkulima apandapo, ili mbegu iwe imedondokea sehemu ipi, ni matokeo ya moyo ulio nao, kwa hiyo ukitaka kuwa na mafanikio, ni lazima kuhakikisha unajitengenezea moyo mzuri, ili neno lijapo, lidondoke mahali sahihi.
Kusudi la Mungu Kukutaka Mbegu yake Isipandwe kando ya Njia.
Kumbuka sana kuwa Mungu kama mkulima hataki au hapendi kupanda njiani, ila mazingira ya moyo wako ndio huifanya mbegu kuelekea hapo !
1. Ili Kuua na Kuuhuisha; Yohana 12:24 Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi.
25 Yeye aipendaye nafsi yake ataiangamiza; naye aichukiaye nafsi yake katika ulimwengu huu ataisalimisha hata uzima wa mikulala
26 Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu.
Kitu neno hufanya ni kuua aina fulani ya maisha yasiyo ya Kiungu, na kuhuisha yaliyo sahihi, Warumi hutuambia vyema kuwa kufa kwa Yesu ni kuua mwili wa dhambi na kufufuka ndimo mlimo na mantiki ya kufufua utu mpya.
Mungu akitaka kuua visivyo vya kwake kwako, na kuhitaji kuhuisha vya kwake, huliachilia neno lake, au mbegu yake, sasa ikianguka mahali sahihi, ndipo hufanikiwa sana, unaposikia alikuwa mwizi na kuacha, maana yake, alipokea neno lililouwa wizi na kuhuisha uadilifu,ambao ni tunda la Kristo.
2. Kukufanya Uzae, na Huwezi zaa kama mazingira sio rafiki kwa uzalishaji, mfano wa mazingira rafiki;
Mathayo 13:23 Naye aliyepandwa penye udongo mzuri, huyo ndiye alisikiaye lile neno, na kuelewa nalo; yeye ndiye azaaye matunda, huyu mia, na huyu sitini, na huyu thelathinhuu.
Kwa hiyo, ukihitaji kuwa na utumishi wenye mafanikio kwako, kuhakikisha kuwa unajiwekea mazingiira mazuri ya kupokea neno la Mungu linalonuia kukubadilisha kitumishi ni muhimu sana, ukihitaji kufanikiwa kimaisha, ni shariti moyo wako uwe na mazingira rafiki katika uzalishaji wa matunda na  hauwezi zaa, kama mbegu haijamea, ikidondoka njiani, haitamea, ya udongo haba au juu ya mwamba, itanyauka yakija mpito, na ile iliyosongwa haiwezi kuivisha kama Luka isemavyo.
Ujumbe huu ni jibu tosha na muhimu sana kwa yule anayehitaji kufanikiwa, au kustawi kihuduma, kimaisha, na kuwa mti mkubwa kama ufalme wa mbinguni ufafanuliwavyo, wengi hutamani sana kufanikiwa kihuduma, ila kuna mahali wamekwama, ambapo ni hapa, mfano utakaouona hapo mbeleni wa mti ulioanza na mbegu ndogo na kisha kupanuka na kuzaa,na ndege kukaa juu yake, ni muhimu kujua kuwa, asili yake ni mbegu, ila sio iliyodondoka njini, wala kusongwa, wala juu ya mwamba, bali ni ile ya udongo au moyo mzuri, kwa hiyo, nawe ukihitaji kufanikiwa katika jambo fulani ni lazima kujua au kuijua hii Kanuni !
Nakupa tena maandiko kuhusu dhima ya mbegu, katika kuuwa na kuhuisha kitu fulani, maandiko haya yakupe kuhakikisha unanufaika vilivyo na neno la Mungu, kama kuna vitu ndani yako huvitaki, na untaka vichipuke vya kiungu, maandiko haya hunena habari za nyakati za mwisho kuhusu kubadilishwa kwetu, ila hapa nataka ujionee thana ya mbegu, na ili iwe na matunda lazima ife, kufa ni kubadilika, kutoka katika mbegu, na kutoa mche, neno la Mungu lililopo kwenye biblia halina matunda hadi liingie moyoni mwako, na kuanza kuzalisha mabadiliko! Mbegu ambayo haijafa,ni mbegu, sasa hatutaki mbegu, tunataka matunda, na ili tuyapate ni lazima tupande, kisha imee, sasa wengi kiroho hutaka mbegu, ila kubadilishwa au kuiruhusu, ama kuipa nafasi ili iwabadilishe, kisha wawe na matunda hawataki, atakuwa ni mkulima wa ajabu sana ambaye ataishilia kununua mbegu, ila hataki mazao ! Na ndivyo wakristo wengi walivyo leo, husoma sana neno, huenda sana kanisani, ila hawairuhusu injili iwabadilishe! Usizini, usiibe, wahi kanisani, uwe mtoaji, toa zaka kamili, ila bado wako pale pale, hawaruhusu neno hilo, kuingiza mabadiliko mapya ndani yao, tujionee maandiko !
