HABARI KUU ZA LEO na OSCAR SAMBA
print this page
HABARI NA Oscar Samba

Kura ya siri, wazi kaa la moto Bunge la Katiba



Mjumbe wa Bunge maalumu la Katiba, Chritopher Ole Sendeka
Na Daniel Mjema na Sharon Sauwa, Mwananchi
Dodoma. Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, juzi na jana wamekuwa katika mtihani mgumu wa kufikia uamuzi wa pamoja kuhusu utaratibu wa upigaji kura, kati ya kura ya wazi na kura ya siri.

Habari kutoka katika kikao cha ndani cha Chama Cha Mapinduzi (CCM), zilisema kutokana na mvutano huo, mjumbe mmoja, Chritopher Ole Sendeka, alijikuta akilia hadharani akitetea upigaji kura ya wazi.
0 Toa maoni yako.

Mafuta yaonekana ya ndege iliyotoweka


Wakuu wa Vietnam wanasema michirizi miwili mikubwa ya mafuta imeonekana katika bahari nje ya mwambao wa kusini wa nchi hiyo, huku msako unaendelea kutafuta ndege ya Shirika la Ndege la Malaysia iliyotoweka Jumamosi asubuhi.
0 Toa maoni yako.

Siku ya kimataifa ya wanawake yaadhimishwa kote Duniani

Kauli mbiu ya mwaka huu kuadhimisha siku ya kimataifa ya wanawake ni ;“ Usawa kwa wanawake ni maendeleo kwa wote.”
Wanawake wa Malaysia wakivalia mavazi ya kitamaduni washerehekea siku ya kimataifa ya wanawake duniani.
Siku ya kimataifa ya wanawake inaadhimishwa kote duniani leo Jumamosi. Umoja wa Mataifa umesema siku hii ni ya kutafakari juu ya hatua za kimaendeleo ambazo wanawake wamepiga, kupongeza juhudi za wanawake wa kawaida kutokana na mchango wao katika historia ya maendeleo ya nchi zao na jamii zao.
0 Toa maoni yako.

Rwanda yajibu mapigo sasa yamfukuza afisa wa Afrika Kusini

Jenerali Kayumba Nyamwasa
Waziri wa mashauri ya nchi za nje wa Rwanda amethibitisha kuwa serikali inawafukuza maafisa sita wa ubalozi wa Afrika Kusini, saa chache baada ya Afrika Kusini kuwataka raia watatu wa Rwanda kuondoka nchini humo.

Afrika Kusini ilichukua hatua hiyo baada ya nyumba ya mpinzani mmoja wa Rwanda anayeishi Afrika Kusini kushambiliwa siku ya Jumaane.
0 Toa maoni yako.

MEZA YA MAGAZETI LEO JUMAMOSI





0 Toa maoni yako.

CHADEMA KUANZA KAMPENI YA CHOPA LEO KATIKA JIMBO LA KALENGA



Leo ndani ya KALENGA tunaanza kampeni ya chopa, pamoja na kamanda Lema. Mpaka kieleweke.

Na Peter Msigwa
0 Toa maoni yako.

‘Natembea na barua ya kifo mkononi’



Veronica Kibuga (katikati) pamoja na watoto wake.
Na Julieth Kulangwa , Mwananchi
Magu. Hebu fikiri... Unaamka asubuhi na kukuta kundi la majirani nje ya mlango wa nyumba yako. Uwepo wao siyo kwa lengo la kukusalimu, bali kukupa ujumbe wa hatima ya maisha yako.

Hali hii ndiyo iliyomkuta Veronica Kibuga (85) mkazi wa Kitongoji cha Kahangala wilayani Magu, Mwanza ambaye kwa miezi kadhaa amekuwa akiishi kwa hofu kwani anasubiri utekelezaji wa ‘adhabu ya kifo’ kukatwa kwa mapanga kutokana na tuhuma kuwa yeye ni mchawi.
0 Toa maoni yako.

