IJUWE KATIBA YA ZANZIBAR NA MABADILIKO YA 10 YA 2010 YALIYOIFANYA KUWA NCHI NA KUKINZANA NA KATIBA YA MUUNGANO.

____K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
KATIBA YA ZANZIBAR
SURA YA KWANZA
Zanzibar na Watu
Sehemu ya Kwanza
Zanzibar
1. Zanzibar na mipaka yake.
2. Zanzibar na Muungano.
2A. Mikoa na Wilaya za Zanzibar.
3. Muhuri wa Serikali na alama nyenginezo.
4. Katiba ya Zanzibar.
5. Zanzibar kufuata mfumo wa Vyama Vingi.
5A. Mgawanyo wa madaraka.
Sehemu ya Pili
Watu
6. Mzanzibari.
7. Haki ya kupiga kura.
SURA YA PILl
Malengo na Maamuru muhimu ya Sera ya Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar
8. Wajibu mkubwa wa Serikali.
9. Serikali na Watu.
10. Malengo ya kisiasa.
10A. Mabadiliko ya masharti ya Sura ya Pili
i
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
SURA YA TATU
Kinga ya Haki za Lazima, Wajibu na Uhuru wa Mtu Binafsi:
11. Usawa wa Binaadamu.
12. Usawa mbele ya Sheria.
13. Haki ya kuwa hai.
14. Haki na Uhuru wa mtu binafsi.
15. Haki ya faragha ya mtu na usalama wake.
16. Kinga ya uhuru wa kwenda.
17. Kinga ya kutokana na kudhulumiwa mali.
18. Uhuru wa maoni.
19. Uhuru wa mtu kuamini dini atakayo.
20. Kinga kwa uhuru wa kujikusanya na kujiunga.
21. Uhuru wa kushiriki shughuli za umma, haki ya kufanya kazi na kupata
ujira.
22. Wajibu wa kushiriki kazini.
23. Wajibu wa kutii sheria za nchi, kulinda mali ya umma na ulinzi wa Taifa.
24. Mipaka kwa haki na uhuru, na hifadhi kwa haki, na wajibu wake.
25. Haki za lazima na uhuru wa binafsi.
25A. Kufungua mashauri.
SURA YA NNE
Serikali
Sehemu ya Kwanza
Rais
26. Afisi ya Rais na sifa za kuchaguliwa kuwa Rais.
27. Uchaguzi wa Rais.
28. Muda wa kuendelea na Urais.
29. Kuongezwa kwa kipindi cha miaka mitano.
30. Kutofaa kuwa Rais.
31. Kiapo cha Rais.
ii
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
32. Kuachishwa Urais kwa ugonjwa.
33. Nafasi katika kiti cha Urais.
34. Mpango wa uchaguzi iwapo kiti cha Rais kiwazi.
35. Mshahara na malipo mengine ya Rais.
36. Rais hatashtakiwa akiwa kazini.
37. Baraza la Wawakilishi laweza kumshtaki Rais.
38. Hadhi ya Rais aliyepita.
Sehemu ya Pili
Makamo wa Kwanza wa Rais na Makamo wa Pili wa Rais
39. Makamo wawili wa Rais.
39A. Kuachwa wazi kwa nafasi ya Makamo wa Kwanza wa Rais.
40. Kuwa wazi kwa nafasi ya Makamo wa Kwanza wa Rais na
Makamo wa Pili wa Rais.
41. Hoja ya kura ya kutokuwa na imani.
Sehemu ya Tatu
Mawaziri, Manaibu Mawaziri na Baraza la Mapinduzi
42. Wizara za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
42A. Kuacha kufanyakazi kwa Makamo wa Kwanza wa Rais na Mawaziri.
43. Baraza la Mapinduzi.
44. Ugawaji wa Wizara kwa Mawaziri.
45. Mikutano ya Baraza.
46. Viapo vya uaminifu.
47. Naibu Mawaziri.
48. Nafasi ya Waziri, Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi kuwa wazi.
49. Katibu wa Baraza la Mapinduzi.
50. Katibu Mkuu.
iii
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
Sehemu ya Nne
Madaraka ya Serikali
51. Malengo ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
52. Kutolazimika kwa Rais kufuata ushauri wa mtu.
53. Uanzishaji wa Afisi na Wadhamini wa Afisi hizo.
54. Muda wa kufanya kazi katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
55. Mwanasheria Mkuu.
56. Kazi za Mwanasheria Mkuu.
56A. Mkurugenzi wa Mashtaka
57. Kiapo cha uaminifu.
58. Washauri Maalum.
59. Uwezo wa kutoa msamaha.
60. Kamati ya Ushauri katika uwezo wa kutoa msamaha.
61. Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya.
62. Kazi za Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya.
SURA YA TANO
Baraza la Wawakilishi
Sehemu ya Kwanza
Muundo wa Baraza la Kutunga Sheria
63. Baraza la Kutunga Sheria.
64. Kuanzishwa kwa Baraza la Wawakilishi.
65. Uchaguzi waWajumbe wa kuchaguliwa.
66. Wajumbe wa kuteuliwa.
67. Wajumbe Wanawake katika Baraza.
68. Sifa za kuchaguliwa.
69. Kutofaa kuchaguliwa.
70. Kiapo cha Mjumbe Mwakilishi.
71. Muda wa Wajumbe kushika madaraka yao.
72. Uamuzi wa suala kama mtu ni Mjumbe Mwakilishi ama sio.
iv
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
73. Spika.
74. Naibu Spika.
75. Taratibu za uchaguzi wa Spika na Naibu Spika.
76. Katibu wa Baraza la Wawakilishi.
77. Afisi ya Baraza la Wawakilishi.
Sehemu ya Pili
Sheria na Taratibu katika Baraza la Wawakilishi
78. Nguvu za kutunga Sheria.
79. Utaratibu wa kutunga Sheria.
80. Kubadilisha Katiba.
80A. Kura ya Maoni kwa mabadiliko ya baadhi ya vifungu vya Katiba.
81. Uongozi wa kikao cha Baraza la Wawakilishi.
82. Viti vilivyo wazi katika Baraza la Wawakilishi na utaratibu wa kuendesha
shughuli za Baraza.
83. Upigaji kura katika Baraza la Wawakilishi.
84. Madaraka ya Rais katika Baraza la Wawakilishi.
85. Kamati za Baraza la Wawakilishi.
86. Baraza la Kutunga Sheria.
87. Lugha rasmi.
88. Kazi za Baraza la Wawakilishi.
Sehemu ya Tatu
Kuitisha na Kuvunja Baraza la Wawakilishi
89. Kuitisha Mkutano wa Baraza la Wawakilishi.
90. Uchaguzi Mkuu na Mkutano wa mwanzo.
91. Kuitisha na kuvunja Baraza la Wawakilishi.
92. Maisha ya Baraza la Wawakilishi.
v
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
SURA YA SITA
Sheria
Sehemu ya Kwanza
Mahkama Kuu
93. Kuundwa kwa Mahkama Kuu.
94. Uteuzi wa Majaji wa Mahkama Kuu.
95. Muda wa kushika madaraka ya Ujaji.
96. Viapo kwa Majaji wa Mahkama Kuu.
97. Uanachama katika vyama vya siasa.
Sehemu ya Pili
Mahkama ya Rufaa
98. [Kimefutwa].
99. Kazi na uwezo wa Mahkama ya Rufaa.
99A. Ufafanuzi wa Katiba kupelekwa Mahkama Kuu.
Sehemu ya Tatu
Mahkama Nyenginezo
100. Kuanzishwa kwa Mahkama nyengine.
Sehemu ya Nne
Utaratibu wa kupeleka Hati na kutekeleza maagizo yaliyomo katika
Hati zilizotolewa na Mahkama
101. Utekelezaji wa maagizo ya Mahkama utafanywa nchini Tanzania kote.
vi
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
Sehemu ya Tano
Tume ya Utumishi ya Mahkama
102. Tume ya Utumishi ya Mahkama.
102A. [Kimefutwa].
103. [Kimefutwa].
SURA YA SABA
Sehemu ya Kwanza
Fedha
Masharti ya Fedha Yahusuyo Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar
104. Mfuko Mkuu wa Hazina na Fedha nyengine za Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar.
105. Makadirio.
106. Ruhusa ya matumizi ya Mfuko Mkuu wa Hazina kwa Sheria ya Matumizi
ya Fedha.
107. Malipo kwa idhini ya Hati Maalum.
108. Mfumo wa matumizi ya dharura.
109. Matumizi ya fedha kabla ya sheria kuanza kutumika.
110. Deni la Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
111. Malipo ya baadhi ya maafisa.
112. Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.
113. Kumuondoa kazini Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu.
Sehemu ya Pili
Masharti ya Fedha Yahusuyo Mambo ya Muungano
114. Mchango wa Muungano.
115. Uwezo wa kutumia kasma.
vii
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
SURA YA NANE
Kamisheni ya Utumishi wa Umma
116. Kamisheni ya Utumishi wa Umma.
117. Tume ya Utumishi ya Serikali.
118. Uwezo wa Tume za Utumishi.
SURA YA TISA
Tume ya Uchaguzi
119. Tume ya Uchaguzi.
120. Majimbo.
SURA YA KUMI
Idara Maalum
121. Idara Maalum.
122. Tume ya Utumishi ya Idara Maalum.
123. Uwezo wa Rais katika Idara Maalum.
SURA YA KUMI NA MOJA
Mamlaka ya Baadhi ya Vyombo vya Muungano
124. Mamlaka ya Baadhi ya Vyombo vya Muungano kutumika Zanzibar.
viii
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
SURA YA KUMI NA MBILI
Vyombo Vyengine vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
Sehemu ya Kwanza
Tume ya Mipango
125. Tume ya Mipango.
126. Wajumbe wa Tume.
127. Katibu wa Tume ya Mipango.
Sehemu ya Pili
Serikali za Mitaa
128. Serikali za Mitaa.
SURA YA KUMI NA TATU
Mambo ya Jumla
129. Kujiuzulu.
130. Uteuzi mpya na kuarifiwa kwa kuachishwa kazi.
131. Maelezo kuhusu utaratibu wa kukabidhi madaraka ya kazi katika
Utumishi wa Serikali.
132. Sheria za Muungano.
133. Masharti ya kutoza kodi.
134. Ufafanuzi.
134A. Kufuta Katiba ya 1979.
135. Jina la Katiba na tarehe ya kuanza kutumika.
ix
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
KATIBA YA ZANZIBAR
UTANGULIZI
AZIMIO LA BARAZA LA WAWAKILISHI KUWEKA
KATIBA YA ZANZIBAR
KWA KUWA Mkutano wa Baraza la Wawakilishi wa tarehe 9 Oktoba,
1984 kwa niaba ya wananchi wa Zanzibar ulielewa na kukubali kwamba jukumu
letu katika historia ya Watu wa Zanzibar kuimarisha Umoja, kuendeleza Mapinduzi
ya Kijamaa katika Zanzibar na kusukuma Mapambano ya Ukombozi na harakati
za Mapinduzi nchini, katika Afrika na duniani kote;
NA KWA KUWA tunatambua kwamba Umoja wa Wananchi wa Zanzibar
unatokana na ushirikiano wa miaka mingi tangu wakati wa mapambano ya
kupigania Uhuru hadi kufikia daraja hii ya mafanikio, na unatokana na siasa yetu
ya Ujamaa na Kujitegemea;
NA KWA KUWA tunazingatia na kuthamini kazi nzuri ya Kimapinduzi
iliyofanywa naViongozi wa Mapinduzi, wakiongozwa na Mwasisi wa Chama
cha ASP na Mapinduzi ya Zanzibar ya 1964, Marehemu Mzee Abeid Amani
Karume, ambaye fikra zake zitaendelezwa na kudumishwa daima, kizazi baada
ya kizazi katika kupambana na Ukoloni, Ubepari, Unyonge, Uonevu na Dharau,
na badala yake kudumisha Uhuru na Umoja, Haki na Usawa, Heshima na Utu;
NA KWA KUWA tunatambua kwamba mafundisho na mawazo ya
Kimapinduzi yatalindwa, yataendelezwa na kudumishwa kwa misingi ya
Kidemokrasia;
NA KWA KUWA tunatambua kuwa mapambano ya kujenga Ujamaa
katika Zanzibar na kushiriki kwetu kikamilifu katika harakati za Mapinduzi ya
Zanzibar kunahitaji SHERIA madhubuti itakayowaongoza watu Ki-Katiba,
kutokana na fikra za Wafanyakazi na Wakulima;
x
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
NA KWA KUWA SISI, Wananchi wa Zanzibar tumeamua rasmi na kwa
dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na
amani;
NA KWA KUWA misingi hiyo yaweza tu kutekelezwa katika jamii yenye
demokrasia ambayo Serikali yake husimamiwa na Baraza la Wawakilishi lenye
Wajumbe waliochaguliwa na linalowakilisha wananchi, na pia yenye Mahkama
huru zinazotekeleza wajibu wa kutoa haki bila woga wala upendeleo wowote,
na hivyo kuhakikisha kwamba haki zote za binadamu zinadumishwa na kulindwa
na wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa ukamilifu;
KWA HIYO BASI, KATIBA HII IMETUNGWA NA BARAZA LA
WAWAKILISHI KATIKA KIKAO CHAKE CHA TAREHE 9 OKTOBA,
1984 kwa niaba ya Wananchi, kwa madhumuni ya kujenga jamii kama hiyo, na
pia kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Zanzibar inaongozwa na Serikali yenye
kufuata misingi ya demokrasia na ya kijamaa.
xi
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
SURA YA KWANZA
ZANZIBAR
Sehemu ya Kwanza
Zanzibar
1. Zanzibar ni Nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la
Visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na Visiwa vidogo vilivyoizunguka
na bahari yake ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na
Zanzibar ikiitwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.
2. Zanzibar ni miongoni mwa Nchi mbili zinazounda Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania.
2A. Kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za Serikali, Rais
aweza kuigawa Zanzibar katika Mikoa, Wilaya na maeneo mengineyo
kwa kufuata utaratibu uliowekwa na sheria iliyotungwa na Baraza la
Wawakilishi.
3.(1) Kutakuwa na Muhuri wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
ambao alama yake itakuwa kama itavyokubaliwa na sheria iliyotungwa
na Baraza la Wawakilishi.
(2) Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itakuwa na uwezo wa
kuweka kitu chochote kitachokuwa kielelezo cha Serikali kama
itavyokubaliwa na sheria iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi.
4. Katiba hii ni Katiba ya Zanzibar na itakuwa na nguvu za kisheria
nchini kote na isipokuwa kutokana na kifungu 80 ikiwa sheria yoyote
inatofautiana na Katiba hii, basi Katiba hii ndiyo itayokuwa na nguvu
na sheria hiyo itakuwa batili kwa kiwango kile ambacho kinahitilafiana.
Zanzibar na
Muungano.
Kif. 4 cha
Sheria Nam.
9/2010.
Zanzibar
na mipaka
yake.
Kif. 3 cha
Sheria Nam.
9/2010.
Muhuri wa
Serikali na
alama
nyenginezo.
Katiba ya
Zanzibar.
Mikoa na
Wilaya za
Zanzibar.
Kif. 5 cha
Sheria
Nam.9/2010
1
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
5. Zanzibar itafuata mfumo wa Kidemokrasia wa Vyama Vingi
vya Siasa wenye kuheshimu utawala wa sheria, haki za binaadamu,
usawa, amani, haki na uadilifu.
5A.(1) Zanzibar itafuata mfumo wa mgawanyo wa madaraka kati
ya mamlaka tatu, Mamlaka ya Utendaji, Mamlaka ya Kutunga Sheria
na Kusimamia Utekelezaji wa Shughuli za Umma na Mamlaka ya
Kutekeleza Utoaji Haki.
(2) Mamlaka ya Utendaji ni Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,
Mamlaka ya kutunga Sheria na Kusimamia Utekelezaji wa Shughuli
za Umma ni Baraza la Wawakilishi na Mamlaka ya Kutekeleza Utoaji
Haki ni Mahkama.
(3) Hakuna mamlaka itakayoingilia Mamlaka nyengine
isipokuwa kama na kwa kadri ilivyoelezwa katika Katiba hii.
Sehemu ya Pili
Watu
6.(1) Kutakuwa na Mzanzibari ambaye upatikanaji wake, upoteaji
wake na urudishwaji wake atakuwa kama alivyoainishwa katika Sheria
iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi.
(2) Kila Mzanzibari, kwa misingi ya Katiba hii, ataweza kufaidi
haki na fursa zote anazostahiki Mzanzibari, na atapaswa kutekeleza
wajibu, majukumu na dhamana za Mzanzibari kama ilivyo kwenye
Katiba hii au kwenye Sheria iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi.
Mgawanyo
wa
madaraka
Kif. 4 cha
Sheria
Nam. 2/
2002.
Zanzibar
kufuata
mfumo wa
vyama
vingi.
Kif. 3 cha
Sheria Nam.
2/2002.
Mzanzibari.
Kif. 5 cha
Sheria
Nam. 2/
2002.
2
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
7.(1) Kila Mzanzibari aliyetimiza umri wa miaka kumi na nane
anayo haki ya kupiga kura katika uchaguzi unaofanywa Zanzibar na
wananchi. Na haki hii itatumiwa kwa kufuata masharti ya kijifungu cha
(2) cha kifungu hiki pamoja na masharti mengine ya Katiba hii na ya
Sheria inayotumika Zanzibar kuhusu mambo ya uchaguzi.
(2) Baraza la Wawakilishi laweza kutunga Sheria na kuweka
masharti yanayoweza kuzuia Mzanzibari asitumie haki ya kupiga kura
kutokana na yoyote kati ya sababu zifuatazo, yaani Mzanzibari huyo:
(a) kuwa na uraia wa nchi nyengine;
(b) kuwa na ugonjwa wa akili uliothibitishwa na Mahkama
Kuu;
(c) kutiwa hatiani na kuendelea kutumikia adhabu kwa
kosa la jinai katika Chuo cha Mafunzo, isipokuwa
kwamba mtu aliyewekwa rumande atakuwa na haki
ya kuandikishwa kupiga kura;
(d) kukosa au kushindwa kuthibitisha au kutoa
kitambulisho cha umri, uraia au uandikishwaji kama
mpiga kura.
(3) Baraza la Wawakilishi litatunga Sheria ya Uchaguzi inayohusu
uchaguzi wa Rais, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Madiwani
wa Serikali za Mitaa na kuweka masharti kuhusu mambo yafuatayo:
(a) kuanzisha daftari la kudumu la wapiga kura na kuweka
utaratibu wa kurekebisha yaliyomo katika daftari hilo;
(b) kutaja sehemu, nyakati za kuandikisha wapiga kura
na muda wa ukaazi katika Jimbo la Uchaguzi kwa ajili
ya kupiga kura;
Haki ya
kupiga
Kura.
Kif.6 cha
Sheria
Nam. 2/
2002.
3
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
(c) utaratibu wa kumwezesha mpiga kura aliyejiandikisha
sehemu moja kupiga kura sehemu nyengine na kutaja
masharti ya utekelezaji wa utaratibu huo;
(d) kutaja kazi na shughuli za Tume ya Uchaguzi na utaratibu
wa kila uchaguzi ambao utaendeshwa chini ya uongozi
na usimamizi wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar.
(4) Mbali na sababu zilizoelezwa katika kifungu hiki hakuna
sababu nyengine yoyote inayoweza kumzuia Mzanzibari asitumie haki
ya kupiga kura.
SURA YA PILl
Malengo na Maamuru Muhimu ya Sera ya Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar
8. Itakuwa ni wajibu wa vyombo vyote vya Serikali pamoja na
vyombo vyengine vyenye uwezo pamoja na watu wenye kutunga Sheria
kiutawala au uwezo wa kimahkama kufuata misingi ya uhuru, haki na
amani.
9.(1) Zanzibar itakuwa ni nchi ya kidemokrasia na haki za kijamii.
(2) Kwa hivyo hapa inaelezwa rasmi kwamba:
(a) mamlaka ya kuendesha nchi ni ya wananchi wenyewe
ambapo nguvu na uwezo wote wa Serikali kufuatana
na Katiba utatoka kwa wananchi wenyewe;
(b) usalama na hali nzuri kwa wananchi itakuwa ndiyo
lengo kubwa la Serikali;
4
Wajibu
mkubwa wa
Serikali.
Serikali na
watu.
Kif. 6 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(c) Katiba hii itahakikisha kwamba wananchi wanashiriki
katika Serikali yao.
(3) Muundo wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar utakuwa
wa Umoja wa Kitaifa na utendaji wa kazi zake utafanywa katika
utaratibu utakaohakikisha kuendelezwa kwa umoja nchini na lengo la
kufikia demokrasia.
10. Kwa madhumuni ya kuendeleza umoja na maendeleo ya watu
na ustawi wa jamii katika nchi itakuwa ni wajibu wa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar:-
(a) kutoa huduma za kutosha kwa ajili ya kuendeleza watu
katika njia za mtu kuwa huru kwenda atakapo na utoaji
huduma kwa watu wote na kutoa haki zote za kuishi
kwa Mzanzibari sehemu zote za Zanzibar;
(b) kuondosha kabisa vitendo vya rushwa na utumiaji mbaya
wa cheo dhidi ya umma kwa wale wote walio na
madaraka;
(c) kusimamia Maendeleo ya Uchumi wa Nchi kufuatana
na misingi na madhumuni yaliyowekwa na Katiba,
kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora, kuratibu na
kusimamia uendeshaji wa rasilimali muhimu za Nchi;
(d) kutoa mwongozo na kuhakikisha maendeleo ya uchumi
yenye urari na yaliyopangika na kwamba mfumo wa
kiuchumi hautafanyika katika utaratibu utakaopelekea
kulimbikiza kwa utajiri na njia za kuzalisha mali kwa watu
wachache au kikundi fulani;
5
Malengo ya
kisiasa.
Kif. 7 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
(e) kuhakikisha kwamba kila raia atakuwa na haki sawa,
majukumu na fursa sawa kwa mujibu wa sheria, utu wa
mtu utaheshimiwa na heshima ya mtu itaenziwa na
kuendelezwa na kwamba uhuru, kutopendelea na
uaminifu wa Mahkama pamoja na kupata fursa kwa
urahisi ya kwenda katika Mahkama hizo kutapatikana
na kuheshimiwa;
(f) kuhakikisha kwamba zipo huduma za kutosha za kiafya
kwa watu wote, zipo fursa sawa na za kutosha za kielimu
katika madaraja yote na kwamba utamaduni wa Zanzibar
unalindwa, unaimarishwa na unaendelezwa;
(g) kwamba kila mtu mwenye uwezo wa kufanyakazi ana
fursa ya kufanya kazi, na kazi maana yake ni shughuli
yoyote ya halali inayompatia mtu riziki yake, na kwamba
msaada unatolewa kwa wale wasiojiweza, wazee,
wagonjwa, watoto na walemavu;
(h) vyeo vyote vya madaraka ni dhamana na vipo kwa faida
na manufaa ya umma na wale wote walio na madaraka
watawajibika ama moja kwa moja kwa umma au kupitia
kwa vyombo vya uwakilishi;
(i) vyombo vyote vya Serikali na watumishi wake
vitaongozwa na vitazingatia Mikataba ya Kimataifa
kuhusu Haki za Binadamu na misingi ya utawala ulio bora.