(1 Wakorintho 15:35 Lakini labda mtu atasema, Wafufuliwaje wafu? Nao huja kwa mwili gani?
36 Ewe mpumbavu! Uipandayo haihuiki, isipokufa;
:37 nayo uipandayo, huupandi mwili ule utakaokuwa, ila chembe tupu, ikiwa ni ya ngano au nyingineyo;
:38 lakini Mungu huipa mwili kama apendavyo, na kila mbegu mwili wake. )
Kumbuka/ Fahamu: Mungu ni Mpanzi, na Shetani naye ni Mpaanzi, kwa hiyo moyo wako usipopandwa mbegu njema, utapandwa mbaya, na nia ya mbegu njema, ni Ufalme wa Milele;
(1 Petro 1:23 Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima, lidumulo hata milele. )
Mungu alipoiumba dunia, alipanda pando jema, adui akaja, baada ya kulala kwa Adamu, akapanda pando baya, hii ikupe kuenenda kwa umakini humu ulimwenguni;
Mathayo 13:24 Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;
:25 lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
:26 Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.
27 Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu?
Ukindelea mbele ya hayo maandiko utapata kujua kuwa magugu yanatakiwa kuachwa hadi siku ya mavuno, kwa hiyo inawezekana nawe katika kwaya, au utumishi ama kanisani u gugu, ila bado umeachwa haimaaniishi parapanda ikilia nawe utakuwa mawinguni, la!
Bali utaingia jehanum ya moto, hekima ya kuachwa kwa magugu haikupi kuingi mbinguni, maana siku ya mavuno, itachambuliwa ngano na kufungwa matitamatita, kisha kuwekwa ghalani, na magugu nayo yatafungwa, ila yatatupwa motoni, na huko ndimo mlimo kilio na kusaga meno, sasa hii ikupe kutengeneza na Bwana, yaani uruhusu mbegu njema, ambapo mimi kama mpanzi kwa uweza wa Mpanzi Mkuu, ninanuia kupanda moyoni mwako leo, au majira haya, ili sasa pando jema liwe ndani yako, na kuuwa kila pando baya, yaani ufisadi, ulafi, uasherati, wizi, matukano, kiburi, dharau na kadhalika.
3. Kumbuka Hauwezi Kufika Hapa kama Mbegu yako haikupandwa Sehemu sahihi; Mathayo 13:31 Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na punje ya haradali, aliyoitwaa mtu akaipanda katika shamba lake;
32 nayo ni ndogo kuliko mbegu zote; lakini ikiisha kumea, huwa kubwa kuliko mboga zote, ikawa mti, hata nyuni wa angani huja na kukaa katika matawi yake.
Ni dhairi kuwa ukihitaji kuinuliwa, au kupanuka kimaisha na kiroho, na kihuduma, ni lazima kuhakikisha kuwa moyo wako una mazingira sahihi katika kulipokea, na kulitunza neno la Mungu, mkulima makini huliandaa shamba vyema na kulitilia mbolea, nawe kama Mkristo makini, hakikisha moyo wako ni uliopondeka.
Isaya 66, hutuambia kuwa mtu ambaye akilisikia neno la Bwana hutetemeka, huyo ndiye Mungu humuangalia, kwa maana kwamba huyu mtu moyo wake, u na mazingira mazuri, akionywa huonyeka, akihaswa huzingatia, iwe hivyo kwako !
Madhara ya Kupandwa Kando ya Njia, au Nia ya Adui Anapoweka Mazingira moyoni mwa mtu ili Neno lipandwe kando ya Njia:
Kuna vijitabia ambavyo Shetani huvitumbukiza ndani ya moyo wa mtu, na wengi hawajui ni kwa nini ! Nia yake ni kumuwekea muhusika mazingira ya mbegu au neno alisikialo lisidondoke sehemu sahihi !
Mathalani kiburi, huyu mtu asikii maonyo, asikii mahusia, maana njia yake imenyooka machoni pake mwenyewe, ikiwa na maana kwamba kile akiwazacho, akionacho, akipangacho hukiona ni sahihi hata kama atashauriwa, kwenye kiburi kuna upumbvu, pia ujinga, ukija katika Obadia 1:3-4, utagundua kuwa kiburi pia hudanganya, yaani hupotosha, kwa hiyo kitamuaminisha kuwa njia hii ni sahihi, wazo hili ni sahihi, kama ilivyokuwa kwa mfalme Sauli, maana kiburi kilimpa kujiamini hata kama Mungu atakuwa amemuacha, maana kii na mbinu na tabia ya kudanganya, mtu hujiona yu salama kumbe sivyo !