Wanyarwanda watatu waondolewa Afrika ya kusini


Raisi Wa Rwanda Paul Kagame
  Na RFI
Afrika ya kusini imewaondoa wanadiplomasia watatu raia wa Rwanda ikiwahusisha na shambulizi dhdidi ya makazi ya kiongozi wa zamani wa Rwanda Kayumba Nyamwasa.

Taarifa zinabainisha kuwa Rwanda nayo imeamuru kuondolewa kwa wajumbe sita wa Afrika ya kusini .

Hatua hizo zinakuja baada ya watu wenye silaha kushambulia makazi ya Kayumba Nyamwasa aliyewahi kushika wadhifa wa juu katika serikali ya Rwanda.
0 Toa maoni yako.

Kenyatta, Ruto na serikali kupunguziwa mishahara

Baraza la mawaziri la Kenya na wajumbe wa tume ya bajeti ya bunge
Rais Uhuru Kenyatta, atapunguziwa mshahara wake kwa Sh 248,000 za Kenya karibu sawa na dola 3,000, na naibu rais William Ruto anapunguziwa Sh210,000. mawaziri na makatibu wakuu wote wanapunguziwa pia mishahara yao kwa asili mia 10.
0 Toa maoni yako.

ICC yamtia hatiani Katanga wa DRC


Mtuhumiwa wa mauaji ya jinai Germain Katanga
Mahakama ya kimataifa ya jinai ICC imempata na hatia ya uhalifu wa kivita mbabe wa kivita kutoka Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo, Germain Katanga.
0 Toa maoni yako.

Kaimu rais wa Ukraine atia saini kufuta kura ya maoni.

Waandamanaji wakibeba mabango wakati wa maandamano ya kupinga vita mbele ya jengo la ubalozi wa Russia huko Kyiv.Machi 7, 2014.
Kaimu rais wa Ukriane Oleksandr Turchynov ametia saini amri ya kufuta kura ya maoni iliyopangwa kufanyika Crimea kutaka kujiunga na Russia, lakini maafisa wa Crimea wameapa kuendelea na mpango wao.
0 Toa maoni yako.

WAFUASI CCM WADAIWA KUMPIGA PADRI JIMBONI KALENGA



Paroko wa Kanisa la Orthodox, Parokia za Nyamihuu Kalenga, Iringa, Costantino Mbilinyi akizungunza na waandishi wa habari nyumbani kwake katika Kijiji cha Nyamihuu jana kuhusu kushambuliwa kwake.
Padri wa Makanisa ya Orthodox katika Kijiji cha Nyamihuu, Kata ya Nzihi, jimboni Kalenga Constantino Mbilinyi (36) amepigwa na kujeruhiwa na watu wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa CCM.
0 Toa maoni yako.

