AJALI ; GARI YAPIGA MWELEKA NA KUINGIA MTARONI JIJINI MBEYA LEO



Wasamalia wema wakijaribu kulinasua gari aina ya Toyota Corolla (namba zake za usajili hazikuweza fahamamika mara moja kutokana na kutokuwepo) lililoingia kwenye mtaro baada ya dereva wake kuzidiwa maarifa ya kiudereza na kujikuta akiingia mtaroni,katika eneo la Mafiat mkabala na kituo cha mafuta cha Oilcom jijini Mbeya asubuhi hii.Dereva wa Gari hilo pamoja na mtu mwingine mmoja wamejeruhiwa na kukimbizwa hospital kwa matibabu.Chanzo cha ajali hiyo inaelezwa ni mwendo kasi aliokuwa nao Dereva wa gari hilo.


Wasamalia wema hao wakiangalia namna ya kuweza kulichomoa gari hilo.

Hayaaaa..... Moja.... mbili.... tatuuu twendeeeeeeee......

Mara wakafanikiwa kulitoma kwenye mtaro huo.Picha na Fadhil Atick,Mbeya

CHANZO; LUKAZA BLOG
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company