Maadhimisho miaka mitatu tangu apinduliwe Mubarak, yapita kwa kishindo Misri wengi wa uwawa


Waandamanaji kadha wameuwawa katika mapambano yaliyotokea mjini Cairo na miji mengine ya Misri, wakati maandamano ya pande zinazopingana yamefanywa kuadhimisha mwaka wa tatu wa maandamano yaliyompindua Hosni Mubarak.

Mjini Cairo polisi walitumia moshi wa kutoza machozi na kufyatua risasi hewani kuwatawanya wanaharakati walioandamana na waandamanaji Waislamu wanaomuunga mkono rais wa zamani Mohamed Morsi ambaye alitolewa madarakani na jeshi.

Inaarifiwa kuwa bomu lilotegwa kwenye gari liliripuka karibu na kambi ya polisi katika mji wa Suez.

Wafuasi wa serikali piya walikusanyika katika medani ya Tahrir kuadhimisha siku hiyo, wakipiga kelele huku wamebeba picha za mkuu wa jeshi, Jenerali Abdul Fattah al-Sisi.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company