GAZETI LA LEO TANZANIA DAIMA


0 Toa maoni yako.

Viongozi wa Umoja wa Ulaya wanakutana kwa dharura jijini Brussels kuijadili Urusi Baadhi ya viongozi wa Umoja wa Ulaya wakikutana jijini Brussels Na Ali Bilali Viongozi wa Umoja wa Ulaya wanakutana Alhamisi hii katika kikao cha dharura mjini Brussels nchini Ubelgiji kuamua hatua za kuichukulia Urusi, baada ya kutuma jeshi lake katika eneo la Crimea nchini Ukraine. Baadhi ya viongozi wa Umoja huo kutoka Mashariki mwa Ulaya wanataka serikali ya rais Vladimir Putin kuwekewa vikwazo vya kiuchumi na siasa lakini Kansela wa Ujerumani Angela Merkel anaona ni vema ikiwa mazungumzo yatatumiwa kuipatanisha Urusi na Ukraine. Katika hatua nyingine, rais wa Tume ya Umoja wa Ulaya Jose Manuel Barroso amesema kuwa Umoja huo utatoa msaada wa Dola Bilioni 15 kwa serikali ya Ukraine ili kujikwamua Kiuchumi baada ya uchumi wake kuanza kudorora kutokana na mzozo wa kisiasa na usalama unaendelea nchini humo. Wakati uo huo, Katibu Mkuu wa Majeshi ya nchi za kujihami NATO Anders Fogh Rasmussen amesema kuwa jeshi hilo linaangalia upya uhusiano wake na Urusi katika juhudi zinazofanyika kuishinikiza serikali ya Urusi kuyaondoa majeshi yake nchini Ukraine. Haya yote yanajiri baada ya wawakilishi wa Marekani na Urusi kukutana jijini Paris nchini Ufaransa siku ya Jumatano na kuahidi kuendelea kuzungumza kuhusu hali ya usalama na kisiasa nchini Ukraine. Waziri wa Mambo ya nje wa Marekani John Kerry na mwenzanke wa Urusi wa Sergei Larvov wamesema mazungumzo yao hayakuwa mepesi lakini hawana lingine bali kuendelea kuzungumza kupata suluhu la kudumu. Katika mkutano huo Lavrov alikataa kukutana na Waziri wa Mambo ya nje wa Ukraine Andriy Deshchytsia, kwa sababu Moscow haiitambui serikali iliyoko madarakani na juhudi za Kerry kujaribu kumshawishi Larvov kukutana na mwakilishi huyo wa Ukraine ziliambulia patupu. Urusi imeendelea kushtumiwa kuivamia Ukraine kijeshi tuhma ambazo Moscow inakanusha kwa kile inachokisema kuwa ilikwenda kuisaidia nchi hiyo baada ya ombi kutoka kwa rais wa zamani Viktor Yanukyovich na pia walikwenda kuwalinda raia na maslahi yao katika eneo hilo la Crimea. Brian Wanyama ni mchambuzi wa siasa za Kimaifa na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Masinde Muliro nchini Kenya ameimbia RFI Kiswahili kuwa Jumuiya ya Kimataifa itafanikiwa kusuluhisha mgogoro huu kwa kuileta Urusi na Ukraine katika meza ya mazungumzo. Marekani pamoja na Mataifa mengine ya Magharibi yamesema yatasimama na Ukraine na kuipa msaada wa kifedha na kijeshi.


Baadhi ya viongozi wa Umoja wa Ulaya wakikutana jijini Brussels
Na Ali Bilali
Viongozi wa Umoja wa Ulaya wanakutana Alhamisi hii katika kikao cha dharura mjini Brussels nchini Ubelgiji kuamua hatua za kuichukulia Urusi, baada ya kutuma jeshi lake katika eneo la Crimea nchini Ukraine.
Baadhi ya viongozi wa Umoja huo kutoka Mashariki mwa Ulaya wanataka serikali ya rais Vladimir Putin kuwekewa vikwazo vya kiuchumi na siasa lakini Kansela wa Ujerumani Angela Merkel anaona ni vema ikiwa mazungumzo yatatumiwa kuipatanisha Urusi na Ukraine.
0 Toa maoni yako.

KATUNI YA KIPANYA KUHUSU UKRAINE NA SYRIA

0 Toa maoni yako.

Benki ya Uwekezaji ya Umoja wa Ulaya kuendelea kuipa mkopo serikali ya Uganda licha ya kusaini sheria ya kipiga marufu ndoa za watu wa jinsi moja


Makam mwenyekiti wa benki ya uwekezaji barani Ulaya Pim Vam Ballekom
Na Ali Bilali
Benki ya uwekezaji ya Umoja wa Ulaya, inasema kuwa itaendelea kuisaidia Uganda kwa kuwapa mikopo na kuwekeza katika sekta mbalimbali ili kuinua uchumi wao licha ya rais Yoweri Museveni kutia saini sheria inayopiga marufuku ndoa za jinsi moja nchini humo.
Marekani na Uingereza na Mataifa mengine ya Magharibi yametishia kusitisha misaada nchini Uganda, na tayari Benki ya Dunia imesitisha kutoa mkopo kwa serikali ya Kampala.
0 Toa maoni yako.

