Kim Jong Un ahamasisha jeshi lake kuwa tayari kuingia vitani

Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un akikagua jeshi lake wakati wa mafunzo ya kijeshi katika pwani ya mashariki ya peninsula ya Korea.
Reuters/路透社
Na RFI

Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un amewaagiza wanajeshi wake kuwa tayari kuingia vitani kutokana na hali ya wasiwasi kati ya jeshi la nchi hiyo na lile la Korea Kusini.


Tangazo hili limetolewa baada ya kutokea kwa urushaji wa makombora katika mipaka ya nchi hizo mbili zinazoendelea kutishana mara kwa mara.

Vyombo vya habari nchini Korea Kaskazini zinaripoti kuwa uamuzi wa Kim Jong Un umefikiwa baada ya kikao cha dharaura na wakuu wa jeshi nchini humo.

Kiongozi huyo wa Pyongyang amewaambia wanajeshi kuwa tayari kuanza kutekeleza Operesheni na kuweka silaha zao tayari kuishambulia Korea Kusini na watasalia katika hali hiyo hadi kesho Jumamosi saa kumi na moja jioni.

Viongozi wa Jeshi nchini Korea Kusini wamemjibu kiongozi huyo wa Korea Kaskazini kwa kumwambia kuwa wako tayari kujilinda ikiwa watashambuliwa.

Tangu kumalizika kwa vita vilivyoigawa Korea mwaka 1953, mataifa haya mawili yameendelea kutishana kwa kushambuliana kijeshi hali inayoendelea kuzua hali ya wasiwasi katika Peninsula ya Korea.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company