Mazingira mbayo ni hatarishi sana kwa Neno kuweza kuchipusha linalotakiwa kuhipusha !
1. Ili Aweze Kuinyakuwa, au kuiharibu, ama Kuizuilia Isichipuke: Luka 8:12 Wale wa karibu na njia ndio wasikiao, kisha huja Ibilisi akaliondoa hilo neno mioyoni mwao, wasije wakaamini na kuokoka.
Unapohubiri na mtu kusema ananisema, au moyoni mwake kuwa na mawazo mengine, kimawazo kuwa mbali ama kiakili,ama anapofanikiwa kubana akili ama fikra zake, au ufahamu wake ili asielewe, uwe na uhakika kuwa baada ya mahubiri, au neno hilo, adui huja na kulinyakuwa, ama hukanyagwa !
2. Ananuia Kukuzuilia Kunufaika na Kile Kilichokusudiwa na Mpanzi; Yohana 12:40 Amewapofusha macho, Ameifanya mizito mioyo yao; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakafahamu kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya..
Wakati wakina Bartomayo kipofu wakipokea miujiza yao, Mafarisayo, haikuwa hivyo kwao, hakuna mahali wananufaika na injili yaa Yesu isipokuwa Nikodemu aliyejua kuweka kiburi cha kidini na elimu pembeni na kukubali kunyenyekea, sio kwamba hawakuwa na mahitaji la! Walikuwa nayo, ila tatizo ni mioyo yao kugoma kuipokea hiyo mbegu !
Sasa maandiko hayo hutuambia kuwa ni ili wasije wakapokea nuru ama mwanga kisha kuweza kuponywa na Kristo Yesu, kwa hiyo, unapohubiri na watu kutema chakula, maana yake, adui amefanikiwa kuwazuilia kubadilishwa na hilo neno, dalili kubwa ya mtu ambaye mbegu haijadondoka njiani ni mabadiliko yake, ukiwa na mshirika asiyebadilika, kuwa makini na shamba upandalo mbegu, kama hana kiburi, sio mwenye madharau, na mkataa maonyo, basi ombea ufahamu wake, maana kuna namna umefungwa,katika mpanzi huambiwa kuwa mtu anapolisikia hilo neno na kushindwa kulielewa hapo ndipo huja adui na kulinyakuwa, kwa hiyo adui akifanikiwa kuzuilia au kubana uekewa wako ama wake uwe na uhakika amezuilia jambo kubwa sana.
Katika kitabu chetu cha IJUWE HUDUMA YA UINJILISTI, nimewataka wainjilisti kuhakikisha kuwa wanaombea hii mioyo, yaani wanaandaa hili shamba vyema, ila katika upandaji, waweze kupanda mahali sahihi, hakuna mpanzi atakaye kupanda njiani, ama mahali pasipo mzalia matunda !
Sasa wachungaji, na wale wanaombea ibada, ni lazima sana kujifunza kuelewa usikiaji wao, fahamu zao, kama akikamata fikra, ama mioyo yao na kuitia uzito hufanikiwa kuwazuilia kupata wokovu, basi wewe ombea hizo fikra ziangushe hizo ngome za mawazo mbaya, na kila fikra zijiinuazo kinyume na elimu ya Kristo, kisha zitiishe, hii ni siri kubwa sana,hakikisha unaombea usikiaji wao, maana hapo ndipo adui huwekeza sana, ndiposa wakati wa ibada hujitahidi sana kupambana na usikiaji wao, asipoamisha mawazo, basi atafinya hata mtoto ili aliye, kwa nia ya kuondoa usikivu !
3.
Mazingira Rafiki na Hatarishi kwa Mbegu:
1. Roho na Tabia ya Kupuzia Maonyo, au Mahubiri, ama Mafundisho, ama Makaripio: Mithali 1:28 Ndipo watakaponiita, lakini sitaitika; Watanitafuta kwa bidii, wasinione.
29 Kwa kuwa walichukia maarifa, Wala hawakuchagua kumcha Bwana.
30 Hawakukubali mashauri yangu, Wakayadharau maonyo yangu yote.
31 Kwa hiyo watakula matunda ya njia yao, Watashiba mashauri yao wenyewe.
32 Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua, Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza.