Waandishi wa habari wazuiwa BUNGENI



Mwenyekiti wa muda wa Bunge la katiba,Pandu kificho.PICHA|MAKTABA
Dodoma. Bunge Maalumu la Katiba limepitisha kanuni ya kuwazuia waandishi wa habari kuingia katika vikao vya kamati za chombo hicho, hatua ambayo inaelezwa ni kinyume na Katiba inayotoa uhuru wa wananchi kupata habari.

Kanuni hiyo ilipitishwa jana baada ya malumbano makali yaliyowagawa wajumbe wa bunge hilo, baadhi wakipinga kifungu hicho kwa sababu kinavunja Katiba ya nchi inayotoa uhuru kwa waandishi kukusanya na kusambaza habari na wengine wakiunga mkono kuwazuia.

Kanuni hiyo ilipitishwa kwa mbinde huku baadhi ya wajumbe wakiendelea kushikilia msimamo wa kuikataa, hata baada ya Mwenyekiti wa Muda wa bunge hilo, Pandu Ameir Kificho kuridhia kipite. Wajumbe waliopinga kanuni hiyo ni Joshua Nasari, Moses Machali, Peter Serukamba, Ezekiah Wenje na Maria Sarungi.
0 Toa maoni yako.

Mwana wa waziri azuia ndege kutua

Shirika la ndege la MEA lasema ndege yake iliyokuwa na abiria 71 ililazimika kurudi Beirut baada ya mtoto wa kiume wa waziri wa uchukuzi wa Iraq kuchelewa kuabiri na kupiga simu Baghdad akiomba ndege hiyo izuiwe kutua.
Ndege aina ya Boeing 747-8
Ndege ya shirika la ndege la Mashariki ya Kati (MEA) iliyokuwa ikitoka Lebanon kuelekea Iraq ililazimika kurejea ilikotoka ikiwa katikati ya safari Alhamis, baada ya mtoto wa kiume wa waziri wa uchukuzi wa Iraq kuchelewa kuabiri ndege hiyo kwa wakati na kupiga simu Baghdad akiomba ndege hiyo izuiwe kutua.
0 Toa maoni yako.

CCM, CHADEMA, CUF WANAVURUGA BUNGE, ASEMA DOVUTWA


Mjumbe wa bunge maalumu la katiba Fahmi Dovutwa akichangia mada wakati wa semina ya wajumbe hao ya kupitia vifungu vya rasimu ya kanuni juzi.Picha na Silvan Kiwale
Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Fahmi Dovutwa alichafua hali ya hewa baada ya kuvituhumu vyama vya CCM, Chadema na CUF kuwa ndiyo vinavuruga Bunge kwa sababu ya misimamo yao.
0 Toa maoni yako.

Mvutano wa madaraka ndani ya chama tawala Uganda-NRM

Waziri Mkuu wa Uganda Amama Mbabazi
Utata umejitokeza katika uwongozi wa chama tawala cha muda mrefu cha Uganda NRM baada ya kutolewa taarifa inayotatanisha kwamba, Rais Yoweri Museveni amemteuwa Katibu Mkuu mpya wa chama chake.
0 Toa maoni yako.

Juhudi za Kerry zagonga mwamba Paris


Katika njia Panda: Sergei Lavrov na John Kerry.
Juhudi za marekani kuwakutanisha kwa mara ya kwanza ana kwa na mawaziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Urusi na Ukraine kuhusu mzozo unaoendelea katika jimbo la Crimea zimegonga mwamba.
Ingawa waziri wa mashauri ya nchi za kigeni Marekani John Kerry amekanusha kwamba palikuwa na nia ya kumkutanisha mwenzake wa Urusi Sergey Lavrov na waziri mpya wa mashauri ya nchi za wa Ukraine Andrii Deschchytsia iwapo wawili hao wangekutana mjini Paris ingekuwa ni mafanikio makubwa ya kidiplomasia.
0 Toa maoni yako.

