Yaliomo kwenye makubaliano ya S.kusini

Image copyrightAFPImage captionSudan kusini ni nchi changa duniani iliyojtangaza uhuru wake 2011

Hivi ndio vipengee vikuu kwenye makubaliano ya amani ambayo rais wa Sudan kusini Salva Kiir anatarajiwa kusiani Juba:
Mapigano yasite mara moja. Wanajeshi wasalie kweny kambi zao kwa siku 30, vikosi vya nje viondoke katika siku 45 na watoto wanaotumiwa jeshini na wafungwa wa vita waachiliwe huru.
Vikosi vyote vya usalama vitoke umbali wa kilomita 25 kutoka Juba, nabadala yake vikosi maalum na polisi ya pomoja vichukuwe nafasi hiyo.
Waasi wapewe cheo cha "makamu wa kwanza wa rais"
Serikali ya mpito ya muungano wa kitaifa iidhinishwe katika muda wa siku 90 na iongoze nchi kwa miezi 30.
Uchaguzi ufanyike siku 60 kablaya ya kumalizika kipindi cha mpito.
Serikali ipate uwingiwa nyadhifa serikalini katika kiwango cha kitaifa na katika majimbo 7 kati ya 10 yaliopo.
Katika majimbo yanayokumbwa na vita - Jonglei, Unity, na Upper Nile - waasi wanapata uwakilishi ulio sawana serikali.
Tume ya ukweli na mapatano ichunguze ukiukaji wa haki za binaadamu.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company