10A. Masharti ya Sehemu hii ya Sura hii hayatatiliwa nguvu ya
kisheria na Mahkama yoyote, na Mahkama yoyote nchini haitakuwa
na uwezo wa kuamua juu ya suala kama kutenda au kukosa kutenda
jambo kama mtu au mamlaka yoyote au kama Sheria au hukumu
yoyote, inaambatana na masharti ya Sehemu hii ya Sura hii.
6
Mabadiliko
ya masharti
ya Sura ya
Pili.
Kif. 8 cha
Sheria
Nam. 2/
2002.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
SURA YA TATU
Kinga ya Haki za Lazima, Wajibu na Uhuru wa Mtu
Binafsi
11.(1) Binadamu wote huzaliwa huru, na wote ni sawa.
(2) Kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa
utu wake.
12.(1) Watu wote ni sawa mbele ya sheria, na wanayo haki, bila
ya ubaguzi wowote, kulindwa na kupata haki sawa mbele ya sheria.
(2) Hakuna sheria itakayokuwa na kifungu chochote ambacho
ni cha ubaguzi wa moja kwa moja au kwa taathira yake.
(3) Haki za raia, wajibu wa maslahi ya kila mtu yatalindwa na
kuamuliwa na Mahkama pamoja na vyombo vya nchi na vyenginevyo
vilivyowekwa na Sheria.
(4) Hakuna mtu atakayebaguliwa na mtu yeyote anayefanya
kazi chini ya sheria yoyote au katika utekelezaji wa kazi ya Afisi yoyote
ya Serikali au uongozi mwengine wa chama chochote na vyombo
vyake.
(5) Katika kifungu hiki neno “kubagua” maana yake ni kutimiza
haja kwa watu mbali mbali kwa kutegemea utaifa wao, kabila, jinsia,
ulemavu, pahala walipotokea, muelekeo wao kisiasa, rangi au dini
ambapo watu wa aina fulani wanaonekana kuwa ni dhaifu na duni au
wawekewe vikwazo na pingamizi ambavyo wale watu wa aina nyengine
hawawekeani au wanapewa fursa au faida ambayo hawapewi watu
wa aina nyengine.
7
Usawa
mbele ya
Sheria.
Kif. 9 cha
Sheria
Nam. 2/
2002 na
Kif. 8 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
Usawa
wa
Binaadamu.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
Isipokuwa kwamba neno “kubagua” halitafafanuliwa kwa
namna ambayo itazuia Serikali kuchukua hatua za makusudi zenye lengo
la kurekebisha matatizo mahsusi katika jamii.
(6) Kwa madhumuni ya kuhakikisha usawa mbele ya Sheria
Serikali itaweka taratibu zinazofaa na zitakazozingatia misingi kwamba:
(a) wakati haki na wajibu wa mtu yeyote vinahitaji
kufanyiwa uamuzi wa Mahkama au chombo
kinginecho kinachohusika basi mtu huyo atakuwa na
haki ya kupewa fursa ya kusikilizwa na pia haki ya
kukata rufaa au ya kupata kitulizo kinginecho cha
kisheria kutokana na maamuzi ya Mahkama au chombo
hicho kinginecho kinachohusika;
(b) mtu aliyeshtakiwa kwa kosa la jinai hatatendewa kama
mtu mwenye kosa hilo mpaka itakapothibitika kuwa
anayo hatia ya kutenda kosa hilo;
(c) ni marufuku kwa mtu kuadhibiwa kwa sababu ya
kitendo chochote ambacho alipokitenda hakikuwa ni
kosa chini ya sheria, na pia itakuwa ni marufuku kwa
adhabu kutolewa ambayo ni kubwa kuliko adhabu
iliyokuwepo wakati kosa linalohusika lilipotendwa;
(d) kwa ajili ya kuhifadhi haki ya usawa wa binadamu
katika shughuli zote zinazohusu upelelezi na
uendeshaji wa mambo ya jinai, katika shughuli
nyenginezo ambapo mtu anakuwa chini ya ulinzi bila
ya uhuru, na katika kuhakikisha utekelezaji wa adhabu,
heshima ya utu wa mtu itatunzwa;
(e) kesi za jinai zinasikilizwa na hukumu kusomwa haraka;
na
8
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(f) mtuhumiwa katika kesi ya jinai anapata fursa ya utetezi
wa Wakili aliyemchagua yeye mwenyewe.
13.(1) Kila mtu anayo haki ya kuwa na hifadhi ya maisha yake.
(2) Kila mtu anayo haki ya kuishi na kupata kutoka kwa jamii
hifadhi ya maisha yake kwa mujibu wa sheria.
(3) Ni marufuku kwa mtu kuteswa, kuadhibiwa kinyama au
kupewa adhabu zinazomtweza au kumdhalilisha.
14.(1) Kila mtu anayo haki ya kuwa huru na kuishi kama mtu
huru.
(2) Kwa madhumuni ya kuhifadhi haki ya mtu kuwa huru na
kuishi kwa uhuru, itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kukamatwa,
kufungwa, kufungiwa, kuwekwa kizuizini, kuhamishwa kwa nguvu au
kunyang’anywa uhuru wake vyenginevyo isipokuwa tu:
(a) katika hali na kwa kufuata utaratibu uliowekwa na
sheria; au
(b) katika kutekeleza hukumu, amri au adhabu iliyotolewa
na Mahkama kutokana na shauri au kosa la jinai
ambalo mtu amekutwa na hatia ya kulitenda.
15.(1) Kila mtu anastahili kuheshimiwa na kupata hifadhi kwa
nafsi yake, maisha yake binafsi na ya nyumbani kwake, na pia heshima
na hifadhi ya maskani yake na mawasiliano yake.
(2) Kwa madhumuni ya kuhifadhi haki ya mtu kwa mujibu wa
kifungu hiki, Mamlaka ya nchi itaweka utaratibu wa sheria kuhusu hali,
9
Haki ya
kuwa hai.
Kif. 10 cha
Sheria
Nam. 2/
2002
Haki ya
uhuru wa
mtu binafsi.
Haki ya
faragha ya
mtu na
usalama
wake.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
namna ya kiasi ambacho haki ya mtu na faragha na usalama wa nafsi
yake, mali yake na maskani yake, yaweza kuingiliwa bila ya kuathiri
kifungu hiki cha Katiba hii.
16.(1) Hakuna mtu atakayenyimwa uhuru wake wa kwenda, na
kwa madhumuni ya kifungu hiki uhuru uliotajwa humu maana yake ni
haki ya kwenda popote katika Zanzibar, haki ya kuishi katika sehemu
yoyote ya Zanzibar, haki ya kuingia Zanzibar, haki ya kuondoka
Zanzibar na kinga ya kutofukuzwa Zanzibar.
(2) Kizuizi cha kutokutembea kwa mtu yeyote kutokana na
kuwekwa ndani kwake kisheria, haitochukuliwa kuwa inapingana au
ni kinyume na kifungu hiki.
17. Hakuna mali ya mtu yeyote itayochukuliwa kwa nguvu na
hakuna maslahi au haki yoyote inayotokana na mali hiyo itayochukuliwa
kwa nguvu isipokuwa pale ambapo masharti yafuatayo yametimizwa,
yaani:
(a) kumilikiwa au kuchukuliwa kwa mali hiyo ni muhimu
sana kwa ajili ya ulinzi, usalama wa wananchi, mazingira
ya afya, kuimarisha maendeleo ya upangaji wa mji
pamoja na kuendeleza mambo ambayo yataleta faida
kwa wananchi kwa ujumla;
(b) umuhimu wa kuchukuliwa kitu hicho ni mkubwa sana
hata kwamba unahalalisha uchukuaji wake hata kama
utampa ugumu na matatizo mwenye mali hiyo; na
(c) sheria imewekwa kuhusiana na umilikaji au uchukuaji
huo kwa kutoa fidia inayolingana.
10
Kinga ya
uhuru wa
kwenda.
Kinga
kutokana
na
kudhulumiwa
mali.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
18.(1) Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na
maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta kupokea na
kutoa habari na dhana kupitia chombo chochote, bila ya kujali mipaka
ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati.
(2) Kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu
matukio mbali mbali nchini na duniani kote ambayo ni muhimu kwa
maisha na shughuli za wananchi, na pia juu ya masuala muhimu kwa
jamii.
19.(1) Kila mtu anastahili kuwa na uhuru wa mawazo, wa imani
na wa uchaguzi katika mambo ya dini, pamoja na uhuru wa kubadilisha
dini au imani yake.
(2) Bila ya kuathiri sheria zinazohusika kazi ya kutangaza dini,
kufanya ibada na kueneza dini itakuwa huru na jambo la hiari ya mtu
binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya
shughuli za Mamlaka ya nchi.
(3) Kila palipotajwa neno “dini” katika kifungu hiki ifahamike
kwamba maana yake ni pamoja na madhehebu ya dini, na maneno
mengineyo yanayofanana au kuambatana na neno hilo nayo
yatatafsiriwa kwa maana hiyo.
20.(1) Isipokuwa kwa hiari yake, hakuna mtu atakayezuiwa
kufurahia uhuru wake wa kuchanganyika au kujiunga yaani haki yake
ya kuchanganyika na kujihusisha atakavyo na watu wengine na hasa
kuunda au kuwa mwanachama wa vyama vya wafanyakazi, vyama
vya haki za binadamu au vyama vyengine kwa faida yake na ambavyo
vimekubaliwa kisheria.
Uhuru wa
maoni.
11
Uhuru wa
mtu kuamini
dini atakayo.
Kif. 11 cha
Sheria Nam.
2/2002.
Kinga kwa
uhuru wa
kujikusanya
na
kujiunga.
Kif. 12 cha
Sheria
Nam. 2/
2002.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
(2) Hakuna chochote kilichomo ndani ya au kufanywa chini
ya sheria yoyote kitakachohesabiwa kuwa hakilingani au ni kinyume
na kifungu hiki (katika kiwango ambacho sheria mama inaeleza):
(a) mambo yanayotakiwa kwa faida ya ulinzi, usalama
wa raia, mazingira ya afya na jamii;
(b) mambo yanayotakiwa kwa madhumuni ya kulinda
haki na uhuru wa watu wengine;
(c) mambo yanayotakiwa kuweka makatazo fulani kwa
maafisa wa Serikali, Wanajeshi au watu wanaofanya
kazi waliochaguliwa kwa hiari.
21.(1) Kila Mzanzibari anayo haki ya kushiriki katika shughuli za
utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia Wawakilishi
waliochaguliwa kwa hiari.
(2) Kila Mzanzibari anayo haki na uhuru wa kushiriki kwa
ukamilifu katika kufikia uamuzi juu ya mambo yanayomhusu yeye maisha
yake au yanayolihusu Taifa.
(3) Kila Mzanzibari anayo haki ya kufanya kazi na anastahili
fursa na haki sawa, kwa masharti ya usawa ya kushika nafasi yoyote
ya kazi na shughuli yoyote iliyoko chini ya Mamlaka ya Zanzibar.
(4) Kila mtu, bila ya kuwapo ubaguzi wa aina yoyote, anayo
haki ya kupata ujira unaolingana na kazi yake na watu wote wafanyao
kazi kulingana na uwezo wao watapata malipo kulingana na kiasi ya
sifa za kazi wanayoifanya.
12
Uhuru wa
kushiriki
shughuli za
umma, haki
ya kufanya
kazi na
kupata
ujira.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
22.(1) Kazi pekee ndiyo huzaa utajiri wa mali katika jamii, ndio
chimbuko la ustawi wa wananchi na kipimo cha utu, kila mtu anao
wajibu wa:
(a) kushiriki kwa kujituma na kwa uaminifu katika kazi
halali na ya uzalishaji mali; na
(b) kutimiza nidhamu ya kazi na kujitahidi kufikia malengo
ya uzalishaji ya binafsi na ya pamoja yanayotakiwa
au yaliyowekwa na sheria.
(2) Bila ya kujali masharti ya kijifungu cha (1) hakutakuwepo
na kazi ya shurti katika Zanzibar.
23.(1) Kila mtu ana wajibu wa kufuata na kutii Katiba hii na Sheria
za Zanzibar, kuchukua hatua za kisheria kama zilivyowekwa,
kuhakikisha hifadhi ya Katiba na Sheria za nchi.
(2) Kila mtu ana wajibu wa kulinda maliasili ya Zanzibar, mali
ya nchi na mali yote inayomilikiwa kwa pamoja na wananchi, na pia
kuiheshimu mali ya mtu mwengine.
(3) Watu wote watatakiwa na sheria kulinda vizuri mali ya
Zanzibar na kwa pamoja kupiga vita aina zote za uharibifu na ubadhirifu
na kuendesha uchumi wa Zanzibar kwa makini kama watu ambao
ndio waamuzi wa hali ya baadae ya Taifa lao.
(4) Kila Mzanzibari anawajibu wa kulinda, kuhifadhi kudumisha
uhuru, mamlaka, ardhi na umoja wa Zanzibar.
(5) Baraza la Wawakilishi laweza kutunga sheria zinazofaa
kwa ajili ya kuwawezesha wananchi kutumikia katika majeshi na katika
ulinzi wa Taifa.
13
Wajibu wa
kushiriki
kazini.
kif. 13 cha
Sheria
Nam. 2/
2002.
Wajibu wa
kutii sheria
za nchi,
kulinda
mali ya
umma na
ulinzi wa
Taifa.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
24.(1) Haki na Uhuru wa binadamu ambayo misingi yake
imeorodheshwa na Katiba hii haitatumiwa na mtu mmoja kwa namna
ambayo itasababisha kuingiliwa kati au kukatizwa kwa haki na uhuru
wa watu wengine au maslahi ya umma na inaweza kubanwa na sheria
iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi iwapo tu kibano hicho ni lazima
na kinakubalika katika mfumo wa kidemokrasia. Kwa vyovyote vile
kibano hicho:
(a) hakitaingilia haki ya kutokuteswa, kutoadhibiwa
kinyama na kutokudhalilishwa; au
(b) hakitaingilia misingi ya haki yenyewe; au
(c) hakitailetea jamii athari zaidi ya iliyopo kutokana na
jambo ambalo kibano hicho kinalenga.
(2) Mtu yeyote anayedai kuwa sharti lolote katika Sehemu hii
ya Sura hii au katika sheria yoyote inayohusu haki yake au wajibu
wake limevunjwa, linavunjwa au inaelekea litavunjwa na mtu yeyote
Zanzibar, anaweza kufungua shauri katika Mahkama Kuu. Mahkama
Kuu itakuwa na uwezo wa kutoa tamko na kuamuru nafuu au fidia
kwa mtu yeyote anayehusika.
(3) Rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahkama Kuu katika shauri
lililofunguliwa dhidi ya masharti ya Sura hii ya Katiba yatasikilizwa na
Mahkama Kuu mbele ya Majaji watatu bila ya kumjumuisha Jaji
aliyeamua shauri hilo mara ya kwanza. Majaji hao watatu watateuliwa
na Jaji Mkuu na uamuzi wao utakuwa ni wa mwisho na hautokatiwa
rufaa kwenye Mahkama ya Rufaa ya Tanzania.
(4) Bila ya kuathiri masharti mengineyo yaliyomo katika Katiba
hii, Mahkama Kuu itakuwa na mamlaka ya kusikiliza kwa mara ya
kwanza shauri lolote lililoletwa mbele yake kwa kufuata kifungu hiki,
na Mamlaka ya nchi yaweza kuweka sheria kwa ajili ya:
14
Mipaka kwa
haki na
uhuru, na
hifadhi kwa
haki na
wajibu.
Kif. 14 cha
Sheria Nam
2/2002 na
Kif. 9 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(a) kusimamia utaratibu wa kufungua mashauri kwa
mujibu wa kifungu hiki;
(b) kufafanua uwezo wa Mahkama Kuu katika kusikiliza
mashauri yaliyofunguliwa chini ya kifungu hiki;
(c) kuhakikisha utekelezaji bora wa madaraka ya
Mahkama Kuu, hifadhi na kutilia nguvu, haki, uhuru
na wajibu kwa mujibu wa Katiba hii.
25.(1) Ilivyokuwa kila mtu wa Zanzibar anawajibika kupata haki
zake za lazima na uhuru wa binafsi bila ya kujali kabila, pahali alipotoka
au maskani au mahusiano mengine yoyote yale, mtazamo wa kisiasa
alionao, rangi, dini au jinsi, lakini mradi iwe uhuru wake unaheshimu
haki na uhuru wa wengine na iwe kwa faida ya jamii, basi atakuwa na
haki kupata kwa kila kimoja kwa vyote vya hivi vifuatavyo:
(a) maisha yake, uhuru wake, usalama wake na kulindwa
na sheria;
(b) uhuru wa kufikiri, wa kujieleza, wa mkusanyiko na
mchanganyiko; na
(c) haki ya kuweza kukaa faragha katika nyumba yake
na kulindwa kwa mali yake pamoja na
kutokuchukuliwa mali hiyo bila kupewa fidia
ipasavyo.
(2) Maelezo ya Sura hii yatakuwa na madhumuni ya kuwezesha
kulinda haki hizo na uhuru kulingana na mipaka maalumu ya haki hizo
na uhuru kama ilivyoelezwa katika vifungu vinavyohusika kwa mipaka
iliyowekwa ili kuhakikisha kwamba kutumika kwa haki hizo na uhuru
huo wa mtu binafsi hakuathiri haki na uhuru wa wengine au maslahi ya
Taifa kwa ujumla.
15
Haki za
lazima na
uhuru wa
binafsi.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
25A.(1) Mtu yeyote anaweza kufungua shauri katika Mahkama
Kuu iwapo ataona kuwa Katiba hii imevunjwa au inavunjwa au
inaelekea kuvunjwa. Mahkama Kuu itakuwa na uwezo wa:-
(a) kumtaka Afisa yeyote au chombo chochote cha
Serikali kutoa taarifa inayohitajika na Mahkama
Kuu yaweza kufanya hivyo kwa kuombwa au kwa
uamuzi wake yenyewe;
(b) kutamka na kutoa amri kuwa Katiba hii imevunjwa,
inavunjwa au inaelekea kuvunjwa, na Mahkama
Kuu inaweza kutoa maagizo kwa Afisa anayehusika
au chombo cha Serikali kinachohusika.
(2) Rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahkama Kuu katika shauri
lililofunguliwa dhidi ya masharti ya kifungu hiki itasikilizwa kwa mujibu
wa masharti ya kifungu cha 24(3) cha Katiba.
SURA YA NNE
Serikali
Sehemu ya Kwanza
Rais
26.(1) Kutakuwa na Rais wa Zanzibar ambaye atakuwa Mkuu
wa Nchi ya Zanzibar, Kiongozi Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.
(2) Mtu yeyote anaweza kufaa kuchaguliwa kuwa Rais ikiwa:
(a) ni Mzanzibari wakuzaliwa; na
(b) ameshatimia umri wa miaka 40; na
16
Kufungua
mashauri.
Kif. 15 cha
Sheria
Nam. 2/
2002 na
Kif. 10 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
Afisi ya
Rais na
sifa za
kuchaguliwa
kuwa Rais.
Kif. 3 cha
Sheria
Nam. 13/
1992 na
Kif. 11
cha Sheria
Nam. 9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(c) anazo sifa za kumuwezesha kuchaguliwa kuwa
Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi; na
(d) ni mwanachama na mgombea aliyependekezwa na
chama cha siasa kilichosajiliwa rasmi kwa mujibu wa
Sheria ya Vyama vya Siasa ya 1992.
27.(1) Rais atachaguliwa kufuatana na Katiba hii na kwa mujibu
wa sheria yoyote itakayotungwa na Baraza la Wawakilishi kuhusu
uchaguzi wa Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.
(2) Uchaguzi wa Rais utafanyika katika tarehe itayowekwa na
Tume ya Uchaguzi.
(3) Kwa madhumuni ya uchaguzi huo, Zanzibar itahesabika
kuwa ni jimbo moja. Mtu yeyote aliyejiandikisha kupiga kura katika
kumchagua Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi atakuwa na uwezo wa
kupiga kura katika uchaguzi wa Rais.
28.(1) Kufuatana na Katiba hii mtu ataendelea kuwa Rais mpaka:
(a) Rais anayefuata ale kiapo cha kuwa Rais; au
(b) afariki wakati akiwa Rais; au
(c) hapo atapojiuzulu; au
(d) iwapo amechaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania; au
(e) kwa sababu yoyote nyengine ameacha kuwa
Kiongozi kwa mujibu wa vifungu vyengine vya Katiba
hii.
17
Muda wa
kuendelea
na Urais.
Kif. 13 cha
Sheria
Nam. 9/
2010.
Uchaguzi
wa Rais.
Kif. 12 cha
Sheria
Nam. 9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
(2) Kufuatana na maelezo ya kijifungu (1) cha kifungu hiki,
Rais ataacha madaraka yake baada ya kumalizika miaka mitano
kuanzia tarehe, ambapo:
(a) kama yeye ni mtu ambaye ndiye mara ya kwanza
amechaguliwa kuwa Rais chini ya Katiba hii alipokula
kiapo cha uaminifu na kiapo cha kuwa Rais; na
(b) kwa sababu nyenginezo mtu wa mwisho kushika
madaraka hayo kwa mujibu wa Katiba hii alipokula
kiapo cha uaminifu na kiapo cha kuwa Rais, au
pasingelikuwa na sababu ya kifo chake, basi angalikula
kiapo hicho.
(3) Bila ya kuathiri chochote kilichomo katika kifungu hiki
cha Katiba hii hakutakua na mtu yeyote ataechaguliwa kuwa Rais wa
Zanzibar kwa zaidi ya vipindi viwili vya miaka mitano kila kimoja.
29. Ikiwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imo katika vita na
ikiwa Rais anaona kuwa ni muhimu kuzuia uchaguzi, Baraza la
Wawakilishi linaweza kwa kupitisha Azimio, kuzidisha muda wa miaka
mitano uliotajwa kwenye kijifungu (2) cha kifungu cha 28 katika kipindi
hadi kipindi lakini hakutakuwa na kipindi kitakachozidi miezi sita
mfululizo.
30.(1) Mtu hatofaa kuchaguliwa kuwa Rais ikiwa:
(a) amefanya kitendo chochote, au hitilafu yoyote ambapo
kama angekuwa ni Mjumbe wa Baraza la
Wawakilishi kungemfanya asite kuwa Mjumbe wa
Baraza hilo;
(b) amechaguliwa kushika madaraka hayo katika vipindi
viwili vilivyokwisha;
18
Kutofaa
kuwa Rais.
Kif. 15 cha
Sheria Nam.
9/2010.
Kuongezwa
kwa kipindi
cha miaka
mitano.
Kif. 14 cha
Sheria
Nam. 9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
Isipokuwa kwamba kijifungu hiki kisitafsirike kuwa kinamzuia
mtu huyo kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
(2) Katika muda wake wa Urais, Rais hatashika madaraka
yoyote mengine yenye mapato isipokuwa yale ya Urais.
31.(1) Mtu anayechukua madaraka ya Urais, kabla ya kuanza
wadhifa huo, atakula kiapo cha uaminifu na kiapo cha kazi kama
kitavyowekwa na Baraza la Wawakilishi lakini kwa hali yoyote itabidi
ashike madaraka hayo kabla ya kupita siku saba baada ya kuchaguliwa.
(2) Viapo hivyo vilivyotajwa vitaendeshwa na Jaji Mkuu wa
Zanzibar au iwapo hayupo, vitaendeshwa na mtu anayeshikilia nafasi
hiyo.