Wabunge Kenya wataka sheria kali dhidi ya wapenzi wa jinsia moja

Mbunge Irungu Kang’ata anaongoza juhudi za kundi lililoundwa majuzi la kupinga wapenzi wa jinsia moja nchini Kenya. Sheria zilizopo zasema ni hatia kwa watu kujiingiza katika tabia za ushoga na adhabu yake ni kifungo cha miaka 14 jela.
Mwandishi vitabu Binyavanga Wainaina aliyetangaza majuzi kuwa anashiriki mapenzi ya jinsia moja
Kenya huenda ikawa nchi inayofuata kwenye utata unaohusiana na haki za wapenzi wa jinsia moja, huku wabunge wakipanga kuwasilisha mswada bungeni kushinikiza serikali kufanya juhudi zaidi kutekeleza sheria zilizomo za kupiga marufuku ushoga.
0 Toa maoni yako.

Mapigano mapya mjini Juba


Wanajeshi wa waasi nchini Sudan Kusini
Wanajeshi watano wa serikali ya Sudan Kusini wameuawa kufuatia mapigano makali ndani ya kambi moja ya kijeshi mjini Juba.
0 Toa maoni yako.

WHO yapunguza kiwango cha sukari


Madhara ya sukari.
Shirika la Afya duniani WHO limepunguza kwa nusu kiwango cha sukari kilichopendekezwa kwa matumizi ya binadamu ili kuepusha matatizo ya kiafya kama vile kunenepa kupita kiasi na meno kuoza.
0 Toa maoni yako.

‘WACHINA WALITOA RUSHWA’



Raia wa China wanaotuhumiwa kukutwa na pembe za ndovu zaidi ya vipande 700 wakisubiri kuanza kwa shauri lao katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam jana. Picha na Venance Nestory.
0 Toa maoni yako.

Afya ya Maranda sasa yatetereka, alazwa Moi

Dar es Salaam. Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rajabu Maranda, anayetumikia kifungo cha miaka 18 gerezani kwa wizi wa fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (Epa) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili akisumbuliwa na tatizo la mgongo.

Msemaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Upasuaji wa Mishipa ya Fahamu (MOI), Jumaa Almasi aliliambia gazeti hili jana kuwa Maranda alifikishwa hospitalini hapo Februari 16, mwaka huu.
0 Toa maoni yako.

Mtoto wa miaka 13 anusurika kuchinjwa na baba yake mzazi

Kahama. Mwanafunzi wa darasa la tatu Shule ya Msingi Majengo, wilayani Kahama, mkoani Shinyanga amelazwa katika Hospitali ya wilaya baada ya kunusurika kifo kutokana na jaribio la kuchinjwa na baba yake mzazi.

Tukio hilo limekuja siku 10 baada ya mtu mmoja, Ustadh Mohamed Kurangwa (36), kumuua mwanafunzi wa Shule ya Msingi Nzasa, Jamal Salum (12) kisha naye kuuawa, Mbagala, Dar es Salaam.
Kurangwa alimuua Jamal nyumbani kwake Mbagala Charambe Mianzini kwa kumchinja na kuweka kichwa cha marehemu kwenye miguu ya mtoto huyo, kisha kuupeleka mwili wake choo cha nyumba anayoishi muuaji. Muuaji huyo alizoa damu na kuijaza kwenye ndoo kisha kuiweka pembeni ya nyumba yake kabla ya kuingia chumbani kwake, kujifungia na kusoma Koran. Katika tukio la Kahama, Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk Joseph Fwoma alimtaja mwanafunzi huyo kuwa ni Said Siraji (13) na alifikishwa hospitalini hapo jana alfajiri baada ya kuokotwa na wasamaria mwema akivuja damu shingoni.
0 Toa maoni yako.

