Image copyrightImage captionRais Pierre Nkurunziza wa Burundi
Katika hotuba kwa taifa rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza ameonyesha hisia zake kuhusu kujumuisha vikosi vya usalama nchini humo.
Hayo yamekuja wiki moja baada ya kuapishwa kushika hatamu za uongozi wa nchi hiyo ambapo wakasoaji wanasema ni kinyume cha katiba.
Suala hilo limezusha ghasia kali na jaribio lililotibuka la kuipindua serikali.
Amezitaka kamati za usalama kufanya kazi usiku na mchana kupambana kile alichokiita kundi la watu wachache wanaofanya mauaji na kusababisha hofu kwa raia.
Amesema vijana hasa wa vyuo vikuu sasa watapata mafunzo ya uzalendo.
TAIFA STARS HAZARANI
-
Kaimu kocha wa timu ya taifa ya Tanzania Etiene Ndairagije ametangaza
kikosi cha timu ya taifa chenye wachezaji 30 ambao wanajiaandaa na mchezo
wa kuwania ...
5 years ago