32.(1) Suala lolote la kwamba Rais au mtu yeyote anayefanya
kazi au kutaka kufanya kazi za Rais, hawezi kwa sababu ya maradhi
ya kimwili au kiakili, itaamuliwa kwa mujihu wa kifungu hiki.
(2) Iwapo suala ni kwamba Rais hawezi kufanya kazi zake
kwa maradhi ya kimwili au kiakili na ikiwa Jaji Mkuu ameombwa na
Baraza la Mapinduzi, kushughulikia suala hilo, hapo:-
(a) Jaji Mkuu atateua Kamati ambayo itakuwa na watu
si chini ya watano ambao kati yao ni Madaktari na
watu wawili wanaofaa kuwa Majaji wa Mahkama
Kuu;
(b) Kamati hiyo itafanya utafiti kuhusiana na hali ya Rais
na baadae itapeleka ripoti yake kwa Jaji Mkuu
ikieleza maoni yake iwapo Rais huyo kwa maradhi
19
Kuachishwa
Urais kwa
ugonjwa.
Kif. 16
Sheria
Nam. 9/
2010.
Kiapo cha
Rais.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
aliyonayo ya kimwili au akili, kama hawezi kufanya
kazi za Urais; na
(c) Jaji Mkuu atathibitisha kwa kadri aonavyo baada
ya kuitafakari ripoti ya Kamati na atapeleka hati ya
uthibitisho kwamba Rais hawezi kumudu kufanya kazi
zake kutokana na maradhi ya kimwili au akili kwa
Baraza la Mapinduzi na kwa Spika wa Baraza la
Wawakilishi na iwapo Jaji Mkuu hatabatilisha
uthibitisho wake ndani ya siku saba kutokana na Rais
kupata nafuu na kurejea kazini, basi itahesabiwa
kwamba kiti cha Rais kiwazi kwa mujibu wa kifungu
33(1)(c) cha Katiba na masharti yaliyomo katika
kifungu cha 34(1) cha Katiba yatatumika.
33.(1) Endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kwa:
(a) kufariki; au
(b) kujiuzulu; au
(c) maradhi ya kimwili au kiakili; au
(d) sababu nyengine yoyote itakayomfanya Rais
kushindwa kutekeleza kazi za Rais,
watu wafuatao, kwa mujibu wa mpangilio, watashika nafasi hiyo:
(i) Makamo wa Pili wa Rais, au ikiwa hayupo;
(ii) Spika wa Baraza la Wawakilishi ambaye
anatoka katika chama anachotoka Rais na yeye
ikiwa hayupo;
(iii) Jaji Mkuu wa Zanzibar.
20
Nafasi
katika kiti
cha Urais.
Kif. 17 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(2) Iwapo kiti cha Urais:
(a) kwa sababu Rais anataka kuondoka Tanzania; au
(b) kwa sababu nyengine yoyote ile,
Rais anaweza kwa maandishi na kufuatana na masharti atakayoainisha
akayatoa madaraka yake kwa mujibu wa mpangilio, kwa:
(i) Makamo wa Pili wa Rais au naye ikiwa hayupo;
(ii) Mjumbe mmoja wa Baraza la Mapinduzi ambaye
Rais ataona anafaa.
(3) Iwapo mtu yeyote anafanya shughuli za Rais chini ya
vijifungu (1) na (2) vya kifungu hiki, ataendelea kufanya shughuli hizo
mpaka ataporejea mmoja ya watu waliomtangulia katika kijifungu cha
(1) cha kifungu hiki mpaka hapo atapochaguliwa Rais mwengine au
kwa shughuli za kijifungu cha (2) hadi hapo Rais ataporejea nchini au
atapobatilisha uwezo huo alionao.
34.(1) Endapo kiti cha Rais kiwazi kwa sababu ya kufariki au
kujiuzulu au kwa maradhi chini ya kifungu cha 33 cha Katiba hii, nafasi
hiyo itajazwa kama ifuatavyo:
(i) iwapo Rais aliyekuwapo ametumikia kwa muda wa
chini ya miaka minne basi mtu anayemfuatia kwa
madaraka kwa mujibu wa kifungu cha 33(1) cha
Katiba atachukua madaraka ya Urais kwa muda na
uchaguzi utaitishwa ndani ya siku mia moja na ishirini,
na uchaguzi huo utaendeshwa kwa utaratibu
ulioelezwa katika vijifungu vya (2) hadi (7) vya
kifungu hiki;
21
Mpango wa
uchaguzi
iwapo kiti
cha Rais
kiwazi.
Kif.4 Sheria
Nam13/
1992,
Kif.2 cha
Sheria Nam.
11/1995, na
Kif. 18 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
(ii) iwapo Rais aliyekuwepo ametumikia Urais kwa
miaka minne au zaidi, basi mtu anayemfuatia kwa
madaraka atachukua madaraka ya Urais na
ataendelea na madaraka hayo kwa kipindi
kilichobaki cha muda wa Urais.
(iii) mtu atayechukua madaraka hayo ya Urais atakuwa
na madaraka yote ya Rais, kwa mujibu wa Katiba
na atateua Makamo wa Kwanza wa Rais na
Makamo wa Pili wa Rais Mawaziri na Viongozi
wengine kadri atavyoona inafaa.
(iv) bila ya kujali masharti ya vifungu vya 28(3) na
30(1)(b) vya Katiba, endapo mtu anayemfuata Rais
kwa madaraka atashika kiti cha Rais kwa kipindi
kinachopungua miaka minne ataruhusiwa kugombea
nafasi ya Rais mara mbili, lakini kama atashika kiti
cha Rais kwa muda wa miaka minne au zaidi
ataruhusiwa kugombea nafasi ya Rais mara moja tu.
(2) Litokeapo jambo lolote lilotajwa katika Katiba na kulazimu
uchaguzi wa Rais kufanyika, kila chama cha siasa kinachopenda
kushiriki katika uchaguzi wa Rais kitawasilisha kwa Tume ya Uchaguzi
ya Zanzibar, kwa mujibu wa Sheria, jina la mwanachama wake mmoja
kinayetaka asimame kama mgombea katika uchaguzi wa Rais wa
Zanzibar.
(3) Mapendekezo ya majina ya wagombea katika uchaguzi
wa Rais yatawasilishwa kwa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar katika
siku na saa itakayotajwa kwa mujibu wa Sheria iliyotungwa na Baraza
la Wawakilishi, na mtu hatakuwa amependekezwa kwa halali isipokuwa
tu kama kupendekezwa kwake kumeungwa mkono na wananchi
wapiga kura kwa idadi na kwa namna itakayotajwa na Sheria
iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi.
22
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(4) Endapo inapofika siku na saa iliyotajwa kwa ajili ya
kuwasilisha mapendekezo ya majina ya wagombea, ni mgombea mmoja
tu ambaye amependekezwa kwa halali, Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar,
itawasilisha jina lake kwa wananchi, nao watapiga kura ya kumkubali
au kumkataa, kwa mujibu wa masharti ya kifungu hiki na ya Katiba.
(5) Uchaguzi wa Rais wa Zanzibar utafanywa siku
itakayoteuliwa, na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kwa mujibu wa Sheria
iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi.
(6) Mambo mengine yote yahusuyo utaratibu wa uchaguzi wa
Rais yatakuwa kama itakavyofafanuliwa katika Sheria iliyotungwa na
Baraza la Wawakilishi kwa ajili hiyo.
(7) Iwapo mgombea ametangazwa na Tume ya Uchaguzi ya
Zanzibar kwamba amechaguliwa kuwa Rais kwa mujibu wa kifungu
hiki, basi hakuna Mahkama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya
kuchunguza kuchaguliwa kwake.
35.(1) Rais atapokea mshahara na posho, na anapostaafu atapata
malipo ya uzeeni, kiinua mgongo au posho, kama itakavyoamuliwa na
Baraza la Wawakilishi.
(2) Mshahara na posho la Rais hautopunguzwa wakati akiwa
bado ni Rais.
(3) Pesa zote zilizoainishwa na kifungu hiki zitatoka kwenye
Mfuko Mkuu wa Hazina.
36.(1) Hakuna mashtaka yoyote ya jinai yatakayofunguliwa au
kuendelezwa dhidi ya Rais wakati akiwa kazini, au dhidi ya mtu yeyote
ambaye anafanya kazi ya Urais, kwa mujibu wa kifungu cha 33 cha
Katiba hii.
23
Mshahara
na malipo
mengine
ya Rais.
Rais
hatashtakiwa
akiwa
kazini.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
(2) Hakuna mashtaka ya kihukukia ambapo kuna madai
kuhusiana na kitu chochote kilichotendwa au kuachwa kutendwa
yatakayoanzishwa na kuendelezwa dhidi ya Rais wakati akiwa kazini,
au dhidi ya yeyote anayefanya kazi za Urais.
(3) Iwapo kuna sheria imewekwa ambayo inaweka muda
maalum ambapo mashtaka ya aina yoyote yanaweza kuanzishwa dhidi
ya mtu yeyote muda wote ambapo mtu anakuwa Rais au kufanyakazi
za Rais hautahesabiwa kuwa ni muda maalum kuhusiana na sheria hiyo
iwapo mashtaka yoyote ya aina kama yaliyotajwa katika kijifungu cha
(1) au (2) ni dhidi ya mtu huyo.
37.(1) Bila ya kujali masharti ya kifungu cha 36 cha Katiba hii,
Baraza la Wawakilishi linaweza kupitisha Azimio la kumuondoa Rais
madarakani endapo itatolewa hoja ya kumshtaki Rais na ikapitishwa
kwa mujibu wa masharti ya kifungu hiki.
(2) Bila ya kuathiri masharti mengineyo ya kifungu hiki, hoja
yoyote ya kumshtaki Rais haitotolewa isipokuwa tu kama inadaiwa
kwamba Rais ametenda vitendo vinavyovunja Katiba au amekuwa na
mwenendo unaodhalilisha kiti cha Rais, na haitatolewa hoja ya namna
hiyo ndani ya miezi kumi na mbili tangu hoja kama hiyo ilipotolewa na
ikakataliwa na Baraza la Wawakilishi.
(3) Baraza la Wawakilishi halitapitisha hoja ya kumshtaki Rais
isipokuwa tu kama:
(a) taarifa ya maandishi iliyotiwa sahihi na kuungwa
mkono na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi
wasiopungua nusu ya Wajumbe wote wa Baraza la
Wawakilishi itatolewa kwa Spika siku thalathini kabla
ya kuwasilishwa katika Baraza la Wawakilishi
24
Baraza la
Wawakilishi
laweza
kumshtaki
Rais.
Kif. 5 cha
Sheria
Nam 13/
1992 na
Kif. 19 cha
Sheria
Nam. 9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
ikifafanua makosa aliyoyatenda Rais, na ikipendekeza
kuwa Kamati Maalum ya Uchunguzi iundwe ili isikilize
shauri la kushtakiwa kwa Rais;
(b) wakati wowote baada ya Spika kupokea taarifa
iliyotiwa sahihi na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi
itatolewa kwa Spika na kujiridhisha kwa masharti ya
kuleta hoja yametimizwa, Spika atalitaka Baraza la
Wawakilishi, bila ya majadiliano, lipige kura juu ya
hoja ya kuunda Kamati Maalum ya Uchunguzi na
kama ikiungwa mkono na Wajumbe wa Baraza la
Wawakilishi wasiopungua theluthi mbili ya Wajumbe
wote wa Baraza la Wawakilishi, atatangaza majina
ya wajumbe wa Kamati Maalum ya Uchunguzi;
(c) Kamati Maalum ya Uchunguzi, kwa madhumuni ya
kifungu hiki, itakuwa na wajumbe wafuatao, yaani:
(i) Jaji Mkuu wa Zanzibar, ambaye ndiye atakuwa
Mwenyekiti wa Kamati;
(ii) Jaji wa Mahkama ya Rufaa ya Tanzania;
(iii) Jaji kutoka nchi yoyote ya Jumuiya ya Madola;
(iv) Wajumbe wanne wa Kamati ya Katiba na Sheria
ya Baraza la Wawakilishi akiwemo Mwenyekiti.
(d) ndani ya siku saba baada ya Kamati Maalum ya
Uchunguzi kuundwa, itakaa, ichunguze na kuchambua
mashtaka dhidi ya Rais na kisha mapema
iwezekanavyo itatoa taarifa kwa Baraza la
25
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
Wawakilishi kama kwa maoni yake mashtaka dhidi
ya Rais yana msingi au hayana;
(e) Rais atakuwa na haki ya kujitetea na kuwakilishwa
mbele ya Kamati Maalum ya Uchunguzi.
(4) Endapo Kamati Maalum ya Uchunguzi itatoa taarifa kwa
Baraza la Wawakilishi kwamba jambo lolote katika mashtaka dhidi ya
Rais halina msingi, basi Baraza la Wawakilishi halitaendelea
kuishughulikia zaidi hoja ya kumshtaki Rais kuhusiana na jambo hilo.
(5) Endapo Kamati Maalum ya Uchunguzi itatoa taarifa kwa
Baraza la Wawakilishi kwamba mashtaka dhidi ya Rais yana msingi,
suala la kushtakiwa Rais litawasilishwa mbele ya Baraza la Wawakilishi
zima, na Baraza la Wawakilishi laweza, baada ya mjadala, kwa kura
za Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wasiopungua theluthi mbili za
Wajumbe wote wa Baraza la Wawakilishi kupitisha Azimio kuwa
mashtaka dhidi ya Rais yamethibitika na kwamba hastahili kuendelea
kushika kiti cha Rais, na hapo Rais atawajibika kujiuzulu kabla ya
kwisha kwa siku tatu tangu Baraza la Wawakilishi lilipopitisha Azimio
hilo.
(6) Spika wa Baraza la Wawakilishi atawasilisha rasmi Azimio
hilo kwa Rais pamoja na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya
Zanzibar.
(7) Hakuna shughuli zozote kwa mujibu wa kifungu hiki
zitakazoanzishwa au zitakazoendelezwa wakati wowote ambapo
Baraza la Wawakilishi litakua limeahirishwa.
(8) Endapo Rais ataacha kushika kiti cha Rais kutokana na
mashtaka dhidi yake kuthibitika, basi:-
26
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(i) hatakuwa na haki ya kupata malipo yoyote ya
pencheni walakupata haki au nafuu nyenginezo
alizonazo kwa mujibu wa Katiba au Sheria yoyote
iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi; na
(ii) hataweza kugombea tena nafasi ya Urais au
Uwakilishi kwa muda wa miaka mitano tokea siku
aliyoachishwa Urais;
Isipokuwa pindi Rais huyo akiwa ameshatumikia kipindi cha
miaka mitano ya awali na akakutwa na mashtaka katika kipindi cha
pili basi atapata nusu ya haki na nafuu nyengine alizonazo kwa mujibu
wa Katiba au Sheria yoyote iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi.
38. Itakuwa ni jukumu la Serikali kulinda hadhi ya mtu yeyote
atakaeacha kiti cha Urais kwa sababu ya kutochaguliwa tena, muda
wake kumalizika, kujiuzulu au kwa sababu nyengine yoyote iliyochini
ya misingi ya Katiba hii kama itavyokubaliwa na Sheria iliyotungwa na
Baraza la Wawakilishi.
Sehemu ya Pili
Makamo wa Kwanza wa Rais na Makamo wa Pili wa Rais
39.(1) Kutakuwa na Makamo Wawili wa Rais ambao watajuilikana
kama Makamo wa Kwanza wa Rais na Makamo wa Pili wa Rais.
(2) Ndani ya siku saba mara baada ya kushika madaraka,
Rais atateua Makamo wa Kwanza wa Rais na Makamo wa Pili wa
Rais.
(3) Makamo wa Kwanza wa Rais atatakiwa awe na sifa za
kumuwezesha kuchaguliwa kuwa Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi
27
Hadhi ya
Rais
aliyepita.
Makamo
wawili wa
Rais.
Kif. 21 cha
Sheria
Nam. 9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
na atateuliwa na Rais baada ya kushauriana na chama kilichotokea
nafasi ya pili katika matokeo ya kura ya Uchaguzi wa Rais.
Isipokuwa kwamba:-
(i) iwapo chama kilichotokea nafasi ya pili katika
matokeo ya kura ya Uchaguzi wa Rais kimepata chini
ya asilimia kumi (10%) ya kura zote za Uchaguzi wa
Rais, au
(ii) endapo Rais atakuwa hana mpinzani,
basi nafasi ya Makamo wa Kwanza wa Rais itapewa chama chochote
cha upinzani kilichotokea cha pili kwa wingi wa viti vya Majimbo katika
Baraza la Wawakilishi.
(4) Makamo wa Kwanza wa Rais hatokuwa Mjumbe wa
Baraza la Wawakilishi.
(5) Makamo wa Kwanza wa Rais atakuwa ni Mshauri Mkuu
wa Rais katika kutekeleza kazi zake na atafanya kazi zote
atakazopangiwa na Rais.
(6) Makamo wa Pili wa Rais atateuliwa na Rais kutoka miongoni
mwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kutoka katika chama
anachotoka Rais.
(7) Makamo wa Pili wa Rais atakuwa ndiye Mshauri Mkuu
wa Rais katika kutekeleza kazi zake na pia atakuwa ndiye Kiongozi
wa shughuli za Serikali katika Baraza la Wawakilishi.
28
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(8) Makamo wa Kwanza wa Rais na Makamo wa Pili wa
Rais hawatoanza kazi mpaka waapishwe kiapo cha uaminifu na kiapo
chengine mbele ya Rais kama kitakavyoelezwa katika Sheria
iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi.
(9) Makamo wa Kwanza wa Rais na Makamo wa Pili wa
Rais wakati wote watakapokuwa madarakani watawajibika kwa Rais.
39A.(1) Endapo, ndani ya siku saba mara baada ya Rais kushika
madaraka, chama kinachostahiki kutoa Makamo wa Kwanza wa Rais,
kitashindwa kuwasilisha kwa Rais jina la uteuzi wa Makamo wa
Kwanza wa Rais, Rais, bila ya kujali masharti ya kifungu cha 39(1) na
(3) cha Katiba, atawacha wazi nafasi ya Makamo wa Kwanza wa
Rais na kuteua Makamo wa Pili wa Rais.
(2) Kwa mujibu wa masharti ya kijifungu cha (1) cha kifungu
hiki, Rais, bila ya kujali masharti ya kifungu cha 42 (2) cha Katiba,
atateua Mawaziri na kuwacha wazi nafasi za uteuzi wa chama au vyama
vya upinzani.
40.(1) Endapo nafasi ya Makamo wa Kwanza wa Rais au Makamo
wa Pili wa Rais itakuwa wazi:
(a) kwa sababu ya kufariki au kujiuzulu; au
(b) ikiwa Rais amefuta uteuzi huo; au
(c) kwa sababu nyengine yoyote itakayomfanya ashindwe
kuwa na sifa za Makamo wa Kwanza wa Rais au
Makamo wa Pili wa Rais;
Rais atamteua Makamo wa Kwanza wa Rais au Makamo wa Pili wa
Rais kutegemeana na nafasi iliyo wazi.
29
Kuwa wazi
kwa nafasi
ya
Makamo
wa Kwanza
wa Rais au
Makamo
wa Pili wa
Rais.
Kif. 23
Sheria
Nam.9/
2010.
Kuachwa
wazi kwa
nafasi ya
Makamo wa
Kwanza wa
Rais.
Kif. 22 Sheria
Nam.9/2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
(2) Iwapo mtu atafutwa katika nafasi ya Makamo wa Kwanza
wa Rais kwa mujibu wa kijifungu cha (1)(b) cha kifungu hiki, chama
chake si zaidi ya siku kumi na nne kitapendekeza kwa Rais jina la mtu
mwengine.
41.(1) Bila ya kujali masharti ya Katiba hii, Baraza la Wawakilishi
linaweza kupitisha Azimio la kura ya kutokuwa na imani na Makamo
wa Kwanza wa Rais au Makamo wa Pili wa Rais endapo itatolewa
hoja kupendekeza na ikapitishwa kwa mujibu wa masharti ya kifungu
hiki.
(2) Bila ya kuathiri masharti mengineyo ya kifungu hiki, hoja
yoyote ya kutaka kupitisha kura ya kutokuwa na imani na Makamo
wa Kwanza wa Rais au Makamo wa Pili wa Rais haitatolewa katika
Baraza la Wawakilishi endapo:
(a) haijapita miezi sita tangu Makamo wa Kwanza wa
Rais au Makamo wa Pili wa Rais kuteuliwa na Rais;
(b) haijapita miezi tisa tangu hoja ya namna hiyo
ilipotolewa katika Bazara laWawakilishi na Baraza la
Wawakilishi likakataa kuipitisha.
(3) Hoja ya kura ya kutokuwa na imani na Makamo wa
Kwanza wa Rais au Makamo wa Pili wa Rais haitapitishwa na Baraza
la Wawakilishi isipokuwa tu kama:
(a) taarifa ya maandishi, iliyotiwa sahihi na kuungwa
mkono na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi
wasiopungua nusu ya Wajumbe wote wa Baraza la
Wawakilishi itatolewa kwa Spika siku angalau kumi
na nne kabla ya siku inapokusudiwa kuwasilishwa
katika Baraza la Wawakilishi;
30
Hoja ya
kura ya
kutokuwa
na imani.
Kif. 6 cha
Sheria
Nam 13/
1992, Kif.
4 cha
Sheria
Nam 11/
1995 na
Kif. 24
Sheria
Nam. 9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(b) baada ya Spika kuridhika kwamba taarifa hiyo ya
hoja inatimiza masharti yote ya Katiba hii na
imefafanua sababu za kutokuwa na imani, basi
itawasilishwa katika Baraza la Wawakilishi.
(4) Endapo Spika ataridhika na akaamua kuwa hoja
iwasilishwe katika Baraza la Wawakilishi, basi hoja itawasilishwa na
kuamuliwa na Baraza la Wawakilishi zima mapema iwezekanavyo na
kwa mujibu wa Kanuni za Baraza la Wawakilishi.
(5) Azimio la hoja ya kura ya kutokuwa na imani na Makamo
wa Kwanza wa Rais au Makamo wa Pili wa Rais litapitishwa na Baraza
la Wawakilishi endapo hoja inaungwa mkono na Wajumbe wa Baraza
la Wawakilishi wasiopungua theluthi mbili ya Wajumbe wote wa Baraza
la Wawakilishi.
(6) Mapema iwezekanavyo, na kwa vyovyote vile ndani ya
siku mbili tangu Baraza la Wawakilishi lilipopitisha Azimio la hoja ya
kura ya kutokuwa na imani na Makamo wa Kwanza wa Rais au
Makamo wa Pili wa Rais, Spika atawasilisha Azimio hilo kwa Rais,
Makamo wa Kwanza wa Rais au Makamo wa Pili wa Rais atatakiwa
kujiuzulu na Rais atamteua mjumbe mwengine wa Baraza la
Wawakilishi kuwa Makamo wa Pili wa Rais.
(7) Endapo Makamo wa Kwanza wa Rais au Makamo wa
Pili wa Rais ataacha kushika wadhifa wake huo kutokana na Azimio la
hoja ya kura ya kutokuwa na imani:
(i) hatakuwa na haki ya kupata malipo yoyote ya
pencheni wala kupata haki au nafuu nyenginezo, kwa
mujibu wa Katiba au Sheria yoyote iliyotungwa na
Baraza; na
31
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
(ii) atabaki kuwa Mwakilishi lakini hataweza kuteuliwa
tena kuwa Makamo wa Pili wa Rais, Waziri, Naibu
Waziri au Mkuu wa Mkoa kwa kipindi chote cha
uhai wa Baraza hilo.