Chausta kuzindua kampeni leo

Iringa. Mgombea wa ubunge Jimbo la Kalenga kupitia Chama cha Chausta, Richard Minja atazindua kampeni zake rasmi leo.

Katibu Mkuu wa Chausta, Mwaka Mgimwa alisema pamoja na kuchelewa kuanza kampeni, watafanya kazi kubwa ili kuhakikisha wanapata ushindi katika jimbo hilo.

Alisema alikuwa bungeni Dodoma na kwamba amejipanga kufanya kampeni kijiji hadi kijiji katika muda uliobaki.

Chama hicho kimeshindwa kuanza kampeni mapema kutokana na mgombea wake kuwa nje ya mkoa kwa muda mrefu kutokana na kubanwa na shughuli za kijamii.

Chausta walitarajiwa kuzindua kampeni tangu Februari 22 katika Kijiji cha Kibaoni Kata ya Ifunda, lakini ilishindikana kwa kuwa mgombea alikuwa nje ya jimbo.

Akiongea na Mwananchi kwa njia ya simu, Minja alisema kwamba kuwa kimya haina maana kwamba, hatafanya kampeni kwenye uchaguzi huo.

“Nafanya kampeni kimya kimya, siyo lazima kusindikizwa na matarumbeta kwenda kwenye kampeni kama wanavyofanya wengine. Wao wana staili yao na mimi nina yangu,” alisema Minja.

Wakati Chausta wakisuasua kuanza kampeni, vyama vya CCM na Chadema vimeendelea kushikana mashati.

Kwa upande wao CCM, wamewataka wapinzani wao Chadema kufanya kampeni zenye taswira ya amani na utulivu kwa faida ya wananchi wa Kalenga.

Wakati CCM wanatoa kauli hiyo, Chadema wamelishukia Jeshi la Polisi wakitaka litende haki wakati wote wa kampeni ili kuepusha vurugu zisizo na ulazima.

Kauli hizo zimetolewa na viongozi wa vyama hivyo wa kitaifa waliowasili Kalenga kushiriki kampeni.
0 Toa maoni yako.

Sitta apiga jaramba kuongoza Bunge



Mwenyekiti wa Muda wa Bunge Maalumu la Katiba, Pandu Ameir Kificho, akizungumza na mjumbe wa Bunge hilo, Samuel Sitta (kushoto), ndani ya Ukumbi wa Bunge, Dodoma jana. Picha na Emmanuel Herman
Na Waandishi Wetu, Mwananchi
Dodoma. Siku moja baada ya kuteuliwa na CCM kuwania uenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amesema ameanza kupitia sheria na kanuni zitakazomwezesha kuliongoza huku akiahidi kutenda haki kwa wajumbe wote iwapo atachaguliwa.
0 Toa maoni yako.

Obama ataka wachunguzi kutumwa Ukraine


Hali ya wasiwasi imekumba jimbo la Crimea.
Rais Obama ametangaza mapendekezo ambayo huenda yakatoa suluhu kwa mzozo wa Ukraine, ikiwemo kuwatuma wachunguzi wa kimataifa na kuanzishwa mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Moscow na serikali mpya mjini Kiev.
0 Toa maoni yako.

Urusi yaionya Marekani dhidi ya vitisho vya kuiwekea vikwazo vya kiuchumi na kwamba inauwezo wa kujikumu pekeake


