Serikali yatakiwa kuoanisha sheria za vipodozi SADC


Friday Feb 22, 2013
| Text Size
[-]
[+]
Pekua IPPmedia
Mwenyekiti Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii, Magreth Sitta
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii imeitaka serikali kuoanisha sheria zake na zile za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (Sadc) kuhusiana na matumizi ya dawa na vipodozi ili kulinda afya za watumiaji.
 
Mwenyekiti wake, Magreth Sitta alitoa wito huo juzi baada ya kamati yake kutembelea mpaka wa Tanzania na Malawi katika eneo la Kasumulo wilayani Kyela na Mto Songwe unaotenganisha nchi hizo  kwa umbali wa zaidi ya kilometa 15.
 
Akiwa katika maeneo hayo, alishuhudia njia nyingi za panya zinazotumika kuingiza nchini bidhaa za vyakula kama vile sukari na vipodozi ambavyo baadhi yake havijasajiliwa nchini.
 
Alisema  kuna baadhi ya dawa na vipodozi ambavyo havikubaliki nchini lakini katika baadhi ya nchi za Sadc vinakubalika hali ambayo inasababisha udhibiti wake kuwa mugumu.
Alisema ili kuondokana na hali hiyo ni vema sheria za Tanzania zikaoanishwa na zile za nchi za Sadc ili bidhaa za aina moja ziruhusiwe kutumika kwenye nchi zote za Jumuiya hiyo.
 
 Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kyela ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Magreth Ester Malenga alisema kuwapo kwa bidhaa ambazo hazikubaliki nchini lakini zinatumika katika nchi jirani kunatoa changamoto kubwa kwenye ulinzi wa mipaka hasa katika kudhibiti zisiingizwe nchini kwa magendo.
 
Alisema kwa sasa sheria ya Tanzania hairuhusu kuingizwa kwa sukari kutoka Malawi, lakini wakati huo huo kuna uhaba mkubwa wa bidhaa hiyo wilayani humo, hali ambayo inatoa changamoto kubwa kwake binafsi kama Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya na kwa vyombo vya dola. 
 
Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid, alisema Serikali itaufanyia kazi ushauri uliotolewa na Kamati hiyo, hasa ule ambao uko chini ya wizara yake na kuihakikishia kuwa suala la ushirikiano baina ya Tanzania na nchi jirani litaimarishwa
CHANZO: NIPASH
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company