wakenya waombea uchaguzi.


Mamia ya Wakenya wamehudhuria mkusanyiko wa mwisho wa sala mjini Nairobi, kuomba uchaguzi mkuu wa juma lijalo uwe wa salama.
Bendera ya Kenya. Kenya yaamua uchaguzi
Mhadhara huo wa ibada umefanywa baada ya polisi kusema kuwa vipeperushi vinavochochea fujo vilisambazwa katika baadhi ya maeneo.
Wagombea kadha wa urais walihudhuria mhadhara wa leo, pamoja na Naibu Waziri Mkuu, Uhuru Kenyatta.
Anakabili mashtaka ya uhalifu dhidi ya binaadamu kuhusu ghasia zilizotokea baada ya uchaguzi wa Kenya miaka mitano iliyopita ambazo ziliuwa watu zaidi ya elfu moja.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company