Waandishi 2 wauawa wakiwa hewani Marekani

Image captionWaandishi waliopigwa risasi

Waandishi wawili wa habari wamepigwa risasi katika jimbo la Marekani la Virginia wakati wakifanya mahojiano ya moja kwa moja ya runinga.

Kanda ya video inaonyesha mwandishi wa habari wa kike akimtania mgeni aliyekua akimuhoji kabla ya risasi kufyatuliwa mara nane.

Mwandishi huyo anaonekana akiruka na kamera kuanguka sakafuni huku mwanamume aliyevalia nguo nyeusi na kubeba bunduki akipita karibu.

Kituo kilichoajiri waandishi hao cha WDBJ kinasema mwandishi huyo wa habari Alison Parker na mpiga picha Adam Ward walikufa katika tukio hilo .

Polisi wanasema mshukiwa hajulikani aliko.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company