Raia zaidi wakimbia makwao Sudan Kusini

Watu waliohama makwao nchini Sudan Kusini

Mashirika ya kutoa misaada yamesema kuwa maelfu ya watu wamelazimika kuhama makwao kufuatia mapigano nchini Sudan Kusini na wanahitaji misaada ya dharura.

Wengi wamekimbia kambi moja iliyoko ufuko wa mto nile, baada ya kuvuka mto huo kwa mashaua ili kuepuka mapigano yanayoendelea mjini Bor kati ya wafuasi wa rais Salva Kirr na aliyekuwa naibu wake Riek Machar.

Mwandishi wa BBC, mjini humo amesema kuwa wakimbizi hao wamepiga kambi chini ya miti wakiwa na mali yao waliyofanikiwa kubeba.

Afisa mkuu wa Shirika la madaktari wasiokuwa na mipaka Medicins san Frontiers, MSF limesema hakuna maji masafi ya kunywa. Amesema watu wanakunywa maji chafu ya mto nile.

Amesema watu wengi wanajisaidia hadharani kutokana na ukosefu wa vyoo na hivyo kuongeza tishio la kuzuka kwa ugonjwa wa kuraha na kutapika.
www.hakileo.blogspot.com
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company