Nchini Kenya watu 10 wamejeruhiwa wakati washambuliaji waliporusha guruneti ndani ya mkahawa mmoja katika mji wa pwani wa Mombasa na kuzusha hofu ya usalama katika eneo hilo tete.
Mashambulizi yamekuwa yakiongezeka mjini Mombasa.
Mkuu wa polisi mjini Diani, Jack Ekakuro, amesema washambuliaji hao waliilenga baa moja iitwayo
Tandoor mjini Diani mapema leo, wakati ilipokuwa bado imefurika watu waliokuwa wakiendelea kusherehekea mwaka mpya. Hii ni sehemu ya mlolongo wa mashambulizi, ikiwa ni pamoja na lile la bomu kwenye basi moja katika mtaa wa Eastleigh mjini Nairobi mwezi uliopita, hali inayowatia wasiwasi Wakenya wengi.
Mwandishi: Diana Kago
Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman
TAIFA STARS HAZARANI
-
Kaimu kocha wa timu ya taifa ya Tanzania Etiene Ndairagije ametangaza
kikosi cha timu ya taifa chenye wachezaji 30 ambao wanajiaandaa na mchezo
wa kuwania ...
5 years ago