KUMEKUCHA, Mashambulizi mengine Mombasa;10 wajeruhiwa

Nchini Kenya watu 10 wamejeruhiwa wakati washambuliaji waliporusha guruneti ndani ya mkahawa mmoja katika mji wa pwani wa Mombasa na kuzusha hofu ya usalama katika eneo hilo tete.


Mashambulizi yamekuwa yakiongezeka mjini Mombasa.
Mkuu wa polisi mjini Diani, Jack Ekakuro, amesema washambuliaji hao waliilenga baa moja iitwayo
Tandoor mjini Diani mapema leo, wakati ilipokuwa bado imefurika watu waliokuwa wakiendelea kusherehekea mwaka mpya. Hii ni sehemu ya mlolongo wa mashambulizi, ikiwa ni pamoja na lile la bomu kwenye basi moja katika mtaa wa Eastleigh mjini Nairobi mwezi uliopita, hali inayowatia wasiwasi Wakenya wengi.
Mwandishi: Diana Kago
Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company