Na Oscar Samba

Wachezaji wa Young Africans wakisalimiana na wachezaji wa Black Leopard kabla ya kuanza kwa mchezo
Mabingwa wa kombe la Vilabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati almaarufu kombe la Kagame, timu ya Young Africans Sports Club imeifunga timu ya Black Leopard ya Afrika Kusini mabao 3-2 katika mchezo wa kirafiki uliofanyika leo jioni katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaaam.
Young Africans iliyokuwa nje ya nchi kwa kambi ya mafunzo takribani wiki ilikuwa ikicheza mbele ya washabiki wake, iliweza kucheza soka safi na la kuvutia kipindi chote cha mchezo huku Black Leopard ikipata wakati mgumu kwa dakika 45 za kipindi cha kwanza.
Didider Kavumbagu alikosa bao la wazi dakika ya 21 ya mchezo akiwa yeye na mlinda mlango wa Black Leopard Ayanda Mtshali, lakini shuti alilopiga lilipaa juu ya lango la timu hiyo.
Yanga iliednelea kuutawala mchezo kwa wachezaji wake kupigiana migongeo mizuri na kuutawala mchezo hasa eneo la kiungo, Kabange Twite alishindwa pi akuipatia Yanga bao katika dakika ya 25 baada ya kushinda kumalizia pasi safi ya Mbuyu Twite.
Dakika ya 32 Jerson Tegete aliipatia Young Africans bao la kwanza kwa mkwaju wa penati kufuatia mlinzi wa Balck Leopard Harry Nyirenda kumuangusha Haruna Niyonzima katika eneo la hatari, amabpo mwamuzi Hashim aliamuru upigwe mkwaju wa penati na Jerson Tegete kuukwamisha mpira huo wavuni.
Yanga iliongeza kasi ya kusaka bao la pili lakini shambulizi liliofanywa na Mbuyu Twite liliokolewa na mlinda mlango wa Black Leopard Matshal kabla ya Mbuyu tena kupiga kichwa kilichopaa mita chahce juu ya lango la timu ya Black Leopard.
Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika Young Africans 1 – 0 Black Leopard.
Kipindi cha pili kilianza kwa Young Africans kufanya mabadiliko ambapo kocha Brandts aliwatoa Kabange Twite, Mbuyu Twite na golikipa Ally Mustafa ‘Barthez’ nafasi zao zikachukuliwa na Juma Abdul, Saimon Msuva na golikipa Said Mohamed.
Dakika ya 47, Humphrey Khoza aliipatia Black Leopard bao la kusawazisha kwa kichwa akiunganisha mpira wa kona uliopigwa na Edagr Manaka kufutia kutokuwepo kwa mawasilaino kati ya mlinzi Nadir Haroub na mkinda mlango wake Said Mohamed.
Kiungo chipukizi Frank Domayo aliipatia Young Africans bao la pili dakika ya 63 ya mchezo, akimaliza pasi safi iliyopigwa na kiungo Haruna Niyonzima na mpira huo kumkuta Domayo ambaye alimchambua mlinda mlango wa Black Leopard Mtishal na kuhesabu bao la pili.
Dakika 10 baadaye mshambuliaji Jerson Tegete aliipatia Young Africans bao la tatu kwa umakini akimalizia pasi ya kungo mshambuliaji Saimon Msuva aliyewatoka walinzi wa timu ya Black Leopard na kumpasia mfungaji aliyeukwamisha mpira huo wavuni.
Jerson Tegete nusra angeipatia Young Africans bao la nne, kufuatia lakini krosi iliyopigwa na Saimon Msuva kuokolewa na mlinzi wa Black Leopard sentimeta chache pemebeni mwa lango huku Tegete tayari akiwa tayari kwa kuukwamisha mpira huo.
Dakika ya 89, Black Leopard ilijipatia bao la pili kwa mkwaju wa penati kupitia kwa mshambuliaji wake Rodney Magalela kufuatia mlinzi wa kulia wa Young Africans kumcheza madhambi mshambuliaji huyo katika eneo la hatari.
Mpaka mpira unamalizika Young Africans 3- 2 Black Leopard.
Kocha mkuu wa Yanga Ernest Brndts amesema anashukuru timu yake kwa kupata ushindi huo wa leo, kwani timu ya Black Leopard ni timu nzuri, imecheza vizuri lakini mwisho wa siku vijana wangu walikuwa ni bora zaidi ndio maana wameibuk ana ushindi huo.
Kambi yetu ya mafunzo nchini Uturuki imetusaidia sana, wachezaji wanacheza kwa kujiamini wametulia hawana presha ya mchezo, hali inayopelekea kucheza migongeano kwa uhakika na hii ni dalili tosha kuwa tupo tayari kwa mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Vodacom alisema ‘Brandts’
Young Africans: 1.Ally Mustapha ‘Barthez’/Said Mohamed, 2.Mbuyu Twite/Juma Abdul, 3.Oscar Joshua, 4.Nadir Haroub’Cannavaro’, 5.Kelvin Yondani, 6.Athuman Idd ‘Chuji’, 7.Kabange Twite/Saimon Msuva, 8.Frank Domayo, 9.Didier Kavumbagu/Said Bahanuzi, 10.Jerson Tegete/George, 11.Haruna Niyonzima
Black Leopard: 1.Ayanda Mtshali, 2.Ernort Dzaga, 3.Nkosiyabo Xakane, 4.Harry Nyirenda, 5.Humphrey Khosa, 6.Munganga Djunga Jean, 7.Mongezi Bobe, 8.Thomas Madimba, 9.Abbas Amidm, 10.Edagr Manaka 11.Rodney Ramagalelasted: 19th January 2013 by MillardAyo in News