Sehemu ya Tatu
Mawaziri, Naibu Mawaziri na Baraza la Mapinduzi
42.(1) Kutakuwa na Wizara za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
kama zitakavyoanzishwa na Rais.
(2) Rais ndani ya kipindi cha siku kumi na nne mara baada ya
kuteua Makamo wa Kwanza wa Rais na Makamo wa Pili wa Rais,
kwa kushauriana na Makamo wote wa Wawili wa Rais atateua Mawaziri
kutoka miongoni mwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kwa
kuzingatia uwiano wa viti vya majimbo kwa vyama vya siasa vilivyomo
ndani ya Baraza la Wawakilishi.
42A. Endapo Makamo wa Kwanza wa Rais na, au Mawaziri
kutoka vyama vya upinzani watajiuzulu au wataacha kutekeleza kazi
zao kwa zaidi ya siku saba, Rais bila ya kujali masharti ya vifungu vya
39(3) na 42(2) vya Katiba, ataacha wazi nafasi za uteuzi wao, na
iwapo nafasi hizo zitakuwa wazi kwa zaidi ya siku tisini, Rais anaweza
kuteuwa Mawaziri wengine kujaza nafasi zao.
43.(1) Kutakuwa na Baraza la Mapinduzi ambalo litajumuisha
Rais, Makamo wa Kwanza wa Rais na Makamo wa Pili wa Rais,
Mawaziri pamoja na Wajumbe wengine kama Rais atakavyoona inafaa.
(2) Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi watateuliwa na Rais
kutoka miongoni mwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi.
32
Wizara za
Serikali ya
Mapinduzi
ya Zanzibar.
Kif. 25 cha
Sheria
Nam. 9/
2010.
Baraza la
Mapinduzi.
Kif. 5 cha
Sheria Nam
11/1995
Kif. cha 27
cha Sheria
Nam. 9/
2010.
Kuacha
kufanyakazi
kwa
Makamo
wa Kwanza
na
Mawaziri.
Kif.26 cha
Sheria
Nam. 9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(3) Mwanasheria Mkuu wa Serikali atahudhuria mikutano yote
ya Baraza la Mapinduzi na atakuwa na haki zote za Mjumbe wa Baraza
hilo.
(4) Kazi za Baraza la Mapinduzi zitakuwa:
(a) kumsaidia na kumshauri Rais katika masuala ya
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar;
(b) kuratibu shughuli za Rais, Makamo wa Kwanza wa
Rais na Makamo wa Pili wa Rais na Wizara za
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika utekelezaji
wa majukumu yao.
(5) Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya mamlaka ya
Rais ndiyo itakuwa na uwezo wa kufanya maamuzi juu ya sera za
Serikali kwa ujumla, na Mawaziri chini ya uongozi wa Makamo wa
Pili wa Rais watawajibika kwa pamoja katika Baraza la Wawakilishi
kuhusu utekelezaji wa shughuli za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
(6) Maelezo ya kijifungu cha (4) na (5) hayatatumika kuhusiana
na:
(a) kuteuliwa na kuachishwa kazi kwa Makamo wa
Kwanza wa Rais na Makamo wa Pili wa Rais,
Mawaziri, Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi na
Naibu Mawaziri chini ya vifungu 39, 42 na 47 au
kupewa dhamana kwa Waziri yoyote chini ya kifungu
cha 44;
(b) kuvunjwa kwa Baraza la Wawakilishi;
(c) kuhusiana na mambo yaliyotajwa katika kifungu cha
59 (yanayohusiana na uwezo wa kutoa msamaha).
33
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
44.(1) Majukumu kwa shughuli zote za Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar ikiwa ni pamoja na utawala wa Idara yoyote ya Serikali
yanaweza kuwekwa kwa Makamo wa Kwanza wa Rais na Makamo
wa Pili wa Rais na Mawaziri wengine kama Rais atavyoidhinisha kwa
maandishi.
(2) Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi ambao hawana
Mawizara watakuwa Mawaziri wasio na Wizara Maalum.
45.(1) Rais akiwa ni Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
ataongoza mikutano yote na ikiwa hayupo, Makamo wa Pili wa Rais
atakuwa Mwenyekiti wa muda.
(2) Iwapo Makamo wa Pili wa Rais naye hayupo Zanzibar
basi mikutano itasimamiwa na mtu anayeshikilia madaraka ya Urais.
(3) Kiwango cha kufanyika mkutano wa Baraza la Mapinduzi
itakuwa ni theluthi mbili ya Wajumbe wote.
46. Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi hataanza kufanyakazi zake,
mpaka aapishwe kiapo cha uaminifu na kiapo cha utekelezaji wa kazi
zake mbele ya Rais kama vitavyowekwa na Baraza la Wawakilishi.
47. Rais anaweza kwa kushauriana na Makamo wa Kwanza wa
Rais na Makamo wa Pili wa Rais kuteua Naibu Mawaziri kutoka
miongoni mwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi ili kumsaidia Rais,
Makamo wa Kwanza wa Rais na Makamo wa Pili wa Rais na Mawaziri
katika utekelezaji wa kazi zao na hawatoanza kazi zao mpaka kwanza
waapishwe kiapo cha uaminifu na kiapo cha utekelezaji wa kazi zao
mbele ya Rais kama vitavyowekwa na Baraza la Wawakilishi.
34
Ugawaji wa
Wizara
kwa
Mawaziri.
Kif. 28 cha
Sheria
Nam. 9/
2010.
Mikutano
ya Baraza.
Kif. 29 cha
Sheria
Nam. 9/
2010.
Viapo vya
uaminifu.
Kif.30 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
Naibu
Mawaziri.
Kif.cha 31
cha Sheria
Nam. 9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
48. Nafasi ya Waziri, Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi na Naibu
Waziri itakuwa wazi:
(a) endapo Rais atamwondosha kwenye madaraka hayo
kwa hati yenye muhuri wa Rais; au
(b) iwapo mjumbe ameacha kuwa mjumbe wa Baraza la
Wawakilishi kwa sababu nyengine zaidi ya kuvunjika
kwa Baraza hilo; au
(c) endapo Rais atakubali ombi la kujiuzulu kwa mshika
wadhifa huo; au
(d) mara baada ya Rais kushika madaraka.
49.(1) Kutakuwa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi ambaye
atakuwa pia Katibu Mkuu Kiongozi ataeteuliwa na Rais na ambaye
ndiye atakayekuwa dhamana wa Afisi ya Baraza hilo na dhamana kwa
mujibu wa maelekezo atakayopewa na Rais, kwa kupanga shughuli za
mikutano pamoja na kuweka kumbukumbu ya mikutano hiyo, na
kupeleka maamuzi yanayohusika kwa watu au vyombo vinavyohusika
na atafanya kazi nyengine atakazopewa na Rais mara kwa mara.
(2) Katibu Mkuu Kiongozi atakuwa ndiye Kiongozi wa
Utumishi wa Umma kwa Zanzibar na hatoanza kazi zake mpaka
atakapoapishwa na Rais.
50.(1) Pale Makamo wa Kwanza wa Rais na Makamo wa Pili
wa Rais au Waziri yeyote mwengine anapokuwa na dhamana ya Wizara
yeyote ya Serikali, atakuwa ndiye kiongozi na Msimamizi Mkuu na
bila ya kuathiri masharti yoyote ya usimamizi, Katibu Mkuu ambaye
afisi yake itakuwa ni ya utumishi wa Serikali atakuwa ndiye Afisa
Mtendaji Mkuu wa Wizara.
35
Nafasi ya
Waziri,
Mjumbe wa
Baraza la
Mapinduzi
kuwa wazi.
Kif.cha 32
cha Sheria
Nam. 9/
2010.
Katibu wa
Baraza la
Mapinduzi.
Kif.33 cha
Sheria
Nam. 9/
2010.
Katibu
Mkuu.
Kif.34 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
(2) Kutakuwa na Katibu Mkuu katika Afisi ya Rais, Katibu
Mkuu katika Afisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais, Katibu Mkuu
katika Afisi ya Makamo wa Pili wa Rais na Makatibu Wakuu wengine
wa Wizara mbali mbali kama Rais atakavyoona inafaa.
(3) Makatibu Wakuu waliotajwa kwenye kijifungu cha (2)
cha kifungu hiki watateuliwa na Rais.
(4) Rais anaweza kuteua Naibu Katibu Mkuu wa Wizara.
(5) Katibu Mkuu Kiongozi, Katibu Mkuu na Naibu Katibu
Mkuu yeyote hatoanza kazi yake mpaka kwanza aapishwe kiapo cha
uaminifu na kiapo chengine chochote cha utendaji wa kazi zake mbele
ya Rais kama kitavyowekwa na Baraza la Wawakilishi.
Sehemu ya Nne
Madaraka ya Serikali
51. Madaraka ya Serikali ya Zanzibar yatakuwa mikononi mwa
Rais, na kwa mujibu wa Katiba hii, anaweza kuyatekeleza yeye
mwenyewe moja kwa moja au kuwapa viongozi walio chini yake
kutekeleza madaraka hayo. Ifahamike kwamba masharti yaliyomo
katika kifungu hiki hayazuii sheria kukabidhi madaraka ya kutekeleza
kazi kwa chombo chochote cha umma kwa mtu mwengine yeyote
ambaye si Rais wa Zanzibar.
52. Rais wa Zanzibar halazimiki kufuata ushauri atakaopewa na
mtu yeyote katika utekelezaji wa shughuli zake, isipokuwa kama sheria
inaagiza vyenginevyo.
36
Malengo
ya Serikali
ya
Mapinduzi
ya
Zanzibar.
Kutolazimika
kwa Rais
kufuata
ushauri wa
mtu.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
53. Kwa mujibu wa Katiba hii na bila ya kuathiri masharti ya
Sura ya Nane au Sheria nyengine yoyote iliyopitishwa na Baraza la
Wawakilishi mamlaka:
(a) ya kuanzisha au kufuta afisi katika Zanzibar; na
(b) ya kuteua Wakuu wa afisi hizo na ya kupandisha cheo
kwa muda wa utumishi, kufukuzwa na kushughulikia na
hatua za kinidhamu kwa watu walioteuliwa kushika
dhamana za afisi hizo,
yamo mikononi mwa Rais.
54.(1) Isipokuwa kama imeelezwa vyenginevyo na Katiba hii au
sheria yoyote nyengine kila mtu anayefanya kazi katika afisi ya Serikali
ya Zanzibar atashika dhamana hiyo hadi hapo Rais atakavyoamua
vyenginevyo.
(2) Katika kifungu hiki "Afisi ya Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar" maana yake ni afisi ya Serikali, Idara Maalum au shughuli
nyengine yoyote ilioanzishwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa
mujibu wa Katiba hii na inajumuisha pia afisi katika mashirika yoyote
ya Serikali.
55.(1) Kutakuwa na Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar ambaye ni
Mzanzibari na ambaye atateuliwa na Rais.
(2) Mtu hatafaa kuchaguliwa kuwa Mwanasheria Mkuu au
kufanyakazi za Mwanasheria Mkuu mpaka awe na sifa za kumwezesha
kuwa Mwanasheria katika Zanzibar na ambaye ana sifa hizo kwa muda
usiopungua miaka saba.
37
Uanzishaji
wa Afisi na
Wadhamini
wa Afisi
hizo.
Muda wa
kufanya
kazi katika
Serikali ya
Mapinduzi
ya
Zanzibar.
Kif.35 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
Mwanasheria
Mkuu.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
(3) Mwanasheria Mkuu atakuwa Mjumbe wa Baraza la
Wawakilishi kutokana na wadhifa wake na atashika ujumbe huo mpaka
uteuzi wake utakapofutwa na Rais au mara tu kabla ya Rais mteule
kushika madaraka ya Rais.
56. Mwanasheria Mkuu ndiye atakayekuwa Mshauri Mkuu wa
kisheria kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, na atatekeleza shughuli
nyengine zozote za kisheria zitazopelekwa kwake au atakazoagizwa
na Rais au kwa mujibu wa Katiba hii au Sheria nyenginezo zozote.
56A.(1)(a) Kutakuwa na Mkurugenzi wa Mashtaka ambaye
atateuliwa na Rais.
(b) Mkurugenzi wa Mashtaka atashika wadhifa wake
kwa kipindi cha miaka mitano na ataweza kuteuliwa
tena kwa vipindi vyengine vya miaka mitano mitano.
(2) Mtu hatoweza kuteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Mashtaka
mpaka awe na sifa za kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahkama Kuu.
(3) Mkurugenzi wa Mashtaka atakuwa na uwezo wa kufanya
haya yafuatayo:
(a) kufungua na kushughulikia mashtaka yoyote ya jinai
dhidi ya mtu yeyote mbele ya Mahkama yoyote
(isipokuwa ya Kijeshi) kuhusiana na kosa lolote
ambalo mtu huyo anashtakiwa nalo;
(b) kuchukua na kuendeleza mashtaka yoyote ya jinai
ambayo mwanzoni yalifunguliwa na mtu au chombo
chengine; na
38
Mkurugenzi
wa
Mashtaka.
Kif. 17 cha
Sheria
Nam.2/
2002.
Kazi za
Mwanasheria
Mkuu.
Kif. 16 cha
Sheria
Nam. 2/
2002.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(c) kusitisha mashtaka yoyote ya jinai ambayo
yalianzishwa na mtu yeyote au chombo chochote.
(4) Mamlaka ya Mkurugenzi wa Mashtaka chini ya kijifungu
(3) yanaweza kutekelezwa na Mkurugenzi wa Mashtaka mwenyewe
au na watu wengine kwa maagizo au amri maalum kutoka kwa
Mkurugenzi wa Mashtaka.
(5) Mamlaka ya Mkurugenzi wa Mashtaka chini ya aya (b)
na (c) ya kijifungu (3) yatakuwa mikononi mwake na hayataingiliwa
na mtu yeyote au chombo chochote. Isipokuwa pale ambapo mtu
mwengine au chombo chengine kimefungua mashtaka ya jinai, basi
hakuna chochote katika kijifungu hiki kitakachozuia kufutwa kwa
mashtaka hayo na mtu au chombo kilichoshtaki kwa idhini ya Mahkama.
(6) Kwa madhumuni ya kifungu hiki, rufaa yoyote kutokana
na hukumu katika kesi ya jinai yoyote kwenye Mahkama yoyote, au
suala lolote la kisheria lilioachiwa kwa ajili ya mashtaka hayo kufikishwa
kwenye Mahkama nyengine, itahesabiwa kuwa ni sehemu ya mashtaka
hayo. Kwa kuzingatia kwamba yale mamlaka ya Mkurugenzi wa
Mashtaka chini ya kijifungu (3) (c) hayatatekelezwa kwa ajili ya rufaa
yoyote ya mtu ambaye amehukumiwa katika kosa la jinai lolote
kuhusiana na suala lolote la kisheria lililowekwa makusudi kwa ajili ya
mtu huyo.
(7) Katika kutekeleza madaraka yake kwa mujibu wa
masharti ya kifungu hiki, Mkurugenzi wa Mashtaka hatalazimika kufuata
amri au maagizo ya mtu mwengine yeyote au Idara yoyote ya Serikali,
lakini maelezo haya ya kifungu hiki hayatazuia Mahkama nayo kutumia
madaraka yake kwa ajili ya kuchunguza kama Mkurugenzi wa
Mashtaka ametekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya
Katiba hii au siyo.
39
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
(8) Katika kutumia uwezo wake chini ya kifungu hiki,
Mkurugenzi wa Mashtaka atatilia maanani umuhimu wa maslahi ya
Taifa kwa kutaka kuona haki inatekelezwa na nia yake ya kuzuia
utumiaji mbaya wa vyombo vya kisheria inatimizwa.
(9) Mkurugenzi wa Mashtaka hatoweza kuondolewa ndani
ya kipindi chake cha miaka mitano isipokuwa kwa sababu na utaratibu
uliowekwa kuondolewa Jaji wa Mahkama Kuu kwa mujibu wa kifungu
cha 95 cha Katiba hii.
(10) Baraza la Wawakilishi laweza kutunga Sheria kuhusu
mambo yafuatayo:
(a) Mwenendo wa mashtaka kwa ujumla;
(b) Afisa au mtu mwengine yoyote mwenye sifa
ambaye Mkurugenzi wa Mashtaka anaweza
kukasimu madaraka yake;
(c) utaratibu wa kukata rufaa na muda wa kukata
rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahkama yoyote katika
kesi ya jinai;
(d) utaratibu wa kuanzisha au kufungua shtaka na mtu
binafsi au na taasisi za Serikali na zisizokuwa za
Serikali;
(e) kuwa ni kosa la jinai kwa mtu yeyote kuingilia au
kujaribu kuingilia utekelezaji wa madaraka ya
Mkurugenzi wa Mashtaka kwa mujibu wa Katiba
hii au Sheria yoyote.
40
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
57. Mwanasheria Mkuu, Mkurugenzi wa Mashtaka hatoanza
kazi yake mpaka aapishwe kiapo cha uaminifu na kiapo chengine cha
utekelezaji wa kazi zake na Rais kama kitakavyowekwa na Baraza la
Wawakilishi.
58.(1) Rais anaweza kumteua mtu yeyote kama ni Mshauri wake
Maalum ili kumsaidia katika utendaji wa kazi zake.
(2) Uteuzi wowote chini ya kifungu hiki utafanyika kama
apendavyo Rais na hautaendelea tena iwapo mtu mwengine atashika
madaraka yaUrais.
59. Rais anaweza:
(a) kutoa msamaha bila ya masharti au kwa masharti kwa
mtu yeyote aliyehukumiwa kwa kosa lolote;
(b) kutoa uahirisho ama wa muda au wa moja kwa moja
katika utekelezaji wa adhabu yoyote iliyotolewa na
Mahkama kwa mtu huyo kuhusiana na kosa alilotenda;
(c) kubadili adhabu aliyopewa mtu kutokana na kosa lolote
na kuifanya iwe ndogo zaidi;
(d) kumsamehe kabisa au kwa kiasi fulani mtu yeyote
aliyepewa adhabu kwa kosa lolote au adhabu ya
utaifishaji iliyotolewa na Serikali dhidi yake.
41
Kiapo cha
uaminifu.
Kif. 18 cha
Sheria Nam.
2/2002 na
Kif. 36 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
Washauri
Maalum.
Uwezo wa
kutoa
msamaha.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
60.(1) Kutakuwa na Kamati ya Ushauri kwa Rais katika uwezo
wa kutoa msamaha ambayo itakuwa na Wajumbe wafuatao:
(a) Mwanasheria Mkuu akiwa ndiye Mwenyekiti;
(b) si chini ya wajumbe watatu na si zaidi ya wajumbe
watano watakaoteuliwa na Rais, ambapo kati yao
angalau mmoja atakuwa ni Waziri na angalau mmoja
atakuwa ni mtu mwenye sifa za kuwa Daktari katika
Zanzibar.
(2) Mjumbe wa Kamati aliyeteuliwa kwa mujibu wa kijifungu
(1)(b) ataendelea na dhamana yake kwa kipindi kilichoainishwa kwenye
amri iliyomteua.
Kwa kuzingatia kwamba kiti chake kitakuwa wazi:
(i) ikiwa mtu huyo alipochaguliwa ni Waziri, pale
atakapoachishwa uwaziri;
(ii) ikiwa Rais ataamuru hivyo kwa maandishi.
(3) Bila ya kutegemea kasoro katika jumla ya wajumbe wote,
Kamati hiyo inaweza kufanyakazi na shughuli zake hazitaathirika kwa
kuwepo au kutokuwepo kwa mtu yeyote ambaye hawajibiki kuwepo
au kushiriki katika Kamati hiyo.
(4) Kamati hiyo itapanga utaratibu wake wenyewe.
61.(1) Kutakuwa na Mkuu wa Mkoa katika kila Mkoa wa Zanzibar
ataeteuliwa na Rais.
(2) Kutakuwa na Mkuu wa Wilaya katika kila Wilaya ya
Zanzibar ataeteuliwa na Rais.
42
Kamati ya
Ushauri
katika
uwezo wa
kutoa
msamaha.
Mkuu wa
Mkoa na
Mkuu wa
Wilaya.
Kif.37 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(3) Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilaya aliyeteuliwa kwa
mpangilio chini ya kijifungu (1) na (2) cha kifungu hiki hatoanza kazi
zake hadi kwanza aapishwe kiapo cha uaminifu na kiapo cha utendaji
wake wa kazi zake mbele ya Rais.
62.(1) Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilaya atakuwa ndiye
Mtendaji Mkuu, kwa kadri itavyokuwa wa Mkoa ule au Wilaya ile.
(2) Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilaya anaweza, akipenda
na bila kuathiri masharti yoyote katika Katiba hii au Sheria nyengine
yoyote, kutoa madaraka yake kwa shughuli zozote za Serikali ya Mkoa
huo au ya Wilaya hiyo, kwa kadri itavyokuwa kwa mtu yeyote anayehisi
anafaa, isipokuwa tu madaraka ya kuteuliwa Kaimu Mkuu wa Mkoa
au Wilaya yatakuwa mikononi mwa Rais.
SURA YA TANO
Baraza la Wawakilishi
Sehemu ya Kwanza
Muundo wa Baraza la Kutunga Sheria
63.(1) Kutakuwa na Baraza la Kutunga Sheria ambalo litajuilikana
kama Baraza la Wawakilishi litalokuwa na sehemu mbili, Rais wa
Zanzibar kwa upande mmoja na Wawakilishi kwa upande wa pili.
(2) Iwapo, kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii au masharti
ya sheria nyengine jambo lolote linahitaji kuamuliwa au kutekelezwa
na sehemu zote mbili za Baraza la Kutunga Sheria, basi jambo hilo
halitakuwa na nguvu za kisheria mpaka liwe limeamuliwa au
limetekelezwa na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na vile vile na
Rais.
43
Kazi za
Mkuu wa
Mkoa na
Mkuu wa
Wilaya.
Baraza la
Kutunga
Sheria.
Kif.39 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
64. Kutakuwa na Baraza la Wawakilishi ambalo, bila ya kuathiri
masharti mengine yoyote yaliyomo katika Katiba hii litakuwa na
Wajumbe wafuatao:
(a) Wajumbe wa kuchaguliwa kutokana na kifungu cha 65
cha Katiba hii;
(b) Wajumbe wa kuteuliwa kutokana na kifungu cha 66 cha
Katiba hii;
(c) Wajumbe wanawake wa Baraza la Wawakilishi
kutokana na kifungu cha 67 cha Katiba hii;
(d) Spika iwapo hatakuwa amechaguliwa kutoka miongoni
mwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi;
(e) Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar kutokana na kifungu
55 (3) cha Katiba hii.
65.(1) Zanzibar itagawanywa katika majimbo ya uchaguzi
kutokana na kifungu cha 120 cha Katiba na kila jimbo moja la uchaguzi
litachagua mtu mmoja kuwa Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi kwa
njia ambayo itaelezwa na Katiba au chini ya sheria nyengine yoyote.
(2) Kila mtu ambaye amejiandikisha katika jimbo la uchaguzi
kama ni mpiga kura wa kumchagua Mjumbe, isipokuwa awe
amewekwa kizuizini kwa njia ya halali au hafai kutokana na sheria,
kupiga kura katika uchaguzi huo kwa njia ambayo amekutikana na
kosa lenye kuhusiana na uchaguzi au kwa njia ambayo imeripotiwa
kuwa amepatikana na kosa hilo katika Mahkama au kujaribu kubatilisha
uchaguzi, atastahiki kupiga kura katika jimbo la uchaguzi hilo kwa
mujibu wa sheria iliyowekwa.