33 Bali kila anisikilizaye atakaa salama, Naye atatulia bila kuogopa mabaya.
Kuna Hatari ya Kupotea, na hata Kufa: Mithali 5:23 Atakufa huyo kwa kukosa maonyo, Naye atapotea kwa wingi wa ujinga wake.
Suluhu lake: Tilia Moyoni, Luka 2:49 Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu?
50 Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia.
:51 Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake.
Mamaye na Yesu, hakuwa kama wengine, alitilia moyoni, hapo ukiniuliza sababu ya wengine kutokutilia moyoni, nitakwambia i katika huo mstari wa 50, kwamba hawakuelewa, sasa utaniele ni kwa nini adui huhakikisha kuwa watu wakisoma biblia hawaelewi, wakisikiliza mahubiri hawaelewi, huishilia kusema kile kitabu ni kizuri, somo alihubiri visuri, ila mulize alichoambulia hapo, hana! Anachokumbuka ! Labla kichekesho ama kitu kilichomfanya ama kuwafanya kucheka! Hii ni hatari sana.
Sasa ikupe kuhakikisha unapoonywa, unapokatazwa, unatilia moyoni unayoambiwa, unaposikiliza neno na kugundua dosari yako hapo, kinachotakiwa kufuata ni mabadiliko, ukisikia injili ya onyo kwa wasiotoa zaka,moja kwa moja anza kutubu, kisha msihi Mungu akuumbie tabia na mwenndo mpya, sasa huyu ndiye anayeitwa kuwa humfurahisha Mungu, ama ndiye mtu ambaye Mungu humtazama, tumuejionea kwenye Mithali hapo juu kuwa wapo wamuitao, ama wamtafutao kwa bidii ila hawamuoni, maana wamekataa maarifa, na sababu ni kudharau monyo, sasa leo tuna waombaji wazuri sana, wanataka kumuona Mungu kwenye jambo fulani, ila hawajui kuwa ameshagoma kuwasikiliza maana alinyoosha mkono hawakuutazama, wanamtafuta kwa bidii ila kauficha uso wake kwa maana walikwepa maonyo !
( Kutilia Moyoni ni Kuhifathi: Mwanzo 37:11 Ndugu zake wakamhusudu; bali baba yake akalihifadhi neno hili.)
Ona Mukutadha wa Kutokutilia Moyoni hapa: Isaya 42:18 Sikilizeni, enyi viziwi; tazameni, enyi vipofu, mpate kuona.
19 Ni nani aliye kipofu, ila mtumishi wangu? Au aliye kiziwi, kama mjumbe wangu nimtumaye? Ni nani aliye kipofu, kama yeye aliye na amani? Naam, kipofu kama mtumishi wa Bwana?
20 Unaona mambo mengi, lakini huyatii moyoni; masikio yake ya wazi, lakini hasikii.
Pili Kubali kuonywa; Kusudi la Maonyo ni Kukugeuza: Mithali 1:23 Geukeni kwa ajili ya maonyo yangu; Tazama, nitawamwagia roho yangu, Na kuwajulisheni maneno yangu.
24 Kwa kuwa nimeita, nanyi mkakataa; Nimeunyosha mkono wangu, asiangalie mtu;
:25 Bali mmebatilisha shauri langu, Wala hamkutaka maonyo yangu.
Nia na kusudio kubwa la maonyo ni kukugeuza, kama huo mstari wa 23 uanzavyo, ni sawa na mtu anayetaka kuelekea uwanja wa ndege wa KIA, ila kapanda gari la kuelekea Dar es salam, na kashafika Tanga, anaulizwa na mtu unaenda wapi, KIA, anaambiwa kuwa umepeotea, geuka,anagoma, sasa ni sawa na mtu anayeonywa, kuwa ukitaka kufanikiwa kielimu, achana na ngono, ukitaka kufaulu, acha kiburi, ila bado ni jeuri, baada ya muda, hujikuta amepotea, ila akisiliza, hugeuka, na hapo huelekea njia iliyo salama !
Kuna mahali maonyo hukuelekeza na kukuwezesha kufika, maana ni njia;
Mithali 6:23 Maana maagizo hayo ni taa, na sheria hiyo ni nuru, Na maonyo ya kumwadilisha mtu ni njia ya uzima.
Maonyo kuna kitu yamebeba, ukiyakubali, huweza kunufaika na kilichobebwa nayo, mfano hekima; Mithali 29:15 Fimbo na maonyo hutia hekima; Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.
Na kama hujaokoka na unataka kufanya hivyo sasa tafadhli kwa imani kubwa nakuu kabisa fuatisha pamoja nami maneno haya, au sala hii ya toba ili uweze kuokoka, Sema;

