Rais Kikwete aongoza mazishi ya mbunge

RAIS Jakaya Kikwete ameongoza mamia ya wakazi wa Chalinze, Pwani kwenye mazishi ya mbunge wao, Said Bwanamdogo, aliyezikwa kwenye Kata ya Mioni, Bagamoyo.
Bwanamdogo alifariki dunia Januari 22 mwaka huu katika hospitali ya Taifa Muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu.

Viongozi wengine waliohudhuria mazishi hayo ni Makamu wa Rais, Dk. Gharib Bilal, mke wa rais, Mama Salma Kikwete, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa, Freeman Mbowe na wabunge wengine wengi.

Akizungumza katika mazishi hayo, Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, alisema amesikitishwa na msiba huo, kwani bado walikuwa wakihitaji mchango wa mbunge huyo ndani ya CCM na Bunge.

Mbunge wa Kisarawe, Seleman Jafo (CCM), alieleza kusikitishwa na kifo hicho ambacho kimeacha pengo kwa wabunge wa Mkoa wa Pwani.

Nao baadhi ya wakazi wa Chalinze walielezea masikitiko yao juu ya kifo cha mbunge wao
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company