44
Kuanzishwa
kwa Baraza
Ia
Wawakilishi.
Kif. 40 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
Uchaguzi
wa
Wajumbe
wa
kuchaguliwa.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(3) Uandikishaji wa kupiga kura wa Wajumbe wa kuchaguliwa
na uendeshaji wa uchaguzi huo utaongozwa na kusimamiwa na Tume
ya Uchaguzi.
66. Kutakuwa na Wajumbe kumi wa kuteuliwa wa Baraza la
Wawakilishi ambao watateuliwa na Rais kutoka miongoni mwa watu
wenye sifa zilizoelezwa na kifungu cha 68(a) na (c) cha Katiba ambao
wakiteuliwa watafaa kuwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi.
Isipokuwa kwamba Wajumbe wasiopungua wawili watateuliwa
na Rais kwa kushauriana na Kiongozi wa Upinzani katika Baraza la
Wawakilishi au kwa kushauriana na Vyama vya Siasa vyenye uwakilishi
ndani ya Baraza la Wawakilishi iwapo hakuna Kiongozi wa Upinzani.
67.(1) Kutakuwa na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi
wanawake kwa idadi ya asilimia arobaini (40%) ya wajumbe wote
wa kuchaguliwa katika majimbo ya uchaguzi ambao ni Wazanzibari
na ambao watapendekezwa na vyama vya siasa vinavyowakilishwa
katika Baraza la Wawakilishi kwa mujibu wa masharti ya kijifungu
cha (2) cha kifungu hiki.
(2) Kila chama cha siasa kitachoshinda zaidi ya asilimia kumi
(10%) ya viti vya majimbo katika Baraza la Wawakilishi kitapendekeza
idadi ya majina ya wanachama wanawake kwa kuzingatia masharti ya
uwiano wa uwakilishi baina ya vyama vya siasa vilivyoshinda uchaguzi
katika majimbo na kupata viti katika Baraza la Wawakilishi na kupeleka
majina na sifa zao kwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar.
(3) Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar baada ya kuridhika kuwa
mwanamke aliyependekezwa ana sifa za kuwa Mjumbe wa Baraza la
Wawakilishi kwa mujibu wa masharti ya kifungu cha 68 cha Katiba
hii, itamtangaza mara moja mwanamke huyo kuwa ni Mjumbe wa
45
Wajumbe
wa
kuteuliwa.
Kif. 41 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
Wajumbe
Wanawake
katika
Baraza.
Kif. 20
cha Sheria
Nam.
2/2002
na Kif.42
cha Sheria
Nam.9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
Baraza la Wawakilishi. Isipokuwa kwamba ieleweke kuwa katika
kufanya hesabu ya idadi ya Wajumbe wa kila chama cha siasa kila
sehemu iliyozidi nusu ya Mjumbe itachukuliwa kuwa ni Mjumbe kamili.
68. Mtu atafaa kuchaguliwa kama Mjumbe wa Baraza la
Wawakilishi ikiwa, na hatofaa kuchaguliwa mpaka, siku ya kuchaguliwa
kwake katika uchaguzi:
(a) awe ni Mzanzibari aliyetimia umri wa miaka ishirini na
moja;
(b) awe amejiandikisha au ana sifa za kujiandikisha katika
jimbo la uchaguzi kama mpiga kura katika uchaguzi wa
Baraza la Wawakilishi;
(c) awe anaweza kusoma na isipokuwa hana uwezo wa
kuona au magonjwa mengine ya kiwiliwili, anasema lugha
ya Kiswahili;
(d) awe ni mwanachama na mgombea aliyependekezwa na
chama cha siasa kilichosajiliwa rasmi kwa mujibu wa
Sheria ya Vyama vya Siasa ya 1992;
(e) awe ni mtu ambaye hakuzuiliwa kugombea uchaguzi kwa
mujibu wa masharti ya kifungu hiki au kwa mujibu wa
sheria iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi la Zanzibar.
69.(1) Hakuna mtu atakayechaguliwa kuwa Mjumbe wa Baraza
la Wawakilishi ikiwa mtu huyo:
(a) ana uraia wa nchi nyengine; au
(b) Mahkama Kuu imeamua, baada ya kushauriwa na
Daktari Bingwa wa magonjwa ya akili, kuwa ana
ugonjwa wa akili; au
46
Sifa za
kuchaguliwa.
Kif. 21 cha
Sheria
Nam. 2/
2002.
Kutofaa
kuchaguliwa.
Kif. 22 cha
Sheria
Nam. 2/
2002.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(c) si mwanachama na mgombea aliyependekezwa na
chama; au
(d) ametiwa hatiani na kupelekwa Chuo cha Mafunzo
au Gereza la Tanzania Bara kwa kosa la jinai kwa
kipindi cha kuanzia miezi 6 na zaidi au kosa la
uchaguzi linalohusu uaminifu ndani ya miaka mitano
kabla ya uchaguzi.
(2) Mtu hawezi kugombea kuwa Mjumbe wa Baraza la
Wawakilishi ikiwa wakati huo yeye ni Mweyekiti wa Baraza la
Mapinduzi.
(3) Kanuni zifuatazo zitatumika kwa ajili ya ufafanuzi wa aya
ya (d) ya kijifungu (1) ya kifungu hiki, yaani:
(a) ikiwa mtu amepata adhabu mbili au zaidi kufungwa
muda wa mfululizo, basi adhabu hizo zitahisabiwa
kuwa ni adhabu mbali mbali iwapo muda uliotajwa
katika moja ya adhabu hizo hauzidi miezi sita, lakini
iwapo muda uliotajwa katika adhabu yoyote kati ya
adhabu hizo unazidi miezi sita basi adhabu hizo zote
zitahesabiwa kama ni adhabu moja;
(b) ikiwa mtu amepewa adhabu ya kufungwa Chuo cha
Mafunzo au Gerezani akifahamika kuwa adhabu hiyo
ya kufungwa imetolewa badala ya adhabu ya kutozwa
faini au imetolewa kwa sababu mtu huyo ameshindwa
kulipa faini aliyoamrishwa kulipa, basi muda wa
kifungo cha namna hiyo hautahesabiwa.
(4) Kwa ajili ya ufafanuzi wa maelezo kuhusu sifa za uchaguzi
yaliyomo katika vifungu vifuatavyo, kila itakapotajwa chini ya Katiba
hii kwamba utekelezaji wa jambo lolote, sifa za uongozi, basi ila za
47
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
uongozi au mtu ambaye hakupoteza sifa za uongozi, basi ila iwapo
maelezo yanahitajia vyenginevyo, ifahamike kuwa sifa zinazohusika ni
zile zinazomwezesha mtu kuchaguliwa kuwa Mjumbe Mwakilishi au
Baraza la Mapinduzi kama viongozi katika Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar kama ilivyoelezwa katika vifungu mbali mbali vya Katiba hii
miongoni mwao ikiwa:
(a) ni mwiko kwa kiongozi kutumia madaraka aliyopewa
kwa ajili ya manufaa yake binafsi, au kwa upendeleo
au kwa namna yoyote ambayo ni kinyume na lengo
lililokusudiwa madaraka hayo;
(b) ni mwiko kwa kiongozi kupokea kipato cha kificho,
au rushwa au kushiriki katika mambo yoyote ya
magendo; na
(c) kiongozi aliyeachishwa uongozi hatakuwa na haki ya
kuomba tena nafasi ya uongozi mpaka ipite miaka
mitano.
70. Kila Mjumbe Mwakilishi atatakiwa kuapishwa, katika Baraza
la Wawakilishi, kiapo cha uaminifu kama kitavyowekwa na Baraza la
Wawakilishi lakini Mjumbe Mwakilishi anaweza kushiriki katika
uchaguzi wa Spika, hata kabla hajaapishwa.
71.(1) Mjumbe Mwakilishi ataacha kuwa Mjumbe Mwakilishi
na ataacha kiti chake katika Baraza la Wawakilishi litokeapo lolote
kati ya mambo yafuatayo:
(a) ikiwa litatokea jambo lolote ambalo, kama
asingekuwa Mjumbe Mwakilishi ingemfanya mtu
asiwe na sifa za kuwa Mjumbe Mwakilishi au apoteze
sifa za Uongozi;
48
Kiapo cha
Mjumbe
Mwakilishi.
Muda wa
Wajumbe
kushika
madaraka
yao.
Kif. 9 cha
Sheria
Nam.13/
1992 na
Kif. 23 cha
Sheria
Nam. 2/
2002.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(b) ikiwa Mjumbe Mwakilishi huyo atachagu1iwa
kuwa Rais wa Zanzibar;
(c) ikiwa Mjumbe Mwakilishi atakosa kuhudhuria
Mikutano ya Baraza mitatu mfululizo bila ya ruhusa
ya Spika;
(d) baada ya Baraza la Wawakilishi kuvunjwa;
(e) iwapo Mahkama Kuu itaamuru Mjumbe apoteze kiti
chake kwa mujibu wa kifungu cha 72 cha Katiba hii;
(f) ikiwa Mjumbe, kwa maandishi yake na ayatume kwa
Spika atajiuzulu kuwa Mjumbe wa Baraza la
Wawakilishi.
(g) Mjumbe akijiondoa uanachama katika chama chake
kilichompendekeza kuwa mgombea.
(2) Spika wa Baraza la Wawakilishi atatoa taarifa rasmi kwa
Baraza na kwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kuhusu
kiti cha Mjumbe Mwakilishi kuwa wazi katika kutekeleza masharti ya
kijifungu cha (1) cha kifungu hiki.
(3) Baraza la Wawakilishi linaweza kutunga sheria kwa ajili ya
kuweka masharti yatayomwezesha Mjumbe Mwakilishi kukata rufaa
kwa mujibu wa Sheria kupinga hukumu ya kuthibitishwa kwake kuwa
ni mtu mwenye ugonjwa wa akili au kupinga adhabu ya kifo au ya
kufungwa Chuo Cha Mafunzo au Gerezani, na Sheria hiyo inaweza
kueleza kwamba hiyo hukumu inayopingwa na huyo Mjumbe
Mwakilishi haitatiliwa nguvu kisheria mpaka umalizike kwanza muda
utakaotajwa katika Sheria hiyo.
49
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
72.(1) Mahkama Kuu ya Zanzibar ndio pekee yenye mamlaka
na uwezo wa kusikiliza na kuamua mashauri yote yanayohusiana na
uchaguzi wa Zanzibar.
(2) Wakati wa kusikiliza shauri lolote chini ya kifungu hiki, Jaji
anaweza kuteua washauri wawili wa Mahkama kwa kumsaidia.
73.(1) Kutakuwa na Spika wa Baraza la Wawakilishi ambaye
atachaguliwa na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kutoka miongoni
mwa watu ambao ni Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi au mwenye
sifa za kuchaguliwa kuwa Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi.
(2) Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi, Makamo wa Kwanza
wa Rais na Makamo wa Pili wa Rais, Waziri, Naibu Waziri au mtu
mwenye madaraka ya aina nyengine yoyote yatayotajwa na sheria
iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi kwa madhumuni ya kifungu hiki,
hataweza kuchaguliwa kuwa Spika.
(3) Spika ataacha kuwa Spika na ataacha kiti cha Spika
litakapotokea lolote kati ya mambo yafuatayo:
(a) iwapo mtu huyo alichaguliwa kutoka miongoni mwa
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi basi ikiwa ataacha
kuwa Mjumbe Mwakilishi kwa sababu yoyote ambayo
haihusiki na kuvunjwa Baraza la Wawakilishi; au
(b) ikiwa kutatokea jambo lolote ambalo, kama
asingekuwa Spika lingemfanya mtu huyo asiwe na sifa
za kuwa Mjumbe Mwakilishi au apoteze sifa za
uchaguzi wa Spika; au
50
Uamuzi wa
suala kama
mtu ni
mjumbe
Mwakilishi
ama sio.
Kif. 10
Sheria
Nam.13/
1992.
Kif. 43 cha
Sheria
Nam.9/2010.
Spika.
Kif.11
Sheria
Nam.13/
1992.
Kif.44 cha
Sheria
Nam.
9/2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(c) ikiwa mtu huyo ataondolewa kwenye madaraka ya
Spika kwa Azimio la Baraza la Wawakilishi lililoungwa
mkono na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi ambao
idadi yao haipungui theluthi mbili ya Wajumbe wa
Baraza la Wawakilishi wote.
(4) Hakuna shughuli itakayotekelezwa katika Baraza la
Wawakilishi (isipokuwa uchaguzi wa Spika) wakati wowote ambao
kiti cha Spika kitakuwa wazi, lakini kijifungu hiki, hakitozuwia Kamati
za Baraza la Wawakilishi kufanya shughuli zao.
(5) Mtu yeyote ambaye si Mjumbe Mwakilishi, atayechaguliwa
kuwa Spika, atatakiwa, kabla ya kuanza kutekeleza madaraka yake
kuapishwa katika Baraza la Wawakilishi kiapo cha uaminifu.
74.(1) Kutakuwa na Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi
ambaye atachaguliwa na Baraza la Wawakilishi kutokana na Kanuni
za Baraza ambaye atakuwa ni Mjumbe Mwakilishi ambaye hatokuwa
Makamo wa Pili wa Rais, Waziri, Naibu Waziri au Mjumbe wa Baraza
la Mapinduzi.
(2) Baraza la Wawakilishi litachagua Naibu Spika:
(a) chini ya masharti ya kifungu cha 73(4) katika mkutano
wake wa mwanzo baada ya kuvunjwa Baraza; na
(b) litakapokutana Baraza kwa mara ya mwanzo wakati
kiti cha Naibu Spika kiwazi kwa njia ambayo sio
sababu ya kuvunjwa kwa Baraza, au kwa haraka
iwezekanavyo.
(3) Kiti cha Naibu Spika kitakuwa wazi:
51
Naibu
Spika.
Kif.45 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
(a) ikiwa Baraza la Wawakilishi ni mara yake ya mwanzo
kukutana toka kuvunjwa kwa Baraza lililopita;
(b) ikiwa amechaguliwa kuwa Rais, Makamo wa Kwanza
wa Rais, Makamo wa Pili wa Rais, Waziri, Naibu
Waziri, Mkuu wa Mkoa au Mjumbe wa Baraza la
Mapinduzi;
(c) ikiwa amesita kuwa Mjumbe wa Baraza la
Wawakilishi kwa njia ambayo sio kwa kuvunjwa
Baraza; au
(d) ikiwa Baraza la Wawakilishi limeamua kwa uamuzi
wa kura zisizopungua theluthi mbili za Wajumbe wote
kuwa Naibu Spika huyo aondolewe katika kiti hicho.
75. Katika Uchaguzi wowote wa Spika au Naibu Spika kura za
Wajumbe wa Baraza zitakuwa za siri.
76.(1) Kutakuwa na Katibu wa Baraza la Wawakilishi
atakayeteuliwa na Rais.
(2) Afisi ya Katibu wa Baraza la Wawakilishi na Afisi za
wafanyakazi wake zitakuwa ni Afisi katika huduma ya Serikali.
(3) Katibu wa Baraza la Wawakilishi hatoanza kazi yake ila
kwanza ale kiapo cha uaminifu na kiapo chengine chochote
kitachowekwa na sheria.
77.(1) Kutakuwa na Afisi ya Baraza la Wawakilishi itayoongozwa
na Katibu wa Baraza la Wawakilishi na itakuwa na nafasi za madaraka
kama itavyoidhinishwa na Tume ya Utumishi wa Baraza la Wawakilishi.
52
Afisi ya
Baraza la
Wawakilishi
Kif. 6 cha
Sheria Nam
11/1995.
Taratibu za
uchaguzi
wa Spika
na Naibu
Spika.
Katibu wa
Baraza la
Wawakilishi.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(2) Kutakuwa na Tume ya Utumishi wa Baraza la Wawakilishi
ambayo itakuwa na uwezo wa kuajiri maafisa na watumishi wote wa
Baraza, kuwapandisha vyeo, kuwachukulia hatua za kinidhamu na
kufanyakazi nyengine zozote zitazoelezwa na Sheria kuhusu Utumishi
katika Afisi ya Baraza, isipokuwa kwamba Katibu wa Baraza la
Wawakilishi atateuliwa na Rais kwa mujibu wa kifungu cha 76 cha
Katiba.
(3) Muundo na taratibu za Tume ya Utumishi wa Baraza
utakuwa kama itavyoelezwa na Sheria itayotungwa kwa madhumuni
hayo.
(4) Baraza la Wawakilishi laweza kutunga Sheria ya kuweka
mfumo wa utawala na uendeshaji na mambo mengine yanayohusu Afisi
ya Baraza la Wawakilishi.
Sehemu ya Pili
Sheria na Taratibu Katika Baraza la Wawakilishi
78.(1) Nguvu za kutunga sheria kwa mambo yote yasiyokuwa ya
Muungano katika Zanzibar yatakuwa mikononi mwa Baraza la
Wawakilishi.
(2) Bila ya kuathiri masharti mengine ya Katiba hii, nguvu za
kutunga sheria katika Baraza la Wawakilishi itakuwa kwa kupitishwa
Miswada katika Baraza la Wawakilishi.
(3) Wakati Mswada umepitishwa na Baraza la Wawakilishi,
Spika ataupeleka kwa Rais ndani ya siku thelathini kupata kibali chake.
(4) Iwapo Mswada ambao umepitishwa na Baraza la
Wawakilishi umepelekwa kwa Rais wa Zanzibar kwa kupata kibali
hicho, utakuwa sheria na hivyo utachapishwa katika Gazeti Rasmi.
53
Nguvu za
kutunga
Sheria.
Kif.46 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
(5) Baraza la Wawakilishi linaweza kuahirisha kuanza kutumika
kwa sheria iliyotungwa na bila kuathiri masharti ya kifungu cha 12 cha
Katiba hii linaweza kufanya sheria kuanza siku za nyuma.
(6) Sheria inayotungwa na Baraza la Wawakilishi itajulikana
kuwa ni "Sheria ya Baraza la Wawakilishi" na jina la utunzi litakuwa
“Imetungwa na Baraza la Wawakilishi la Zanzibar".
79.(1) Baada ya Mswada kuwasilishwa kwa Rais kwa ajili ya
kupata kibali chake, Rais anaweza ndani ya kipindi cha siku tisini ama
kukubali au kukataa kuukubali, na iwapo atakataa kuukubali Mswada,
basi ataurudisha kwenye Baraza la Wawakilishi pamoja na maelezo
ya sababu zake za kukataa kuukubali Mswada huo.
(2) Bila ya kujali masharti ya kifungu cha 62(3) cha Katiba
mara baada ya siku tisini tokea siku ya kuwasilishwa Mswada kwa
Rais kumalizika bila ya kukubaliwa au kukataliwa na Rais, Mswada
huo utachukuliwa kuwa ni Sheria.
(3) Endapo itatokea Mswada kuwa Sheria chini masharti ya
kijifungu cha (2) cha kifungu hiki, Spika ataweka maelezo katika Sheria
hiyo kuonesha kuwa Sheria hiyo imekuwa Sheria kwa mujibu wa
masharti ya kifungu cha 79(2) cha Katiba.
(4) Baada ya Mswada kurudishwa Baraza la Wawakilishi kwa
mujibu wa Masharti ya kifungu hiki, hauwezi kupelekwa tena kwa ajili
ya kupata kibali chake kabla ya kumaliza muda wa miezi sita tangu
uliporudishwa, isipokuwa kama katika hatua yake ya mwisho kwenye
Baraza la Wawakilishi kabla haujapelekwa tena kwa Rais Mswada
huo umeungwa mkono na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi ambao
idadi yao haipungui theluthi mbili ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi
wote.
54
Utaratibu
wa kutunga
Sheria.
Kif.47 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(5) Iwapo Mswada umerudishwa kwenye Baraza la
Wawakilishi na Rais halafu ukaungwa mkono kwenye Baraza la
Wawakilishi na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi ambao idadi yao
haipungui theluthi mbili ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wote
kama ilivyoelezwa katika kijifungu cha (2) na kupelekwa kwa Rais,
kwa ajili ya kupata kibali chake kwa mara ya pili kabla haujamalizika
muda wa miezi sita tangu uliporudishwa, basi atatakiwa kuukubali
Mswada huo kabla ya kumalizika muda wa siku ishirini na moja tangu
Mswada huo ulipowasilishwa kwake la sivyo basi itabidi alivunje Baraza
la Wawakilishi.
(6) Masharti yaliyomo katika kijifungu hiki au katika kifungu
cha 79(1) cha Katiba hii hayatalizuia Baraza la Wawakilishi kutunga
sheria ya kuweka masharti ambayo yanaweza kukabidhi kwa mtu
yeyote kwa Idara yoyote ya Serikali madaraka ya kuweka kanuni
zenye nguvu za kisheria au kuzipa nguvu za kisheria kanuni zozote
zilizowekwa na mtu yeyote au Idara yoyote ya Serikali.
80.(1) Kwa masharti ya kifungu hiki Baraza la Wawakilishi
linaweza kubadilisha kifungu chochote katika Katiba hii.
(2) Mswada wa Baraza la Wawakilishi wa kubadilisha Katiba
hii hautopitishwa na Baraza isipokuwa uwe umeungwa mkono kwa
mara ya kwanza na mara ya pili katika kusomwa kwa kura si chini ya
theluthi mbili ya kura zote za Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi.
(3) Katika kifungu hiki:
(a) marejeo katika Katiba hii ni marejeo katika Katiba
kama itakavyorekebishwa mara kwa mara;
(b) marejeo ya kubadilisha Katiba hii ni marejeo ya
kufanya marekebisho, masahihisho au kutunga ikiwa
55
Kubadilisha
Katiba.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
na mabadiliko au masahihisho katika kifungu chochote
cha Katiba hii, kusimamisha au kufuta kifungu hicho
na utungaji wa kifungu tofauti katika mahala pa
kifungu cha zamani.
80A.(1) Bila ya kuathiri masharti ya kifungu cha 80 cha Katiba,
Baraza la Wawakilishi halitaweza kufanya mabadiliko ya Katiba
kuhusiana na sharti lolote liliomo katika kifungu chochote kilichoainishwa
katika kijifungu cha (2) cha kifungu hiki, mpaka kwanza mabadiliko
hayo yakubaliwe na wananchi kwa Kura ya Maoni.
(2) Kwa kuzingatia masharti ya kijifungu cha (1) cha kifungu
hiki, vifungu vinavyohitaji Kura ya Maoni ni:
(a) vifungu vyote vya Sehemu ya Kwanza ya Sura ya
Kwanza;
(b) kifungu cha 9;
(c) vifungu vyote vya Sura ya Tatu;
(d) kifungu cha 26;
(e) kifungu cha 28;
(f) vifungu vyote vya Sehemu ya Pili na Sehemu ya
Tatu ya Sura ya Nne isipokuwa kifungu cha 49 na
50;
(g) kifungu cha 80A; na
(h) vifungu vya 121(1) na 123 vya Sura ya Kumi.
56
Kura ya
maoni kwa
mabadiliko
ya baadhi
ya vifungu
vya Katiba.
