Meneja wa Metro Fm Alex Ngusa (kulia) ameongoza kikao cha watumishi wa kittuo hicho kutoa taarifa na utaratibu wa jinsi ya kujipanga na kwaajili ya kushiriki taratibu zote hata kumpumzisha katika nyumba ya milele mtumishi mwenzao.
Marehemu Dj Alex anatarajiwa kuzikwa leo (jumatano) nyumbani kwao wilayani Bunda mkoani Mara.
Kutoka kulia ni Dj Victor, Tommy Alphonce na Jackob Usungu ambaye alikuwa akishirikiana na marehemu kufanya kipindi kimoja cha muziki wa Afrika kilichokuwa kikiruka majira ya jioni kikitikisa hasa.
Simanzi kubwa imewakumba watangazaji, wanahabari na wasikilizaji wa kituo cha radio Metro Fm ya jijini Mwanza mara baada ya kuondokewa na mmoja kati ya mfanyakazi mwenzao aliyetambulika kwa jina la DJ Alex.
Dj Alex alifariki dunia juzi akiwa ni mmoja kati ya abiria wa basi la kampuni ya Luhuye lililokuwa likitokea Sirari Mkoani Mara Kwenda Kahama kupata ajali katika eneo la Masanza Kona Wilaya ya Busega Mkoani Simiyu.
#USOPEN_VIGOGO CHALI
-
SIKU Safi kwa Muaustralia Nick Kyrgios baada ya ushindi dhidi Johnson na
kutinga raundi ya Pili.
- Rafael Nadal akimchapa Millman Seti Tatu zote mfululi...
4 years ago