HALI BADO NI TETE,Misri yaivunja Muslim Brotherhood kama NGO



Wizara ya mshikamano wa kijamii ya Misri imeamua kulivunja kundi la Muslim Brotherhood kama shirika lisilo la kiserikali.

Wizara inayoshughulikia kutoa leseni ya kuundwa kwa mashirika hayo baadaye itakutana na waandishi wa habari ili kuzungumzia zaidi suala hilo. Hapo jana kamati ya baraza la mawaziri iliamuru kuondolewa kundi la Brotherhood katika orodha ya serikali ya mashirika yasiyo ya kiserikali yaliyopewa vibali. Awali, mahakama ya Cairo iliamuru kupigwa marufuku kwa shughuli zote za kundi hilo, kuzuia fedha na kuunda jopo la kusimamia mali za kundi hilo.www.hakileo.blogspot.com
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company