Kif.48 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(3) Bila ya kuathiri masharti ya vijifungu vya (1) na (2) vya
kifungu hiki, kifungu chochote kilichotajwa chini ya kijifungu cha (2)
kinaweza kurekebishwa bila kuitisha Kura ya Maoni pale Baraza la
Wawakilishi kwa Azimio Maalum lililopitishwa kwa kuungwa mkono
na theluthi mbili ya Wajumbe waliohudhuria na kupiga kura,
litaporidhika kwamba marekebisho yanayotaka kufanywa ni ya
kiutaratibu, ya kiuandishi ama ya kuweka bayana jambo lenye utatanishi
na hayaathiri madhumuni ya msingi ya kifungu husika.
(4) Bila ya kuathiri masharti yaliyoelezwa katika kijifungu cha
(2) cha kifungu hiki, Kura ya Maoni inaweza kuitishwa kwa mujibu
wa masharti ya Sheria iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi.
81. Ki1a Kikao cha Baraza la Wawakilishi kitaongozwa na:
(a) Spika; au
(b) ikiwa hayupo Naibu Spika; au
(c) ikiwa Spika hayupo na Naibu Spika hayupo, Mjumbe
mwengine wa Baraza la Wawakilishi (asiyekuwa
Makamo wa Pili wa Rais, Waziri, Naibu Waziri,
Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi au Mkuu wa Mkoa)
kama Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi
watakayemchagua kwa ajili hiyo.
82.(1) Baraza la Wawakilishi linaweza kuendesha shughuli bila
ya kujali kuweko kwa kiti wazi kuhusu Mjumbe kuhusiana na kiti
ambacho hakikujazwa wakati Baraza ndio kwanza liitishwe au kuundwa
kwa mara ya kwanza na shughuli hizo zitaendelea bila ya kujali kuweko
kwa mtu asiyehusika kuwepo au kupiga kura katika Baraza au kuwepo
katika shughuli zinazoendelea.
57
Viti vilivyo
wazi katika
Baraza la
Wawakilishi
na
utaratibu
wa
kuendesha
shughuli za
Baraza.
Uongozi wa
kikao cha
Baraza la
Wawakilishi.
Kif.49 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
(2) Bila ya kuathiri masharti yaliyomo katika kifungu cha 80
cha Katiba hii, idadi ya Wajumbe kufanya mkutano itakuwa nusu ya
Wajumbe wote wa Baraza la Wawakilishi.
83.(1) Isipokuwa kama imeelezwa vyengine katika Katiba hii,
suala lolote au uamuzi katika Baraza la Wawakilishi litaamuliwa
kutokana na idadi kubwa ya Wajumbe waliohudhuria kwenye kikao
na kupiga kura.
(2) Jambo lolote litakalopelekwa kwa uamuzi katika Baraza
la Wawakilishi, mtu atakayekuwa anaongoza kikao cha Baraza la
Wawakilishi:
(a) ikiwa ni Spika, atakuwa na kura ya uamuzi na siyo
kura ya asili;
(b) ikiwa siye Spika atakuwa na kura ya uamuzi pamoja
na kura ya asili;
(3) Kanuni za Baraza la Wawakilishi zinaweza kuweka vifungu
ambavyo Mjumbe ambaye anapiga kura na huku akiwa na maslahi
fulani ya jambo linalopigiwa kura asiwe na kura.
84. Rais atahusika katika mamlaka ya shughuli zake kama Rais
wa Zanzibar kuhutubia Baraza la Wawakilishi wakati atakaoona unafaa
kufanya hivyo.
58
Madaraka
ya Rais
katika
Baraza la
Wawakilishi.
Kif.50 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
Upigaji
kura
katika
Baraza la
Wawakilishi.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
85.(1) Kutakuwa na Kamati za Kudumu za Baraza la Wawakilishi
zitazoundwa kwa mujibu wa Kanuni za Baraza la Wawakilishi.
(2) Kwa madhumuni ya kifungu hiki cha Katiba hii, kazi na
shughuli za Kamati za Baraza la Wawakilishi zitakuwa kama
zitakavyoainishwa katika Kanuni za Baraza la Wawakilishi.
(3) Baraza linaweza Iikaanzisha Kamati nyengine zozote
inazohisi zinafaa.
86.(1) Baraza la Wawakilishi linaweza, kwa ajili ya ufanisi mzuri
wa kazi zake, kutunga sheria kuhusiana na haki za Wajumbe, nguvu
zao, fursa na kinga zao pamoja na Kamati zao kwa misingi
inayokubalika.
(2) Bila ya kuathiri masharti mengine ya Katiba hii, Baraza la
Wawakilishi linaweza kufanya Kanuni za kudumu za Baraza hilo zikitilia
maanani amri za kuendesha mikutano, na kwa kutilia maanani sheria
zitazotungwa kwa mujibu wa kijifungu (1) cha kifungu hiki kutoka
katika kanuni hizo haki za Wajumbe, nguvu zao, fursa na kinga za
Wajumbe wa Kamati zao.
(3) Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi katika kutekeleza
majukumu yao Barazani, katika Kamati za Kudumu za Baraza au
katika Kamati Teule za Baraza:
(i) watakuwa na kinga kwa mashtaka yoyote ya jinai au
madai;
(ii) watakuwa na kinga ya maelezo wanayoyazungumza;
na
(iii) hawatokamatwa wakati wakiwa katika shughuli hizo.
59
Kamati za
Baraza la
Wawakilishi.
Kif. 7 cha
Sheria Nam
11/1995.
Baraza la
kutunga
Sheria.
Kif.51 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
87.(1) Bila ya kuathiri kifungu hiki, lugha rasmi ya Baraza la
Wawakilishi itakuwa ni Kiswahili.
(2) Kila Mswada (pamoja na vijalizo vilivyofuatana na Mswada),
kila sheria inayotungwa na Baraza, kila Sheria ya msingi au sheria
inayopendekezwa chini ya chombo cha sheria na Baraza, maafikiano
yote ya kifedha na nyaraka zenye kuhusiana na kila sheria halisi au
inayopendekezwa, kusahihishwa au inayoendelea itaandikwa kwa lugha
ya Kiswahili na ikihitajika kwa lugha ya Kiingereza.
88. Baraza la Wawakilishi pamoja na kuongoza shughuli zake
kutokana na vifungu vya Katiba hii, litafanya kazi kwa mambo yafuatayo
ya utekelezaji:
(a) kutunga sheria pale ambapo utekelezaji wa jambo
unahitaji kuwepo kwa sheria hiyo;
(b) kujadili shugliuli za kila Wizara wakati wa kikao cha
mwaka wa Bajeti katika Baraza la Wawakilishi;
(c) kuuliza masuala mbali mbali kwa Serikali ya Mapiduzi
ya Zanzibar katika Baraza la Wawakilishi;
(d) kuidhinisha na kusimamia mipango ya maendeleo ya
Serikali katika njia ile ile ambayo Bajeti ya mwaka
inaidhinishwa.
Sehemu ya Tatu
Kuitisha na Kuvunja Baraza la Wawakilishi
89.(1) Bila ya kuathiri masharti ya kifungu hiki, mkutano wa Baraza
utakuwa sehemu yoyote katika Zanzibar na utafanyika wakati wowote
ambapo Rais ataamuru.
60
Lugha
rasmi.
Kazi za
Baraza la
Wawakilishi.
Kuitisha
mkutano wa
Baraza la
Wawakilishi.
Kif. 24 cha
Sheria
Nam.2/
2002.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(2) Kutakuwa na mkutano wa Baraza la Wawakilishi angalau
mara moja kila mwaka na kipindi cha miezi kumi na mbili hakitopita
baina ya mkutano mmoja na mwengine.
90.(1) Wakati Baraza litakapovunjwa, Uchaguzi Mkuu wa
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi utafanywa na mkutano wa
mwanzo wa Baraza jipya utafanywa si zaidi ya siku tisini toka kuvunjwa
kwa Baraza.
(2) Bila kuathiri masharti ya kifungu hiki, kikao cha Baraza la
Wawakilishi katika mkutano wowote wa Baraza utafanyika wakati
wowote na siku yoyote kama itakavyoelezwa kulingana na Kanuni za
Baraza.
(3) Kukitokea hali ya hatari au kama kuna hali ya hatari ambayo
Rais anaona inasababisha kuitisha Mkutano wa Baraza la Wawakilishi
na iwapo wakati huo Baraza la Wawakilishi limevunjwa na matokeo
ya kura zilizo nyingi za Uchaguzi Mkuu hayajatangazwa basi Rais aweza
kutoa Taarifa Maalum ya kuitisha Mkutano wa Baraza la Wawakilishi
na kuagiza kwamba Spika na watu wote waliokuwa Wajumbe wa
Baraza la Wawakilishi mara tu kabla ya Baraza la Wawakilishi
halijavunjwa wahudhurie Mkutano huo na watahesabiwa hivyo mpaka
usiku wa manane wa siku yatakapotangazwa matokeo ya kura zilizo
nyingi za Uchaguzi Mkuu.
91.(1) Rais wakati wowote anaweza kuitisha Baraza la
Wawakilishi kuendelea na shughuli zake.
(2) Rais hatakuwa na uwezo wakati wowote wa kulivunja
Baraza la Wawakilishi isipokuwa tu:
61
Kuitisha na
kuvunja
Baraza la
Wawakilishi.
Kif. 8 cha
Sheria Nam
11/1995 na
Kif.52 cha
Sheria
Nam.9/2010.
Uchaguzi
Mkuu na
Mkutano
wa
mwanzo.
Kif. 25 cha
Sheria
Nam.2/
2002.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
(a) kama Baraza la Wawakilishi limemaliza uhai wake
kwa mujibu wa kifungu cha 92 cha Katiba; au
(b) anaweza kulivunja wakati wowote ndani ya miezi
kumi na mbili ya mwisho ya uhai wa Baraza la
Wawakilishi kwa madhumu ya kuitisha Uchaguzi
mapema kidogo; au
(c) kama Baraza la Wawakilishi limekataa kupitisha
Bajeti inayopendekezwa na Serikali; au
(d) kama Baraza la Wawakilishi limekataa kupitisha
Mswada wa Sheria kwa mujibu wa kifungu cha 79
cha Katiba; au
(e) kama Baraza la Wawakilishi limekataa kupitisha hoja
ambayo ni ya msingi katika sera za Serikali na Rais
anaona kwamba njia muafaka ya kulinda maslahi
ya Taifa si kuvunja Baraza la Mawaziri au kuteua
Makamo wa Pili wa Rais mpya bali ni kuitisha
Uchaguzi Mkuu; au
(f) endapo, kutokana na uwiano wa uwakilishi wa
Vyama vya Siasa katika Baraza la Wawakilishi, Rais
anahisi kwamba hakuna uhalali kwa Serikali iliyopo
kuendelea kuwapo na wala haiwezekani kuunda
Serikali mpya.
Isipokuwa kwamba hataweza kulivunja Baraza chini ya
masharti ya vijifungu (b), (c), (e) na (f), kama Spika amepokea taarifa
rasmi inayopendekeza kuundwa kwa Kamati Maalum ya Uchunguzi
kwa madhumuni ya kumuondoa Rais madarakani kwa mujibu wa
kifungu cha 37 cha Katiba.
62
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(3) Bila ya kuathiri masharti yoyote ya Katiba, Spika anaweza
wakati wowote kuliitisha Baraza la Wawakilishi kwa jambo la dharura
baada ya kupata ombi la Mjumbe wa Baraza na Spika akaridhika
kwamba sababu zilizoelezwa katika ombi hilo ni za msingi na inafaa
Baraza la Wawakilishi kuitishwa.
92.(1) Maisha ya Baraza la Wawakilishi yataendelea kwa muda
wa miaka mitano tangu tarehe ile ulipoitishwa Mkutano wake wa kwanza
baada ya kuundwa, ila tu pale iwapo Baraza la Wawakilishi limevunjwa
mapema kutokana na sababu mbali mbali zilizoelezwa katika Katiba
hii.
(2) Wakati wote Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
itakapokuwa iko kwenye vita, Baraza la Wawakilishi laweza mara kwa
mara kuongeza kipindi cha miaka mitano iliyoelezwa katika kijifungu
cha (1) cha kifungu hiki na si zaidi ya miezi sita kwa wakati mmoja.
SURA YA SITA
Sheria
Sehemu ya Kwanza
Mahkama Kuu
93.(1) Kutakuwa na Mahkama Kuu ya Zanzibar ambayo itakuwa
ndio Mahkama ya kumbukumbu na kuwa na mamlaka yote ya kesi za
jinai na madai na nguvu nyengine zitazopewa kwa mujibu wa Katiba hii
au Sheria nyengine yoyote.
(2) Majaji wa Mahkama Kuu watakuwa Jaji Mkuu na Majaji
wengine, wasiopungua wawili wataojulikana kama Majaji wa Mahkama
Kuu.
63
Kuundwa
kwa
Mahkama
Kuu.
Maisha ya
Baraza la
Wawakilishi
Kif. 26 cha
Sheria
Nam. 2/
2002 na
Kif.53 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
(3) Mahkama Kuu itakuwa imekamilika kisheria licha ya kuwa
na nafasi wazi ya kiti cha Jaji wa Mahkama hiyo.
(4) Kazi ya Jaji haitafutwa wakati yupo mtu aliyehusika na
madaraka ya kiti cha Jaji.
(5) Mahkama Kuu itakaa pahala popote ambapo Jaji Mkuu
atakapoteua kwa ajili hiyo.
94.(1) Jaji Mkuu atateuliwa na Rais kutoka miongoni mwa Majaji
wa Mahkama Kuu na baada ya kushauriana na Tume ya Utumishi ya
Mahkama.
(2) Majaji wa Mahkama Kuu watateuliwa na Rais kutokana
na mapendekezo ya Tume ya Utumishi ya Mahkama.
(3) Mtu hatoweza kuteuliwa kuwa Jaji au Kaimu Jaji wa
Mahkama Kuu mpaka:
(a) awe na shahada ya Sheria ya Chuo Kikuu
kinachotambuliwa au Chuo cha aina hiyo; na
(b) (i) awe au amewahi kuwa Jaji wa Mahkama
zilizofanana na hii kwa kesi zote za jinai na madai
katika Tanzania au sehemu yoyote ya Jumuiya ya
Madola au Mahkama yenye mamlaka ya Rufaa
kutoka Mahkama hizo; au
(ii) awe ni Mwanasheria wa Zanzibar au Tanzania kwa
kipindi kisichopungua miaka saba; au
(iii) awe na uzoefu wa (i) na (ii) kwa pamoja usiopungua
miaka saba.
64
Uteuzi wa
Majaji wa
Mahkama
Kuu.
Kif. 27 cha
Sheria
Nam.
2/2002.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(4) Ikitokea kwamba kiti cha Jaji kitakuwa wazi au kwamba
Jaji Mkuu atashindwa kutekeleza kazi zake kwa sababu yoyote, basi
kazi hizo zitatekelezwa na Jaji mmoja wapo atakayeteuliwa na Rais
wa Zanzibar kwa ajili hiyo kama Kaimu Jaji Mkuu na Jaji huyo
atatekeleza kazi hizo mpaka atakapoteuliwa Jaji Mkuu mwengine na
kushika madaraka ya kiti cha Jaji Mkuu au mpaka Jaji Mkuu
mwenyewe ambaye alikuwa hamudu kazi zake atakaporejea kazini.
(5) Ikiwa Jaji wa Mahkama Kuu ameteuliwa kuwa Kaimu Jaji
Mkuu au kwa sababu nyengine yoyote ile hawezi kufanya kazi zake za
Ujaji au ikiwa Jaji Mkuu atamshauri Rais kwamba kwa hali ilivyo
Mahkama Kuu inahitajia Jaji mwengine, Rais akishauriana na Tume ya
Utumishi ya Mahkama, anaweza kumteua mtu yeyote kuwa Jaji wa
Mahkama Kuu bila ya kujali umri ulioelezewa katika kifungu 95(1)
cha Katiba hii.
(6)(a) Rais anaweza kumteua mtu yeyote kuwa Kaimu Jaji
wa Mahkama Kuu kwa kipindi kisichozidi miezi kumi
na mbili au Jaji kwa mkataba wa kipindi maalum
kutokana na mapendekezo ya Tume ya Utumishi ya
Mahkama.
(b) Masharti ya Kazi, marupurupu na kiinua mgongo cha
Jaji kwa mkataba wa kipindi maalum yataamuliwa na
Tume ya Utumishi ya Mahkama.
(7) Mtu yeyote aliyeteuliwa chini ya kijifungu cha (5) kushikilia
nafasi ya Jaji wa Mahkama Kuu, ataendelea bila kuathiri matakwa ya
vijifungu (4) na (6) vya kifungu 95, kushika wadhifa huo hadi hapo
uteuzi wake utapofutwa na Rais kutokana na ushauri wa Turne ya
Utumishi ya Mahkama na ataendelea kushikilia wadhifa huo kwa muda
65
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
utaokuwa muafaka kwa kutoa hukumu au kufanya kitu chengine
chochote kutokana na mambo ambayo yamefanyika mbele yake.
(8) Jaji Mkuu hatoweza kuondolewa kwenye kiti cha Jaji
Mkuu isipokuwa kwa sababu na utaratibu uliowekwa kuondolewa
Jaji wa Mahkama Kuu kwa mujibu wa kifungu cha 95 cha Katiba hii.
95.(1) Bila ya kuathiri masharti ya kifungu hiki, Jaji wa Mahkama
Kuu ataendelea kushika wadhifa wake hadi kufikia umri wa miaka
sitini ambapo anaweza kustaafu kwa hiari ama kuendelea hadi kufikia
umri wa miaka sitini na tano ambapo atastaafu kwa lazima.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya kijifungu cha (1) cha kifungu
hiki, Rais kwa kushauriana na Tume ya Utumishi ya Mahkama anaweza
kumteua tena Jaji aliyekwisha staafu kushika madaraka ya Jaji wa
Mahkama Kuu kwa muda au kwa ajili ya kesi maalum.
(3) Licha ya kuwa Jaji amefika umri ulioainishwa katika kijifungu
cha (1) hapo juu, Jaji wa Mahkama Kuu ataendelea katika wadhifa
wake huo hata baada ya kufikia umri huo mpaka pale atapomaliza
shughuli zote ambazo zilimfika yeye kabla ya kutimiza umri huo.
(4) Jaji wa Mahkama Kuu ya Zanzibar aweza tu kuondolewa
katika madaraka ya kazi ya Jaji kwa sababu ya kushindwa kutekeleza
kazi zake (ama kutokana na sababu nyengine yoyote) au kwa sababu
ya tabia mbaya, na hataweza kuondolewa kazini ila kwa mujibu wa
masharti ya kifungu hiki.
(5) Jaji wa Mahkama Kuu ataondolewa kazini na Rais ikiwa
suala la kuondolewa kwake limepelekwa kwa Tume iliyoundwa kwa
madhumuni hayo chini ya kijifungu cha (6) cha kifungu hiki; na Tume
hiyo imependekeza kwa Rais kwamba Jaji huyo anafaa kuondolewa
kutokana na kutomudu kazi zake au kutokana na tabia zake mbaya.
66
Muda wa
kushika
madaraka
ya Ujaji.
Kif. 28 cha
Sheria
Nam. 2/
2002.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(6) Iwapo Rais anaona kwamba suala la kumuondoa Jaji Mkuu
kazini linahitaji kuchunguzwa, au iwapo Jaji Mkuu atapeleka kwa Rais
kwamba suala la kumuondoa Jaji linahitaji kuchunguzwa:
(a) Rais atateua Mwenyekiti na Wajumbe wawili ambao
ni Majaji au watu waliopata kuwa Majaji wa
Mahkama Kuu ya Zanzibar au ya Jamhuri ya
Muungano au Mahkama ya Rufaa ya kesi za
Mahkama hizo.
(b) Tume hiyo itachunguza shauri lote halafu itatoa taarifa
kwa Rais wa Zanzibar kuhusu maelezo ya shauri lote
na itamshauri Rais wa Zanzibar kama huyo Jaji
anayehusika aondolewe kazini kwa mujibu wa
masharti ya kifungu hiki kwa sababu ya kushindwa
kufanya kazi kutokana na maradhi au sababu
nyengine yoyote au kwa sababu ya tabia mbaya.
(7) Ikiwa suala la kumuondoa Jaji kazini limepelekwa kwenye
Tume kwa ajili ya uchunguzi kwa mujibu wa masharti ya kifungu hiki,
Rais akishauriana na Tume ya Utumishi ya Mahkama kwa suala la Jaji
wa Mahkama Kuu, au kwa pendekezo lake mwenyewe kwa suala la
Jaji Mkuu, anaweza kumsimamisha kazi Jaji huyo anayehusika na
kusimamishwa kazi huko kunaweza wakati wowote kutenguliwa kwa
mpango ule ule ulioelezwa wakati wa kusimamishwa kazi na kwa
vyovyote vile uamuzi huo wa kusimamishwa kazi utakuwa hauna nguvu
yoyote pale Tume itapopendekeza kwamba Jaji huyo asingestahili
kuondolewa kazini.
(8) Jaji Mkuu au Jaji wa Mahkama Kuu hatateuliwa au
kuchaguliwa kufanya kazi nyengine katika Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar au sehemu nyengine yoyote kwa kipindi chochote kile bila ya
ridhaa yake kwa maandishi.
67
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
96. Jaji Mkuu, Kaimu Jaji Mkuu na Jaji wa Mahkama Kuu
hatoanza kazi zake mpaka kwanza aapishwe kiapo cha uaminifu na
kiapo chengine chochote mbele ya Rais kitachowekwa na Sheria kwa
ajili hiyo.
97. Itakuwa ni marufuku kwa Jaji wa Mahkama Kuu (pamoja na
Jaji Mkuu), Mahakimu wa ngazi zote, Mrajis, Kaimu Mrajis, Naibu
Mrajis na Msaidizi Mrajis na Makadhi wote (pamoja na Kadhi Mkuu)
kujiunga na Chama chochote cha Siasa isipokuwa tu kwamba atakuwa
na haki ya kupiga kura iliyotajwa katika kifungu cha 7 cha Katiba hii.
Sehemu ya Pili
Mahkama ya Rufaa
98. [Kimefutwa].
99. Mahkama ya Rufaa ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
itakuwa na uwezo wa kusikiliza rufaa kutoka Mahkama Kuu ya
Zanzibar isipokuwa kesi zozote zinazohusika na:
(a) tafsiri ya Katiba hii;
(b) mambo ya Kiislamu ambayo yameanzia katika
Mahkama za Kadhi;
(c) mambo mengine yoyote yaliyoainishwa katika Katiba
hii na Sheria nyengine yoyote iliyotungwa na Baraza la
Wawakilishi.
68
Uanachama
katika
vyama vya
siasa
Kif. 9 cha
Sheria
Nam 11/
1995.
Viapo kwa
Majaji wa
Mahkama
Kuu.
Kif. 54 cha
Sheria
Nam. 9/
2010.
Kazi na
uwezo wa
Mahkama
ya Rufaa.
Kif. 30 cha
Sheria
Nam. 2/
2002.
Kif. 29 cha
Sheria Nam.
2/2002.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
99A.(1) Iwapo katika shauri lolote katika Mahkama yoyote iliyo
chini ya Mahkama Kuu suala la tafsiri ya Katiba hii litajitokeza, suala
hilo mara moja litawasilishwa Mahkama Kuu kwa uamuzi na shauri
hilo halitaendelea mpaka uamuzi wa Mahkama Kuu uwe umepatikana.
(2) Rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahkama Kuu juu ya suala la
tafsiri ya Katiba hii itasikilizwa na Mahkama Kuu mbele ya Majaji
watatu bila ya kumjumuisha Jaji aliyeamua suala hilo mara ya kwanza.
