Ris Uhuru Kenyatta wa Kenya jana aliahidi kuwa serikali yake itashirikiana na jumuiya ya kimataifa katika mapambano dhidi ya ugaidi ili kulinda utulivu wa Kenya, na Kenya haitatishwa na magaidi. Akiongea na balozi wa Marekani nchini Kenya Bw Robert Godec, Rais Kenyatta amesema Kenya itafanya kazi kwa karibu na jumuiya ya kimataifa katika mambo yote ya usalama yenye manufaa kwa Kenya, Afrika Mashariki na dunia.
Balozi Godec amesema serikali ya Marekani iko tayari kutoa msaada wowote ambao Kenya inahitaji katika mapambano dhidi ya ugaidi. Kwa sasa wataalamu wa Marekani wako katika jengo la Westgate lilishambuliwa na magaidi wa kundi la Al Shabaab, wakiendelea kuwasaidia maofisa wa Kenya kutafuta miili ya watu na ushahidi.
TAIFA STARS HAZARANI
-
Kaimu kocha wa timu ya taifa ya Tanzania Etiene Ndairagije ametangaza
kikosi cha timu ya taifa chenye wachezaji 30 ambao wanajiaandaa na mchezo
wa kuwania ...
6 years ago