Kikosi cha Young Africans Sports Club
Timu ya Young Africans ambayo ilikuwa imeweka kambi ya mafunzo takribani wiki mbili mjini Antlaya nchini Uturuki kesho siku ya jumamosi itashuka dimba la Uwanja wa Taifa kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya Black Leopard kutoka nchini Afrika Kusini.
Black Leopard timu inayoshiriki ligi kuu ya Afrika Kusini maarufu kama PSL inatazamiwa kuwasili mchana huu kwa shirika la ndege la South African Airways ikiwa na msafara wa watu 42, ambapo timu pamoja na viongozi wake watafikia katika hotel ya White Sands Mbezi Beach.
Huu utakuwa mchezo wa kwanza kwa Yanga tangu kurejea nchini, hivyo ni nafasi kwa wadau, wapenzi wa soka kufika katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kuweza kujioniea mchezo huo majira ya saa 10 jioni siku ya jumamosi.
Kocha Mkuu wa Young Africans Ernest Brandts amesema kwao ni furaha kwa kupata nafasi ya kucheza na timu kutoka katika ligi kuu ya PSL nchini Afrika Kusini hivyo atatumia nafasi hvyo kukamilisha maandalizi ya mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Vodacom.
Leo asubuhi Young Africans imeendelea na mazoezi katika uwanja wa Mabatiini Kijitonyama tayari kabisa kujianda na mchezo huo.
Wachezaji wote wameendela na mazoezi leo isipokuwa Hamis Kiiza ‘Diego’ na mlinda mlango Yusuph Abdul ambao wanaoumwa malaria.
Aidha katibu mkuu wa Yanga Lawrence Mwalusako amemtambulisha Dr Nassoro Matuzya kwa wachezaji leo asubuhi kama dakatari wa timu ambapo ameanza kazi kushika nafasi ya daktari aliyekuwepo Dr Suphian Juma.
.
Wanamichezo 50 kati ya 52 waliochukua fomu kuomba kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) utakaofanyika Februari 24 mwaka huu wamerejesha fomu hizo.
Waombaji ambao hawakurejesha fomu ni Geofrey Nyange aliyekuwa akiomba ujumbe wa Kamati ya Utendaji kuwakilisha mikoa ya Morogoro na Pwani, na Shufaa Jumanne aliyekuwa akiomba kuwakilisha Kanda ya Dar es Salaam.
Orodha kamili ya waombaji ambao wamerejesha fomu ni Athuman Nyamlani, Jamal Malinzi, Omari Nkwarulo na Richard Rukambura (Rais). Michael Wambura, Ramadhan Nassib na Wallace Karia (Makamu wa Rais).
Kwa upande wa ujumbe wa Kamati ya Utendaji ni Abdallah Musa, Salum Chama na Kaliro Samson (Kagera na Geita), Jumbe Magati, Mugisha Galibona, Richard Rukambura, Samuel Nyalla, Titus Osoro na Vedastus Lufano (Mara na Mwanza).
Epaphra Swai na Mbasha Matutu (Shinyanga na Simiyu), Charles Mugondo, Elly Mbise na Omari Walii (Arusha na Manyara), Ahmed Mgoyi na Yusuph Kitumbo (Kigoma na Tabora), Ayubu Nyaulingo, Blassy Kiondo, Nazarius Kilungeja na Selemani Kameya (Katavi na Rukwa) na James Mhagama na Stanley Lugenge (Njombe na Ruvuma).
Athuman Kambi, Francis Ndulane na Zafarani Damoder (Lindi na Mtwara), Hussein Mwamba na Stewart Masima (Dodoma na Singida), Farid Nahdi, Hassan Othman Hassanoo, Riziki Majala na Twahili Njoki (Morogoro na Pwani), David Lugenge, Elias Mwanjala, Eliud Mvella na John Kiteve (Iringa na Mbeya), Davis Mosha, Khalid Mohamed na Kusiaga Kiata (Kilimanjaro na Tanga) na Alex Kamuzelya, Juma Pinto, Muhsin Balhabou, Omari Abdulkadir na Shaffih Dauda (Dar es Salaam).
n

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.