MIROSLAV KLOSE ASTAAFU UJERUMANI BAADA YA REKODI YA KUTISHA YA MABAO HADI KOMBE LA DUNIA

MFUNGAJI bora wa kihistoria wa Ujerumani, Miroslav Klose, ametangaza kustaafu soka ya kimataifa.
Kiasi kama cha mwezi mmoja tangu ashjinde Kombe la Dunia na nchi yake nchini Brazil, mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 36 ameamua kupumzika timu ya taifa.
Amefikisha jumla ya mabao 16 aliyofunga katika Kombe la Dunia na jumla ameifungia mabao 71 timu yake ya taifa. Huyo ndiye pia mfungaji wa mabao mengi zaidi katika Fainali za Kombe la Dunia, akifuatiwa na Mbrazil Ronaldo Lima mwenye mabao 15.
Mchezo umekwisha: Miroslav Klose ametangaza kustaafu soka ya kimataifa baada ya kuifungia Ujerumani mabao 71
REKODI YA MABAO YA KLOSE KOMBE LA DUNIA
1, 2, 3: Ujerumani 8-0 Saudi Arabia, makundi, 2002
4: Ujerumani 1-1 Jamhuri ya Ireland, makundi, 2002
5: Cameroon 0-2 Ujerumani, makundi, 2002
6, 7: Ujerumani 4-2 Costa Rica, makundi, 2006
8, 9: Ecuador 0-3 Ujerumani, makundi, 2006
10: Ujerumani 1-1 Argentina (baada ya dakika 120, penalti 4-2), Robo Fainali, 2002
11: Ujerumani 4-0 Australia, makundi, 2010
12: Ujerumani 4-1 England, 16 Bora, 2010
13, 14: Argentina 0-4 Ujerumani, Robo Fainali, 2010
15: Ujerumani 2-2 Ghana, makundi, 2014
16: Brazil 1-7 Ujerumani, Nusu Fainali, 2014


Klose alifunga mabao mawili Ujerumani ikitwaa Kombe la Dunia nchini Brazil mwaka huu
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company