Majaji hao watatu watateuliwa na Jaji Mkuu.
Sehemu ya Tatu
Mahkama Nyenginezo
100. Baraza la Wawakilishi linaweza kuanzisha Mahkama
nyengine zilizo chini ya Mahkama Kuu na bila kuathiri masharti ya
Katiba hii, Mahkama hizo zilizoainishwa zitakuwa na uwezo na
madaraka ya aina ambayo yataainishwa katika Sheria.
Sehemu ya Nne
Utaratibu wa kupeleka Hati na kutekeleza maagizo
yaliyomo katika Hati zilizotolewa na Mahkama
101.(1) Hati zenye maagizo yaliyotolewa na Mahkama za Tanzania
Bara na Mahkama za Zanzibar katika mashauri ya madai ya aina zote
na mashauri ya jinai ya aina zote (pamoja na hati za kuamuru kukamatwa
watu) zaweza kupelekwa mahali popote nchini Tanzania na maagizo
hayo yaweza kutekelezwa mahali popote nchini Tanzania kwa kufuata
masharti yafuatayo:
(a) iwapo Mahkama imetoa hati yenye maagizo
yatakayotekelezwa mahali ambapo Mahkama hiyo
69
Kuanzishwa
kwa
Mahkama
nyengine.
Kif. 32 cha
Sheria
Nam. 2/
2002.
Ufafanuzi
wa Katiba
kupelekwa
Mahkama
Kuu.
Kif..31 cha
Sheria Nam.
2/2002.
na kif. 55
cha Sheria
Nam.9/
2010.
Utekelezaji
wa
maagizo
ya
Mahkama
utafanywa
nchini
Tanzania
kote.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
haina mamlaka; basi hati hiyo itapelekwa huko na
maagizo yaliyomo katika hati hiyo yatatekelezwa
kwa mujibu wa utaratibu unaotumika huko kwa ajili
ya kupeleka hati au kutekeleza maagizo yaliyomo
katika hati iliyotolewa na Mahkama yenye mamlaka
huko ilikopelekwa hati; na
(b) iwapo sheria inayotumika huko ilikopelekwa hati
imeweka masharti kwamba hati zilizotolewa na
Mahkama ya mahali pengine ni lazima ithibitishwe
kwanza na Mahkama yenye mamlaka mahali hapo
inapotumika sheria hiyo basi kila hati iliyotolewa na
Mahkama ya mahali pengine itabidi ithibitishwe
kwanza kwa mujibu wa sheria hiyo kabla maagizo
yaliyomo katika hati hiyo hayajatekelezwa.
(2) Iwapo mtu amekamatwa mahali popote nchini Tanzania
kwa mujibu wa hati ya kuamuru kukamatwa kwake iliyotolewa na
Mahkama ambayo haina mamlaka mahali hapo alipokamatwa mtu huyo,
basi mtu atahesabiwa kuwa yuko chini ya ulinzi halali na anaweza
kufikishwa mbele ya Mahkama iliyotoa hati hiyo, lakini masharti haya
yaliyomo katika kifungu hiki itabidi yatumiwe bila kuathiri masharti ya
Sheria inayotumika hapo mahali alipokamatwa mtu huyo.
(3) Masharti yaliyomo katika kifungu hiki hayatazuia Sheria
kuweka utaratibu kwa ajili ya kupeleka nje ya Tanzania hati zilizotolewa
na Mahkama za Tanzania Bara au Mahkama za Zanzibar.
70
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
Sehemu ya Tano
Tume ya Utumishi ya Mahkama
102. Kutakuwa na Tume ya Utumishi ya Mahkama ambayo
muundo, kazi na uwezo wake utakuwa kama ilivyoelezwa na Sheria
iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi.
102A. [Kimefutwa].
103. [Kimefutwa].
SURA YA SABA
Sehemu ya Kwanza
Fedha
Masharti ya Fedha Yahusuyo Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar
104.(1) Kutakuwa na Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar ambao bila ya kuathiri sheria nyengine yoyote
inayotumika, zitawekwa fedha zote zitakazopatikana kutokana na njia
mbali mbali kwa ajili ya matumizi ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
kwa:
(a) kulipwa katika mfuko wa Serikali (mbali na ule
mfuko wa Hazina) na ambao utawekwa kwa
shughuli maalum; au
(b) kwa kuwekwa na Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar katika Mabenki mbali mbali ndani na nje
ya nchi kwa madhumuni ya kulipa matumizi yoyote
ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar;
71
Tume ya
Utumishi
ya
Mahkama.
Kif. 56 cha
Sheria
Nam. 9/
2010.
Mfuko
Mkuu wa
Hazina na
fedha
nyengine
za Serikali
ya
Mapinduzi
ya
Zanzibar
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
Ila ijulikane tu kwamba fedha hizo hazitotolewa kutoka mfuko
huo mpaka iwe utolewaji wa fedha hizo umekubaliwa na Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar au kwa sheria iliyopitishwa na Baraza la
Wawakilishi kwa madhumuni hayo.
105.(1) Waziri anayehusika na Fedha atatayarisha makadirio ya
matumizi kwa ajili ya Serikali kwa mwaka unaofuatia na atayapeleka
Baraza la Wawakilishi.
(2) Makadirio ya matumizi yataonesha matumizi mbali mbali
yanayohitajika kisheria (kama yalivyotafsiriwa katika kijifungu cha (3)
cha kifungu 106) na matumizi mengine ya kawaida ambayo yanahitajika
kutolewa katika Mfuko wa Hazina.
106.(1) Waziri anayehusika na mambo ya fedha atapeleka Baraza
la Wawakilishi mapema iwezekanavyo, kila mwaka wa fedha
unapoanza Mswada kwa ajili ya kuidhinisha matumizi ya Serikali ukiwa
na kasma zinazohusika kwa shughuli mbali mbali zinazohitajika pamoja
na jumla ya fedha zote zinazoombewa kwa matumizi hayo mbali na
matumizi yanayohitajika kisheria kwa mwaka huo wa fedha.
(2) Inapotokea:
(a) kwamba fedha zilizotumika au zinazotaka kutumika
katika mwaka wowote wa fedha kwa madhumuni
fulani ni zaidi ya fedha zilizoruhusiwa na Sheria ya
Matumizi ya mwaka ule; na
(b) kwamba fedha zilizotumika au zinazotaka kutumika
(mbali ya matumizi yanayohitajika kisheria) kwa
mwaka wowote ule wa fedha kwa madhumuni
yoyote yale na ambayo fedha hazikuidhinishwa
katika Sheria ya Matumizi ya mwaka ule;
72
Ruhusa ya
matumizi
ya Mfuko
Mkuu wa
Hazina kwa
Sheria ya
Matumizi
ya Fedha
Makadirio.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
Maelezo ya matumizi ya ziada, au, kadri itavyokuwa Makadirio
ya matumizi ya nyongeza yatawasilishwa kwenye Baraza la Wawakilishi
kuyakubali hayo Makadirio ya Matumizi ya Nyongeza au Maelezo ya
Matumizi ya Ziada, kutawasilishwa kwenye Baraza la Wawakilishi
Mswada wa Sheria ya Matumizi ya Fedha za Serikali kwa ajili ya
kuidhinishwa matumizi ya fedha kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina ya
Serikali, na fedha hizo zitatumiwa kulipia gharama za shughuli
zinazohusika na Makadirio au Maelezo hayo.
(3) Kwa madhumuni ya kifungu hiki na vifungu vitavyofuata
"Matumizi yanayohitajika kisheria" maana yake ni:
(a) matumizi yanayotoka katika Mfuko Mkuu wa
Hazina au katika Mapato ya Taifa kwa masharti ya
vifungu vya sheria nyengine yoyote inayotumika;
(b) riba juu ya deni la Taifa, fedha zinazowekwa akiba
kwa ajili ya kulipa deni, na gharama zote ambazo
zinaambatana na usimamizi wa deni hilo.
107.(1) Hakuna malipo yatayofanywa kutoka Mfuko Mkuu wa
Hazina ila kwa idhini ya Waziri anayehusika na fedha kwa kutoa waraka
maalum kuhusu matumizi hayo.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya kifungu 108 hakuna idhini
itayotolewa ila kwa matumizi yaliyokubaliwa na Sheria ya Matumizi
ya mwaka unaohusika au kwa maelezo ya ziada au kwa kadri
itavyokuwa matumizi ya nyongeza yaliyoidhinishwa na Baraza la
Wawakilishi kwa mujibu wa kifungu cha 106(2) au kwa shughuli
ambazo kisheria zinalipwa toka katika Mfuko Mkuu wa Hazina.
73
Malipo
kwa idhini
ya Hati
Maalum.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
108.(1) Baraza la Wawakilishi linaweza kutunga Sheria kwa
kuanzisha Mfuko wa Matumizi ya Dharura na kwa kumruhusu Waziri
anayeshughulikia mambo ya fedha, ikiwa ataridhika kwamba
kumekuwa na jambo la dharura na muhimu linalohitaji matumizi na
ambalo hakuna njia nyengine ya kisheria ya kupata matumizi hayo,
kutoa fedha katika Mfuko huo kwa ajili hiyo.
(2) Pale ambapo fedha zimetolewa katika Mfuko huo,
Matumizi ya Nyongeza yatapelekwa Baraza la Wawakilishi kwa haraka
inavyowezekana kwa madhumuni ya kuzirejesha fedha hizo zilizotumika.
109.(1) Iwapo mwaka wa Fedha wa Serikali umeanza na Sheria
ya Matumizi ya Fedha ya Serikali inayohusika na mwaka huo haijaanza
kutumika basi Rais wa Zanzibar anaweza kuidhinisha fedha itolewe
kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali kwa ajili ya kulipa gharama
za lazima za shughuli za Serikali, na fedha hizo zitatumika kwa kipindi
kisichozidi miezi mitatu tangu mwanzo wa mwaka wa fedha au mpaka
Sheria ya Matumizi ya Fedha za Serikali itakapoanza kutumika
kutegemea ni lipi kati ya mambo hayo litakalotokea mapema zaidi.
(2) Kwa sharti ya kwamba uidhinishaji huo kwa kipindi hicho
hautozidi robo ya fedha ambazo ziliombwa kutoka Mfuko Mkuu wa
Hazina kama zilivyoidhinishwa na Baraza la Wawakilishi kwa kipindi
cha mwaka wa fedha uliomalizika; lakini na vile vile kwa sharti ya
kwamba fedha hizo kwa pamoja zitaingizwa katika vifungu
vinavyohusika katika Sheria ya Matumizi ya Fedha inayofuata.
110.(1) Deni la Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar litadhaminiwa
na Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
74
Deni la
Serikali ya
Mapinduzi
ya Zanzibar.
Matumizi
ya mfuko
wa dharura.
Matumizi
ya fedha
kabla ya
sheria
kuanza
kutumika.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(2) Kwa madhumuni ya ufafanuzi wa kifungu hiki, deni la
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar maana yake ni deni lenyewe na pia
faida inayolipwa juu ya deni hilo, fedha zinazowekwa akiba kwa ajili
ya kulipa deni pole pole na gharama zile zinazoambatana na usimamizi
wa deni hilo.
111.(1) Watumishi wa Serikali wanaohusika na masharti ya kifungu
hiki watalipwa mshahara na posho kama itavyoelezwa na Sheria
iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi.
(2) Mishahara na marupurupu kwa watu wanaoshika nyadhifa
zinazohusiana na kifungu hiki pamoja na malipo ya uzeeni na kiinua
mgongo italipwa kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina.
(3) Mishahara inayolipwa kwa watu wa aina hii (mbali na
posho ambalo linazingatiwa katika pencheni) hautobadilishwa kwa
madhumuni ya kumkandamiza baada ya kuteuliwa kwake.
(4) Inapokuwa mshahara wa mtu au masharti mengine ya
utumishi yanategemea na kuchagua kwake, mshahara au masharti
ambayo kwa madhumuni ya kijifungu cha (3) yatajaaliwa ni kwa
manufaa yake zaidi kulikoni mshahara au masharti mengine
aliyoyawacha.
(5) Kifungu hiki kinawahusu Makamo wa Kwanza wa Rais
na Makamo wa Pili wa Rais, Spika, Jaji Mkuu, Majaji wa Mahkama
Kuu, Kadhi Mkuu, Wajumbe wa Kamisheni ya Utumishi wa Umma,
Mwanasheria Mkuu, Mkurugenzi wa Mashtaka na Mdhibiti na
Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.
75
Malipo ya
baadhi ya
maafisa.
Kif. 36 cha
Sheria
Nam. 2/
2002.
Tang. Nam.
47/2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
112.(1) Kutakuwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar atakaeteuliwa na Rais.
(2) Mtu hatoweza kuchaguliwa kuwa Mdhibiti na Mkaguzi
Mkuu wa Hesabu za Serikali mpaka awe na sifa zifuatazo:
(a) Shahada ya Chuo Kikuu inayotambulika
inayohusiana na mambo ya Uchunguzi wa Hesabu;
au
(b) Shahada nyenginezo za diploma za uchunguzi wa
hesabu; na
(c) Mafunzo yanayohusiana na mambo hayo ambayo
yamepatikana baada ya kupata moja kati ya shahada
yoyote iliyoainishwa katika kijifungu cha (2) (a) cha
kifungu hiki na kwamba amefanya kazi katika
shughuli hizo kwa muda usiopungua miaka mitano.
(3) Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
atakuwa na jukumu juu ya mambo yafuatayo:
(a) kuhakikisha kwamba fedha zote zinazokusudiwa
kutolewa kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar matumizi yake
yameidhinishwa kisheria na iwapo atatosheka
kwamba masharti hayo yatatekelezwa ipasavyo, basi
ataidhinisha fedha hizo zitolewe;
(b) kuhakikisha kwamba fedha zote ambazo matumizi
yake yameidhinishwa yanatokana na fedha zilizomo
katika Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali ya
76
Mdhibiti
na
Mkaguzi
Mkuu wa
Hesabu za
Serikali.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
Mapinduzi au fedha arnbazo matumizi yake
yameidhinishwa na Sheria iliyotungwa na Baraza la
Wawakilishi, na ambazo zimetumika kwa ajili ya
shughuli zilizohusika na matumizi ya fedha hizo na
kwamba matumizi hayo yamefanywa kwa kufuata
idhini iliyotolewa kuhusu matumizi hayo; na
(c) angalau mara moja kila mwaka kufanya ukaguzi na
kutoa taarifa juu ya ukaguzi wa hesabu za Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar, hesabu zinazosimamiwa
na watumishi wote wa Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar, hesabu za Mahkama zote za Zanzibar,
hesabu za Tume au vyombo vyengine
vilivyoanzishwa na Katiba hii na hesabu zozote
zinazohusika na Baraza la Wawakilishi.
(4) Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali na
kila mtumishi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar aliyeruhusiwa na
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali atakuwa na haki ya
kuchunguza vitabu, kumbukumbu, hati za maelezo, taarifa na hati
nyenginezo zote zinazohusika na hesabu za aina yoyote iliyotajwa katika
kijifungu cha (3) cha kifungu hiki.
(5) Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
atawasilisha kwa Rais kila taarifa atakayotoa kwa mujibu wa masharti
ya kijifungu cha (3) (c) cha kifungu hiki. Baada ya kupokea taarifa
hiyo Rais atawaagiza watu wanaohusika wawasilishe taarifa hiyo
kwenye kikao cha kwanza cha Baraza la Wawakilishi kitachofanyika
baada ya Rais kupokea taarifa hiyo na itabidi iwasilishwe katika kikao
hicho kabla ya kupita siku saba tangu siku ile kilipoanza kikao hicho.
Iwapo Rais hatachukua hatua za kuwasi1isha taarifa hiyo kwenye
Baraza la Wawakilishi, basi Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu
77
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
za Serikali atawasilisha taarifa hiyo kwa Spika wa Baraza la
Wawakilishi au Naibu Spika ambaye atawasilisha taarifa hiyo kwenye
Baraza la Wawakilishi.
(6) Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
atakuwa pia na jukumu la kutekeleza kazi na shughuli nyengine, na
atakuwa na madaraka mengine ya namna mbali mbali, kama
itakavyoelezwa na sheria, kuhusu hesabu za Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar au hesabu ya Mashirika na Makampuni ya Umma ya Zanzibar.
(7) Katika kutekeleza madaraka yake kwa mujibu wa
masharti ya kijifungu cha (3), (4) na (5) ya kifungu hiki, Mdhibiti na
Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali hatalazimika kufuata amri au
maagizo ya mtu mwengine yeyote au Idara yoyote ya Serikali, lakini
maelezo haya ya kifungu hiki hayataizuia Mahkama nayo kutumia
madaraka yake kwa ajili ya kuchunguza kama Mdhibiti na Mkaguzi
Mkuu wa Hesabu za Serikali ametekeleza madaraka yake kwa mujibu
wa masharti ya Katiba hii au siyo.
(8) Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
hatoanza kazi yake ila kwanza ale Kiapo cha Uaminifu na kiapo chengine
chochote kitachowekwa na Baraza la Wawakilishi kwa ajili ya utendaji
wake wa kazi.
113.(1) Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali anaweza
tu kuondolewa katika madaraka ya kazi yake kwa sababu ya
kushindwa kutekeleza kazi zake (ama kutokana na maradhi au sababu
nyengine yoyote) au kwa sababu ya tabia mbaya, na hataweza
kuondolewa kazini ila kwa mujibu wa masharti ya kijifungu cha (3)
cha kifungu hiki, venginevyo ataendelea na kazi hiyo hadi kutimiza umri
wa kuacha kazi kwa mujibu wa Sheria iliyotungwa na Baraza la
Wawakilishi.
78
Kumuondoa
kazini
Mdhibiti na
Mkaguzi
Mkuu wa
Hesabu za
Serikali.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(2) Iwapo suala la kumuondoa kazini Mdhibiti na Mkaguzi
Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mujibu wa masharti ya kifungu hiki
linahitaji kuchunguzwa, basi utaratibu ufuatao ndio utakaotumika:
(a) Rais atateua Tume Maalum ambayo itakuwa na
Mwenyekiti na Wajumbe wengine wasiopungua
wawili;
(b) Tume hiyo itachunguza shauri lote halafu itatoa taarifa
kwa Rais kuhusu maelezo ya shauri lote pamoja na
ushauri wao kama huyo Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu
wa Hesabu za Serikali aondolewe kazini kwa
mujibu wa masharti ya kifungu hiki kwa sababu ya
kushindwa kufanya kazi kutokana na maradhi au
sababu nyengine yoyote au kwa sababu ya tabia
mbaya.
(3) Ikiwa Tume iliyoteuliwa kwa mujibu wa masharti ya
kijifungu cha (2) itamshauri Rais kwamba huyo Mdhibiti na Mkaguzi
Mkuu wa Hesabu za Serikali aondolewe kazini kwa sababu ya
kushindwa kufanya kazi kutokana na maradhi au sababu nyengine
yoyote au kwa sababu ya tabia mbaya, basi Rais atamuondoa kazini.
(4) Iwapo Tume itamshauri Rais kwamba huyo Mdhibiti na
Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali asiondolewe kazini basi Rais
anaweza kukubali au kukataa mapendekezo hayo na hapo Rais
atatumia busara zake.
(5) Mtu ambaye ni Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu
za Serikali au aliyepata kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu
za Serikali hawezi kuteuliwa kushika au kushikilia madaraka ya kazi
nyengine yoyote katika utumishi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
79
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
Sehemu ya Pili
Masharti ya Fedha Yahusuyo Mambo ya Muugano.
114. Fedha zote ambazo ni sehemu ya mchango wa Muungano
na ambazo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inawajibika kulipa zitakuwa
ni gharama itakayotoka Mfuko Mkuu wa Hazina.
115. Hakuna fedha itayotumiwa katika Sehemu hii hadi:
(a) Tume ya Pamoja ya Fedha inayohusu mambo ya
Muungano kama ilivyoanzishwa na Katiba ya
Muungano imechambua mapato na matumizi ya
shughuli za Muungano na kutoa mapendekezo yake
kwa vyombo vinavyohusika juu ya mgawanyo wa
matumizi hayo; na
(b) Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuyakubali
mapendekezo hayo na mgawanyo wake.
SURA YA NANE
Kamisheni ya Utumishi wa Umma
116.(1) Kutakuwa na Kamisheni ya Utumishi wa Umma ambayo
itakuwa ni chombo cha juu kabisa kwa Tume zote za Utumishi, chenye
mamlaka ya kusimamia na kuratibu mambo yote ya utumishi wa umma
kwa Zanzibar.
(2) Muundo, kazi na uwezo wa Kamisheni ya Utumishi wa
Umma utakuwa kama itakavyoelezwa na Sheria iliyotungwa na Baraza
la Wawakilishi.
Mchango
wa
Muungano.
Uwezo wa
kutumia
kasma.
Kamisheni
ya
Utumishi
wa Umma.
Kif.58 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
80
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
117. Kutakuwa na Tume ya Utumishi ya Serikali kama
itavyoelezwa na Sheria iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi.
118. Bila ya kuathiri masharti ya Katiba, Tume za Utumishi
zilizotajwa ndani ya Katiba zitakuwa na mamlaka yafuatayo:
(a) kuajiri watu kushika nafasi za utumishi;
(b) kuthibitisha ajira zao za utumishi;
(c) kusitisha au kuachisha utumishi wao;
(d) kupendekeza serikalini mishahara na marupurupu ya
watumishi wao; na
(e) mamlaka mengine yoyote zitakazopewa kwa mujibu
wa Sheria iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi.
SURA YA TISA
Tume ya Uchaguzi
119.(1) Kutakuwa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ambayo
itakuwa na wajumbe wafuatao:
(a) Mwenyekiti atakayeteuliwa na Rais kwa utaratibu
atakaoona unafaa;
(b) Wajumbe wawili watakaoteuliwa na Rais kufuatana
na mapendekezo ya Kiongozi wa shughuli za Serikali
kwenye Baraza la Wawakilishi;
Tume ya
Utumishi
ya Serikali.
Kif.59 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
81
Uwezo wa
Tume za
Utumishi.
Kif. 60 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
Tume ya
Uchaguzi.
Kif. 37 cha
Sheria
Nam. 2/
2002 na
Kif. 4 cha
Sheria Nam
8/2002.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
(c) Wajumbe wawili watakaoteuliwa na Rais kufuatana
na mapendekezo ya Kiongozi wa Upinzani katika
Baraza la Wawakilishi au iwapo hakuna kiongozi
wa upinzani basi kwa kushauriana na vyama vya
siasa;
(d) Mjumbe mmoja atakayeteuliwa na Rais kutoka
miongoni mwa Majaji wa Mahakama Kuu;
(e) Mjumbe mmoja atakayeteuliwa na Rais kama Rais
atakavyoona inafaa.
(2)(a) Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi atakuwa mtu
aliyekuwa au mwenye sifa za kuwa Jaji katika
Mahkama Kuu au Mahkama ya Rufaa katika nchi
yoyote iliyo mwanachama wa Jumuiya ya Madola
au mtu anayeheshimika katika jamii.
(b) Tume ya Uchaguzi itamteua Makamo Mwenyekiti
kutoka miongoni mwa Wajumbe wake.