BWANA YESU, NIMETAMBUA KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NATUBU MBELE ZAKO LEO, NISAMEHE NA NINAKUOMBA UFUTE JINA LANGU KWENYE KITABU CHA HUKUMU, TAFADHALI LIANDDIKE KWENYE KITABU CHA UZIMA, NINAKUKIRII NA KUKUPOKEA MOYONI MWANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, HAKIKA WEWE NI MUNGU NA ULIFUFUKA KATIKA WAFU, Amen.

Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo, kwa maombi, sadaka kwa njia ya M-Pesa, kupiga simu au Wasats App, ni +25559859287. Tupo Arusha Tanzania.

0 Toa maoni yako.

The Ug Tv Yaja PUNDE, IS COMING SOON

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

MWALIMU OSCAR SAMBA SABABU ZA KUTOA SADAKA NA MAJIBU YAKO KUCHELEWA KIBI...

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

NAFASI YA SADAKA KATIKA KUKUWEZESHA KUTIMIZA MAONO AU NDOTO ZAKO

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

Mwalimu Oscar Samba MSIKILIZE MUNGU

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

Mwalimu Oscar Samba, Mbinu Teule za Kutoka Kwenye Umasikini Kwa Watu Wal...

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

Mwalimu Oscar Samba, Mbinu Teule za Kutoka Kwenye Umasikini Kwa Watu Wal...

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

Mwalimu Oscar Samba, Mbinu Teule za Kutoka Kwenye Umasikini Kwa Watu Wal...

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

Mwalimu Oscar Samba, Mbinu Teule za Kutoka Kwenye Umasikini Kwa Watu Wal...

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

Mwalimu Oscar Samba, Mbinu Teule za Kutoka Kwenye Umasikini Kwa Watu Wal...

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

Mwalimu Oscar Samba, Mbinu Teule za Kutoka Kwenye Umasikini Kwa Watu Wal...

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

Mwalimu Oscar Samba, Mbinu Teule za Kutoka Kwenye Umasikini Kwa Watu Wal...

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

Mwalimu Oscar Samba, Mbinu Teule za Kutoka Kwenye Umasikini Kwa Wtu Wali...

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

Msanii Hafsa Kazinja aokoka baada ya kukutana na mauzauza jukwaani

MWANAMUZIKI aliyeamua kumgeukia Mungu na kuokoka, Hafsa Kazinja aamebainisha kuwa alikuwa akiteswa na mauzauza ya kishirikina pindi alipokuwa katika majukwaa akiimba Bongo Fleva.

 Hafsa alisema alikumbana na mambo mengi sana ya ajabu ikiwemo kuona majoka makubwa jukwaani akiwa anatumbuiza na sauti za ajabu za mara kwa mara.

“Nilikuwa naishi maisha ya ajabu sana jamani yaani, nikiwa jukwaani naimba basi naanza kusikia sauti za ajabu mara naona majoka makubwa yanapita pita mbele yangu na kunifanya niishiwe pozi katika utumbuizaji wangu, hayo yote najua zilikuwa chuki za binadamu, nashukuru tangu niokoke hivi sasa sina matatizo hayo kabisa,” alisema Hafsa
0 Toa maoni yako.

KIGOMA WATAKA UZINDUZI WA ALBAMU TATU ZA MWAITEGE

WAKAZI wa Mkoa wa Kigoma, wameiomba Kampuni ya Msama Promotions kuwapelekea uzinduzi wa albamu tatu za mwimbaji mahiri wa nyimbo za injili nchini Boniface Mwaitege.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex Msama amepokea maombi mengi kwa wakazi wa mkoa huo wakihitaji uzinduzi huo ufanyike mkoani kwao.

