CHANZO REDIO TEHARAN KISWAHILI
Serikali ya Sudan kwa mara nyingine tena imeituhumu Uganda kuwa inawaunga mkono waasi wa nchini humo.
Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Sudan imesisitiza kuwa, Uganda inapasa kuacha mara moja uungaji mkono wake kwa makundi ya waasi yanayopigana na serikali ya Khartoum. Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Sudan imeongeza kuwa, serikali ya Uganda inawapatia hifadhi viongozi wa makundi ya waasi sanjari na kuandaa vikao vya viongozi hao mjini Kampala kwa shabaha ya kupanga mikakati ya kuisambaratisha serikali ya Rais Omar Hassan al Bashir. Taarifa hiyo imeongeza kuwa, serikali ya Sudan iliwahi kuwasilisha mashtaka yake dhidi ya Uganda mwaka 2013 kwenye kikao cha 12 cha Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) mjini Cairo Misri, na pia kwenye kikao cha kimataifa cha Ukanda wa Maziwa Makubwa ya Afrika (ICGLR) kilichofanyika mwaka 2011. Kwa mujibu wa makubaliano yaliyofikiwa kwenye kikao cha ICGLR ni kwamba, ni marufuku kwa mwanachama wa ukanda huo kuyaunga mkono makundi ya waasi yanayopigana na nchi nyingine mwanachama. Makundi ya waasi nchini Sudan yamejizatiti zaidi katika majimbo ya Blue Nile lililoko kusini mwa Sudan na Kordofan Kusini lililoko katika eneo la Darfur, magharibi mwa nchi hiyo.
TAIFA STARS HAZARANI
-
Kaimu kocha wa timu ya taifa ya Tanzania Etiene Ndairagije ametangaza
kikosi cha timu ya taifa chenye wachezaji 30 ambao wanajiaandaa na mchezo
wa kuwania ...
5 years ago