
Akihutubia taifa Rais Zuma alisema Afrika Kusini inaanza kupona vidonda vya historia ya ukatili na mgawanyiko na taratibu inajenga umoja wa taifa.
Lakini alisema bado kuna kazi ya kukamilisha lengo la kuondosha umaskini, tofauti za pato na ukosefu wa ajira.
Sherehe hizo zinafanywa kabla ya uchaguzi mkuu ambapo chama tawala cha ANC kinakabili upinzani dhidi ya uongozi wa nchi tangu kumalizika kwa utawala wa ubaguzi wa rangi mwaka wa 1994.