(3) Watu wafuatao hawataweza kuteuliwa kuwa Wajumbe
wa Tume ya Uchaguzi yaani:
(a) Waziri au Naibu Waziri;
(b) Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi au ikiwa ni
miongoni mwa majeshi ya Tanzania au ana wadhifa
wowote ambao kisheria haruhusiki kuwa mjumbe
wa Tume;
(c) Mbunge au mtu mwengine mwenye madaraka ya
aina yoyote aliyotajwa na Sheria iliyotungwa na
82
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
Bunge kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya
(2) ya Ibara ya 67 ya Katiba ya Muungano;
(d) Kiongozi wa chama chochote cha Siasa.
(4) Bila ya kuathiri masharti mengine ya kifungu hiki, Mjumbe
wa Tume ya Uchaguzi atasita tu kuwa Mjumbe litokeapo lolote kati
ya mambo yafuatayo:
(a) ukimalizika muda wa miaka mitano tangu
alipoteuliwa; au
(b) ikiwa litatokea jambo lolote ambalo, kama
asingekuwa Mjumbe ligemfanya asiweze kuteuliwa
kuwa Mjumbe wa Tume ya Uchaguzi.
(5) Rais anaweza tu kumuondoa katika madaraka Mjumbe
wa Tume ya Uchaguzi kwa sababu ya kushindwa kutekeleza kazi zake,
ama kutokana na maradhi au sababu nyengine yoyote, au kwa sababu
ya tabia mbaya au kupoteza sifa za kuwa Mjumbe.
(6) Mjumbe wa Tume ataondolewa kwenye madaraka yake
na Rais ikiwa suala la kuondolewa kwake kwenye madaraka
limepelekwa kwa Tume maalum iliyoundwa kwa ajili hiyo chini ya
kijifungu cha (7) na Tume hiyo imependekeza kwa Rais kwamba
Mjumbe huyo angefaa aondolewe kutokana na kutomudu kazi zake
kama ilivyoelezwa hapo juu.
(7) Ikiwa Rais atahisi kwamba suala la kumuondoa Mjumbe
wa Tume lingefaa kuchunguzwa, basi:
83
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
(a) Rais atateuwa Tume Maalum itayokuwa na
Mwenyekiti na Wajumbe wasiopungua wawili
kutokana na watu wanaoshikilia au waliowahi
kushika wadhifa wa Jaji wa Mahkama zenye
mamlaka ya kusikiliza kesi za aina zote Tanzania,
au Jaji wa Mahkama ya Rufaa yenye mamlaka ya
rufaa kutoka Mahkama hizo; na
(b) Tume itachunguza suala hilo na itapendekeza kwa
Rais kama Mjumbe huyo angefaa aondolewe au
la.
(8) Ikiwa suala la kumuondoa Mjumbe limepelekwa kwa
Tume Maalum kwa kuchunguzwa, Rais anaweza kumsimamisha kazi
Mjumbe huyo na kumsimamisha huko kunaweza wakati wowote
kukatenguliwa na Rais, na kwa hali yoyote hakutokuwa na taathira
yoyote ikiwa Tume hiyo imependekeza kwamba Mjumbe huyo
asiondolewe kwenye madaraka yake.
(9) Kwa madhumuni ya utekelezaji bora wa majukumu yake,
Tume ya Uchaguzi itakuwa ni Idara inayojitegemea na mtendaji mkuu
wake atakuwa ni Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye atateuliwa na
kufanya kazi kwa mujibu wa masharti ya Sheria iliyotungwa na Baraza
la Wawakilishi.
(10) Kiwango cha mikutano ya Tume ya Uchaguzi ni
Mwenyekiti au Makamo Mwenyekiti na Wajumbe wanne na kila uamuzi
wa Tume ni lazima uungwe mkono na Wajumbe walio wengi.
(11) Baraza la Wawakilishi linaweza kutunga Sheria kwa ajili
ya kuweka masharti ya kuweka utaratibu wa kuwateuwa Wajumbe
wa kusimamia uchaguzi wa Rais, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi
84
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
na Madiwani na bila ya kuathiri masharti ya sheria kama hiyo au maagizo
ya Tume ya Uchaguzi, madaraka ya Tume ya Uchaguzi ya kusimamia
uchaguzi yanaweza kutekelezwa na Wajumbe hao.
(12) Katika kutekeleza madaraka yake kwa mujibu wa
masharti ya Katiba hii, Tume ya Uchaguzi haitalazimika kufuata amri
au maagizo ya mtu yeyote au Idara yoyote ya Serikali, au maoni ya
chama cha siasa.
(13) Hakuna Mahkama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya
kuchunguza jambo lolote lililotendwa na Tume ya Uchaguzi katika
kutekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.
(14) Katika utekelezaji wa madaraka yake kwa mujibu wa
Katiba hii, Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar itashauriana mara kwa mara
na Tume ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano.
120.(1) Bila ya kuathiri masharti ya kifungu hiki, Zanzibar inaweza
kugaiwa katika majimbo ya uchaguzi yenye majina na mipaka kama
yatakavyoelezwa na Tume.
(2) Baraza la Wawakilishi linaweza kuweka kisheria, idadi
ndogo kabisa ya majimbo ya uchaguzi yasiyopungua 40 na idadi kubwa
kabisa ya majimbo yasiyozidi 55.
(3) Majimbo yote yatakuwa karibuni na wakaazi sawa sawa
kama itakavyoonekana na Tume, lakini Tume inaweza kuepuka shuruti
hii kwa kiwango kile kinachofikiria kuwa inafaa kwa ajili ya kuzingatia:
(a) idadi ya watu na zaidi katika kuhakikisha uwakilishi
unaofaa katika miji mikubwa na miji ya mashamba
yenye idadi ndogo ya watu;
85
Majimbo.
Kif. 61 cha
Sheria
Nam. 9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
(b) ukuaji wa idadi ya watu;
(c) njia za usafiri;
(d) mipaka ya sehemu ya utawala, na kwa madhumuni
ya kifungu hiki idadi ya wakaazi wa sehemu yoyote
ya Zanzibar itahakikishwa na ripoti ya kuhesabu
watu ya karibuni sana ambayo imefanywa kwa
mujibu wa sheria.
(4) Katika kipindi cha miaka 8 hadi 10 au wakati wowote
Tume itachunguza idadi ya mipaka na majina ya majimbo hayo kwa
kiwango kile ambacho inahisi ni wajibu kuangaliwa upya, na inaweza
kwa kutoa tangazo, kubadili idadi, mipaka na majina ya majimbo hayo.
(5) Iwapo hesahu ya idadi ya watu imeshafanywa kwa mujibu
wa sheria, au iwapo mabadiliko yamefanywa katika mipaka ya sehemu
yoyote ya utawala, Tume inaweza ikachunguza suala hilo na kuweka
mabadiliko hayo katika kiwango kile ambacho Tume inahisi ingefaa
kufanyiwa mabadiliko hayo.
(6) Amri yoyote iliyofanywa na Tume chini ya kifungu hiki
itatangazwa katika Gazeti Rasmi na itaanza kutumika tarehe ambayo
itaainishwa katika Gazeti hilo.
SURA YA KUMI
Idara Maalum
121.(1) Kutakuwa na ldara Maalum za Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar ambazo kazi zake na shughuli zake zitakuwa kama
zitavyoainishwa katika sheria zinazohusika.
86
ldara
Maalum.
Kif. 62 cha
Sheria
Nam. 9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(2) Idara Maalum zilizoainishwa katika kijifungu cha (1) hapa
juu ni:-
(a) Jeshi Ia Kujenga Uchumi (kwa ufupi JKU);
(b) Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo (kwa kifupi
KMKM);
(c) Chuo cha Mafunzo (cha wahalifu).
(3) Rais wa Zanzibar anaweza, ikiwa ataona inafaa kuanzisha
Idara nyengine yoyote kuwa Idara Maalum.
(4) Mtu yeyote aliye katika utumishi wa Idara Maalum
haruhusiwi kujishughulisha na mambo ya siasa, isipokuwa kupiga kura
katika uchaguzi wowote kulingana na masharti ya kifungu cha 7 cha
Katiba.
122. Kutakuwa na Tume ya Utumishi ya ldara Maalum ambayo
uwezo wake, nguvu zake, kazi zake na Kanuni za mwenendo wake
zitakuwa kama zitavyoainishwa katika Sheria itakayotungwa na Baraza
la Wawakilishi kwa ajili hiyo.
123.(1) Rais atakuwa Kamanda Mkuu wa Idara Maalum na
atakuwa na uwezo wa kufanya chochote kile anachohisi, kwa maslahi
ya Taifa, kinafaa.
(2) Uwezo wa Rais chini ya kijifungu cha (1) unaingiza uwezo
wa kutoa amri ya kufanya shughuli yoyote inayohusiana na Idara hiyo
kwa manufaa ya Taifa.
87
Tume ya
Utumishi
ya Idara
Maalum.
Kif. 63 cha
Sheria
Nam. 9/
2010.
Uwezo wa
Rais
katika
Idara
Maalum.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
SURA YA KUMI NA MOJA
Mamlaka ya Baadhi ya Vyombo vya Muungano
124.(1) Vyombo vilivyoainishwa chini ya kijifungu cha (2) cha
kifungu hiki na kama vilivyoanzishwa kwa mujibu wa vifungu vya Katiba
ya Muungano, vitakuwa na mamlaka ya kutekeleza shughuli zake
Zanzibar kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa katika Katiba ya
Muungano na Sheria yoyote nyengine iliyotungwa na ama Bunge au
Baraza la Wawakilishi kwa ajili hiyo.
(2)Vyombo vyenyewe vilivyotajwa katika kijifungu cha(1) ni:
(a) Mahkama ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano;
(b) Tume ya Pamoja ya Fedha ya Jamhuri ya
Muungano;
(c) Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Jamhuri ya
Muungano.
(3) Kwa madhumuni ya kifungu hiki, vyombo vilivyoainishwa
katika kijifungu cha (2) vitahesabika kama ni vyombo vya Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar katika shughuli zake hapa Zanzibar.
SURA YA KUMI NA MBILI
Vyombo Vyengine vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
Sehemu ya Kwanza
Tume ya Mipango
125.(1) Kutakuwa na Tume ya Mipango ya Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar ambayo ndiyo chombo cha juu chenye uwezo wa kupanga
Mamlaka
ya baadhi
ya
vyombo
vya
Muungano
kutumika
Zanzibar.
Kif. 64 cha
Sheria
Nam. 9/
2010
88
Tume ya
Mipango.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
na kusimamia utekelezaji wa maendeleo ya kiuchumi na mipango ya
huduma za jamii katika Zanzibar.
(2) Taratibu za utekelezaji wa kazi na majukumu ya Tume ya
Mipango pamoja na Wajumbe wa Tume utakuwa kama itavyoelezwa
katika Sheria itayotungwa na Baraza la Wawakilishi.
126. Wajumbe wa Tume ya mipango na utaratibu wa mikutano
utakuwa kwa mujibu wa Sheria itakayotungwa na Baraza la
Wawakilishi la Zanzibar.
127. Kutakuwa na Katibu wa Tume ya Mipango ambaye
atateuliwa na Rais.
Sehemu ya Pili
Serikali za Mitaa
128. Kutakuwa na Serikali za Mitaa ambazo uchaguzi wa viongozi
wake, madaraka na kazi za kila Serikali ya Mtaa zitakuwa kama
zitavyoelezwa na Sheria iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi.
SURA YA KUMI NA TATU
Mambo ya Jumla
129.(1) Bila ya kuathiri masharti ya kifungu hiki, mtu yeyote ambaye
ametajwa, amechaguliwa au ameteuliwa kushika wadhifa wowote ule
ulioainishwa na Katiba hii, anaweza kujiuzulu kutoka katika wadhifa
huo kwa maandishi aliyoweka saini yake akiyapeleka kwa mtu
aliyemtaja, aliyemchagua au aliyemteua.
89
Kujiuzulu.
Kif. 66 cha
Sheria
Nam. 9/
2010.
Wajumbe
wa Tume.
Katibu wa
Tume ya
Mipango.
Serikali za
Mitaa.
Kif. 65 cha
Sheria
Nam. 9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
(2) Mtu aliyetoa taarifa ya kujiuzulu kwa mujibu wa masharti
ya kijifungu cha (1) cha kifungu hiki, atahesabiwa kuwa amejiuzulu
tangu siku ile ambayo taarifa yake ya kujiuzulu itakapopokelewa na
mtu yeyote aliyeruhusiwa kupokea taarifa hiyo na mtu anayehusika na
kikao kinachohusika, lakini kama taarifa hiyo ya kujiuzulu imeeleza
kwamba atajiuzulu siku za baadaye mtu huyo atahesabiwa kuwa
amejiuzulu tangu siku hiyo nyengine ya baadaye.
(3) Taarifa ya kujiuzulu kwa Rais itapelekwa kwa Spika
ambaye ataiwasilisha kwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya
Zanzibar.
(4) Taarifa ya kujiuzulu kwa Makamo wa Kwanza wa Rais,
Makamo wa Pili wa Rais, Waziri, Naibu Waziri na Mjumbe wa Baraza
la Mapinduzi itapelekwa kwa Rais.
(5) Taarifa ya kujiuzulu kwa Spika, itapelekwa Baraza la
Wawakilishi.
(6) Taarifa ya kujiuzulu kwa Naibu Spika, au Mjumbe wa
Baraza la Wawakilishi itapelekwa kwa Spika.
130.(1) Iwapo mtu yeyote mwenye dhamana ya kazi yoyote
iliyoanzishwa na Katiba hii amejiuzulu, basi ikiwa anazo sifa zote
zinazohitajika na kwa kila hali anastahili, anaweza kuteuliwa au
kuchaguliwa tena kushika madaraka ya kazi hiyo kwa mujibu wa
masharti ya Katiba hii.
(2) Iwapo mtu ameachishwa kazi au amesimamishwa kazi
itabidi chombo hicho au mtu huyo aliyemuachisha au aliyemsimamisha
kazi amueleze kwa maandishi kwamba amemuachisha au
amemsimamisha kazi.
90
Uteuzi
mpya na
kuarifiwa
kuachishwa
kazi.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
131. Kwa madhumuni ya ufafanuzi wa masharti ya Katiba hii
kuhusu utaratibu wa kukabidhi madaraka ya kazi katika utumishi wa
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ifahamike kuwa mtu yeyote mwenye
mamlaka kwa mujibu wa Katiba hii, ya kumteua au kumchagua mtu
mwengine kushika madaraka ya kazi fulani anao pia uwezo wa kumteua
au kumchagua Naibu au mtu ambaye atashika kwa muda na kutekeleza
madaraka ya kazi hiyo.
,132.(1) Hakuna Sheria yoyote itakayopitishwa na Bunge la
Muungano ambayo itatumika Zanzibar mpaka Sheria hiyo iwe ni kwa
ajili ya mambo ya Muungano tu na ipitishwe kulingana na maelekezo
yaliyo chini ya vifungu vya Katiba ya Jamhuri ya Muungano.
(2) Sheria kama hiyo lazima ipelekwe mbele ya Baraza la
Wawakilishi na Waziri anayehusika.
(3) Pale Sheria ndogo inapoundwa kwa mujibu wa uwezo
uliowekwa chini ya kijifungu cha (1) na (2) cha kifungu hiki itatumika
tu pale itakapotimiza shuruti zote zilizowekwa kwa matumizi ya Sheria
Mama kama ilivyoainishwa katika kifungu hiki.
133.(1) Hakuna kodi ya aina yoyote itakayotozwa isipokuwa
kwa mujibu wa Sheria iliyotugwa na Baraza la Wawakilishi au kwa
utaratibu uliowekwa kisheria na uliotiliwa nguvu na Sheria iliyotungwa
na Baraza la Wawakilishi.
(2) Masharti yaliyomo katika kijifungu cha (1) cha kifungu
hiki hayatalizuia Bunge kutumia mamlaka yake ya kutoza kodi ya aina
yoyote inayohusiana na mambo ya Muungano kwa mujibu wa
madaraka ya Bunge hilo kwa kujua kwamba mashauriano baina ya
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano
yamefanywa na kukubalika sehemu zote mbili kabla kupitishwa Sheria.
91
Maelezo
kuhusu
utaratibu
wa
kukabidhi
madaraka
ya kazi
katika
Utumishi
wa Serikali.
Sheria za
Muungano.
Masharti
ya kutoza
kodi.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
134.(1) Katika Katiba hii, ila iwapo maelezo yanahitaji
vyenginevyo:
“Baraza la Mapinduzi” linajumuisha na Baraza la Mawaziri;
“Chama” maana yake ni chama cha siasa kilichosajiliwa rasmi
chini ya Sheria ya Vyama vya Siasa ya 1992;
“Jaji” maana yake ni Jaji wa Mahkama Kuu na inajumuisha
Kaimu Jaji;
“Kiapo cha uaminifu”maana yake ni kiapo chochote cha uaminifu
kama kitavyoainishwa na Baraza la Wawakilishi;
“Kiapo” kinajumuisha na uthibitisho;
“Kikao cha Baraza la Wawakilishi” maana yake ni kikao cha
siku moja au sehemu ya siku endapo Baraza halikukaa kwa
siku nzima kinachoanza kwa kusomwa dua na kumalizika
kwa kuakhirishwa hadi siku inayofuata au siku nyengine ya
baadaye;
“Mfanyakazi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar” maana yake
ni mtu anayefanyakazi au anayeshikilia wadhifa wa kazi
katika utumishi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
pamoja na Mashirika yake;
“Mkutano wa Baraza la Wawakilishi” maana yake ni mfululizo
wa vikao vya Baraza kuanzia kikao cha kwanza hadi
kufikia wakati ambao shughuli zote zilizopangwa kwa ajili
ya mkutano huo zitakuwa zinamalizika;
92
Ufafanuzi.
Kif. 38 cha
Sheria
Nam. 2/
2002 na
Kif. 67 cha
Sheria
Nam.9/
2010.
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
“Mwaka wa Fedha” maana yake ni kipindi cha miezi 12
kinachomalizikia tarehe 30 Juni ya mwaka wowote au kwa
siku nyengine yoyote kama Baraza la Wawakilishi
litakavyoainisha kwenye Sheria;
“Rais” maana yake ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi;
“Waziri” maana yake ni Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi na
Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi aliyekabidhiwa wadhifa
wa kazi ya Waziri katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
“Utumishi wa Umma” maana yake ni ajira katika utumishi
unaosimamiwa moja kwa moja na Tume ya Utumishi
Serikalini, Tume ya Utumishi ya Mahkama, Tume ya
Utumishi ya Baraza la Wawakilishi, Tume ya Utumishi ya
Idara Maalum na inajumuisha utumishi katika taasisi
zinazojitegemea ambazo zinafanya kazi za Serikali au
zinazomilikiwa na Serikali na kadri tafsiri itavyohitaji,
inajumuisha utumishi katika Mashirika ya kibiashara
yanayomilikiwa na Serikali. Isipokuwa kwamba
haitajumuisha utumishi wa kisiasa na utumishi wa maofisa
ambao Sheria iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi kwa
masharti ya wazi imewaondoa katika tafsiri ya Utumishi
wa Umma.
(2) Ila iwapo maelezo yatahitaji vyenginevyo, uwezo wowote
uliopewa Baraza la Wawakilishi na Katiba hii kwa kuanzisha au kuelezea
jambo lolote basi utafanywa kwa kutungiwa Sheria.
(3) Kwa madhumuni ya Katiba hii, mtu hatahesabiwa kuwa
na madaraka ya kazi katika utumishi wa Serikali ya Mapinduzi ya
93
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
Zanzibar kwa sababu tu kwamba anapokea malipo ya uzeeni au malipo
mengine ya aina hiyo kwa ajili ya utumishi wake wa zamani.
(4) Katika Katiba hii, ila iwapo maelezo yatahitaji
vyenginevyo, kila anapotajwa mtu mwenye dhamana ya kazi fulani
kwa kutaja madaraka ya kazi yake, ifahamike kuwa mtu anayehusika
kuwa ni pamoja na mtu yeyote ambaye ni Kaimu au aliyeteuliwa kwa
njia ya halali kushikilia dhamana ya kazi hiyo.
(5) Iwapo Katiba inatoa uwezo au nguvu fulani, basi uwezo
huo au nguvu hizo zinaweza kutekelezwa wakati wowote inapohitajika.
(6) Katika Katiba hii, kila yalipotajwa mamlaka ya
kumuondoa mtu katika madaraka ya kazi katika utumishi wa Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar, ifahamike kuwa mamlaka yanayohusika ni
pamoja na mamlaka yaliyotolewa kwa mujibu wa masharti ya sheria
yoyote yanayomtaka mtu huyo au yanayomruhusu mtu huyo kustaafu.
(7) Iwapo mtu ameteuliwa kwa mujibu wa masharti ya Katiba
hii, kuwa Naibu au kushikilia madaraka ya kazi fulani wakati mtu maalum
aliyeteuliwa kushika madaraka ya kazi hiyo anashindwa kutekeleza
shughuli zinazohusika na kazi hiyo, basi haitaruhusiwa kufanya uchunguzi
wowote, kutoa hoja yoyote juu ya uteuzi wa huyo Naibu kwa sababu
tu kwamba huyo mtu maalum aliyeteuliwa kushika madaraka ya kazi
hiyo hakushindwa kutekeleza shughuli zinazohusika na kazi hiyo.
(8) Katika kifungu chochote cha Katiba hii kinachosema
kwamba hakuna mtu au chombo fulani kitachoingiliana na mtu au
chombo chochote katika kutekeleza kazi zake basi hakitokuwa na
maana ya kwamba Mahkama zitazuilika katika mamlaka yake katika
suala lolote hata kama mtu huyo au chombo hicho kimetekeleza wajibu
wake kwa mujibu wa Katiba hii au sheria nyengine yoyote.
94
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
(9) Katika Katiba hii, kila ilipotajwa sheria ambayo inabadilisha
au kufuta sheria nyengine, ifahamike kuwa sheria inayohusika ni pamoja
na sheria ambayo inarekebisha sheria hiyo nyengine au ambayo
inaendeleza kutumika kwa hiyo sheria nyengine ama bila ya mabadiliko
au baada ya kubadilishwa au kurekebishwa au sheria ambayo inaweka
masharti mapya katika sheria nyengine.
134A. Katiba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya 1979
imefutwa.
135.(1) Jina la Katiba hii litakuwa “Katiba ya Zanzibar ya 1984”.
(2) Katiba hii itaanza kutumika kuanzia tarehe 12 Januari,
1985.
95
Jina la
Katiba na
tarehe ya
kuanza
kutumika.
Kufutwa
Katiba ya
1979.
Kif. 39 cha
Sheria
Nam. 2/
2002.
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
96
_________________________K__a_ti_b_a_ y_a_ _Z_a_n_z_i_b_a_r_ y_a_ _1_9_8_4_________________________
KATIBA YA ZANZIBAR YA 1984
Toleo la 2010
(Toleo hili la Katiba ya Zanzibar ya 1984 linajumuisha na kuweka
pamoja marekebisho yote ya Katiba ya Zanzibar yaliyofanywa
kuanzia mwaka 1985 hadi tarehe 13 Agosti, 2010 kwa madhumuni
ya kurahisisha marejeo ya Katiba)
Zanzibar { IDI PANDU HASSAN }
15 Septemba, 2010 Mwanasheria Mkuu
Zanzibar
Imepigwa Chapa na
Kiwanda cha Uchapaji Chuo Kikuu cha Elimu - Chukwani- Zanzibar
_________________________K__a_ti_b_a_ _y_a_ Z__a_n_zi_b_a_r_ _ya_ _1_9_8_4_________________________
KATIBA YA ZANZIBAR
YA
1984
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company