“Nimepokea maombi ya wakazi wa Kigoma wakihitaji uzinduzi wa muimbaji nguli, Bonny Mwaitege ambaye anatarajia kuzindua albamu tatu,” alisema Msama.

Msama alisema mbali ya Kigoma mikoa mingine imeonesha nia ya kutaka uzinduzi huo ufanyike mikoani kwao.

Alisema wakazi wa Kigoma wanatamani kumuona akifanya onyesho mkoani humo kwa kuwa ni moja ya waimbaji ambao wamekuwa wakiwashuhudia wakifanya makubwa jukwaani.

Aidha Msama alisema kuwa kujitokeza kwa baadhi ya wananchi wa mikoa mbali hiyo kuomba, inampa moyo kuona watu wamemgeukia Mungu na kutaka kupata neno kutoka kwa waimbaji wa muziki wa injili ambako alisistiza kuwa yuko pamoja nao na atajitahidi.

Mwimbaji huyu machachari ambaye anatamba na nyimbo mbalimbali kama Mama ni mama, Mke mwema, Wakusamehe, fungua moyo wako na njoo uombewe na Yesu yupo anatarajia kuzindua albamu hizo tatu Agosti 2 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

Msama alisema kuwa Kamati ya Maandalizi itaketi na kujadili kwa sababu ni mikoa mingi iliyoomba kupelekewa uzinduzi huo hivyo ni jambo la kujipanga kuona namna itakavyoweza kufanya na kuwafikia katika mikoa yao.
0 Toa maoni yako.

UNATUMAINI NINI by G J SINGER

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

EWE BWANA na G J SING'ER

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

USALAMA WA KUTOSHA TAMASHA LA PASAKA

Mjumbe wa Kamati ya maandalizi ya tamasha la Pasaka, Khamis Pembe, akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuhusu tamasha hilo litakalofanyika Aprili 5. Kushoto ni Mwenyekiti wa tamasha hilo, Alex Msama. (Picha na Francis Dande)



Mwenyekiti wa Tamasha la Pasaka, Alex Msama akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuhusu tamasha hilo litakalofanyika Aprili 5. Kushoto ni Mwenyekiti wa tamasha hilo, Alex Msama.

NA LOVENESS BERNARD
KAMATI ya Tamasha la Pasaka, imewahakikishia usalama wapenzi wa muziki wa Injili na Watanzania kwa jumla katika tamasha hilo litakalokata utepe Aprili 5 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mjumbe wa Kamati hiyo, Khamis Pembe, alisema tayari wamewasiliana na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna (CP), Suleiman Kova.

Alisema maandalizi ya Tamasha la Pasaka yamekamilika asilimia 90 na mwaka huu litakuwa la aina yake.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Alex Msama, alisema mwaka huu tamasha linaadhimisha miaka 15 tangu lianzishwe na wanatarajia kumwalika Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi kujumuika nao, kwani ndiye alikuwa mgeni rasmi wakati linaanzishwa.

Msama aliwataja waimbaji wengine watakaokuwepo katika tamasha hilo kuwa ni pamoja na John Lisu na Kwaya ya Uinjilisti Kijitonyama huku wakiwa katika mazungumzo na mwimbaji nguli wa nyimbo za Injili, Rose Muhando, kutokana na maombi ya wapenzi wengi wa tamasha hilo.
0 Toa maoni yako.

JENNIFER MGENDI ATOA ALBAMU MPYA YA WEMA NI AKIBA

Mwimbaji wa siku nyingi wa nyimbo za injili nchini, Jennifer Mgendi, ameachia albamu yake mpya mapema wiki hii.

Akizungumza na blogu hii Mgendi amesema albamu hiyo ina jumla ya nyimbo saba ambazo ni Wema ni Akiba, Nani kama Mungu?, Nakungoja aliomshirikisha Mchungaji Abiudi Misholi, Kimbilia Msalabani, Nakuhitaji Roho, Tenda nishangae na Wastahili.

Akizungumzia video ya albamu hiyo, Mgendi amesema maandalizi ya video yameanza na video itazinduliwa Juni 28 katika kanisa la DCT Tabata Shule katika tamasha litakaloambatana na shukurani ya kutimiza miaka 20 tangu aanze uimbaji.

Mbali na uimbaji Jennifer pia ni muandaaji wa filamu mbalimbali za kidini hadi sasa akiwa na filamu tano Joto la roho, Pigo la faraja, Teke la Mama, Chaimoto na Mama Mkwe.
0 Toa maoni yako.
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company