Mgogoro wa Sudan Kusini umekuwa ukiendelea tangu tarehe 15 Disemba
Sudan na Sudan Kusini zimejadili swala la kushirikiana katika kushika doria ili kulinda visima vya mafuta Sudan Kusini ambako waasi wanatishia usalama.
Taarifa hii ni kwa mujibu wa waziri wa mambo ya nje wa Sudan Kusini.
Marais wa nchi hizo mbili wameanza mazungumzo ya kupeleka kikosi cha ulinzi ili kulinda visima vya mafuta Kusini ambako waasi wamezusha vurugu kwa karibu wiki nne sasa.
Taarifa hii inakuja baada ya Rais wa Sudan Omar Bashir kwenda mjini Juba kwa mashauriano na Rais Salva Kiir kuhusu mzozo wa kisiasa unaotokota nchini humo.
Mgogoro huo kati ya wafuasi wa Rais Kiir na hasimu wake Riek Machar aliyekuwa makamu wa rais wa bwana Kiir ingawa alifutwa kazi pamoja na mawaziri wengine wa serikali.
Takriban watu 1,000 wameuawa kwenye mgogoro huo uliozuka tarehe 15 mwezi Disemba.
www.hakileo.blogspot.com
TAIFA STARS HAZARANI
-
Kaimu kocha wa timu ya taifa ya Tanzania Etiene Ndairagije ametangaza
kikosi cha timu ya taifa chenye wachezaji 30 ambao wanajiaandaa na mchezo
wa kuwania ...
5 years ago