CHADEMA Arusha yanyakua kiti cha Naibu Meya

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika Jiji la Arusha,kimeshinda uchaguzi mdogo wa kiti cha unaibu Meya wa Jiji hilo. Katika uchaguzi huo,mgombea wa Chadema, Diwani wa Daraja Mbili, Prosper Msofe, alichaguliwa kushika nafasi hiyo,baada ya kupata kura 25, kati ya kura 28, huku mbili za hapana, na moja iliharibika. Chama cha Mapinduzi (CCM) hawakusimamisha mgombea, huku chama cha TLP, chenye Diwani mmoja, Michael Kivuyo ambaye awali alitangaza kugombea lakini alipima upepo na kuamua kujitoa kabla uchaguzi kufanyika.
www.hakileo.blogspot.com
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company