mkutano wa vyombo vya habari wa rais wa Urusi Vladimir Poutine, March 4, 2014 jijini Moscou
REUTERS/Alexei Nikolskiy/RIA Novosti/Kremlin
Na Ali Bilali
Nchi ya Urusi imeionya serikali ya Marekani dhidi ya hatua yoyote iliyopanga kuchukua ikiwa ni pamoja na kuiwekea vikwazo vya kiuchumi na kuongeza kuwa atakaeumia kwenye mzozo huo atakuwa ni Marekani mwenyewe. Kauli ya Urusi inatolewa wakati huu ambapo rais wa Marekani Barack Obama akitishia kusitisha ushirikiano wake wa kibiashara na nchi ya Urusi ambapo pia amesharangaza kusitisha ushirikiano wa kijeshi na taifa hilo kufuatia hatua yake ya kuivamia nchi ya Ukraine. Urusi inasisitiza kuwa inauwezo wa kusimama yenyewe hata bila ya kutegemea wafanyabiashara toka nchini Marekani.
0 Toa maoni yako.

Mauaji zaidi yatokea Nigeria


Jeshi limekosolewa kwa kukosa kudhibiti mauaji Nigeria
Ghasia zaidi zimetokea Kaskazini Mashariki mwa Nigeria ambapo watu 13 wameuawa.
0 Toa maoni yako.

Zifwatazo ni nukuu za watu mablimbali mashuhuri duniani

Mwalimu Nyerere; “Nibora kuishi na fikra hai kuliko kuishi na fikra zilizo kufa”
“Unaweza kuwadanganya watu wote kwa muda fulani  na baathi ya watu wakati wote ila uwezi kuwadanganya watu wote kwa wakati wote”
Abrahamu Linlccon: “Raisi wa 16 wa nchi ya Marekani: Serikali ya watu,inayowatumikia watu na iliyowekwa na nawatu haita potea duniani”
Nelson Mandela; “Elimu ni silaha yenye nguvu yenye uwezo wa kuibadilisha dunia.”
“Kichwa kizuri na moyo mzuri huwa na ushirika”
“Kama unataka kutengeneza amani na adui yako,tengeneza nae urafiki kisha atakuwa rafiki yako”
0 Toa maoni yako.

UJENZI WA BARABARA YA KIMARA HADI KIVUKONI WAENDELEA, KUKAMILIKA NDANI YA MIEZI SITA


Sehemu ya Magomeni jijini Dar es salaam ikonesha maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo

Kituo cha Magomeni Kagera
0 Toa maoni yako.

Kutoka Bunge Maalum La Katiba Mjini Dodoma


Waziri Mkuu,Mizengo Pinda na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, wakitoka kwenye ukumbi wa Bunge mjini Dodoma Machi 3, 2014 baada ya kusitishwa shughuli za Bunge Maalum la Katiba.
0 Toa maoni yako.

MAAJABU: Chatu amshinda Mamba nguvu Australia



Nyoka huyo alijipinda kwa Mamba na kumbana hadi akafa

Chatu ameshinda vita vikali dhidi ya Mamba Kaskazini mwa mji wa QueensLand, kupigana na Mamba, kumpinda na kisha kumla.

Tukio hilo lilishuhudiwa katika ziwa Moondarra, karibu na mlima Isa na kunaswa kwa kamera na wakazi wa eneo hilo siku ya Jumapili.
0 Toa maoni yako.

Mwelekeo mpya bungeni, Pinda atoa hoja kutuliza hali ya hewa



Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akijibu maswali ya papo kwa hapo Bungeni, mjini Dodoma jana. Picha na Edwin Mjwahuzi
Na Waandishi Wetu, Mwananchi
Dodoma. Waziri Mkuu, Mizengo Pinda jana alifanikiwa kutuliza hali ya hewa bungeni baada ya kutoa mapendekezo yaliyoungwa mkono na pande zote zilizokuwa zinavutana kuhusu kupitisha baadhi ya vifungu vya Kanuni za Bunge la Katiba.
0 Toa maoni yako.
Viongozi wa CORD, raila Odinga (kulia) Moses Wetangula na Kalonzo Musyoka
Viongozi wa chama kikuu cha upinzani Kenya ODM katika Mungano wa CORD, wameweza kukubaliana Jumatatu baada ya malumbano makali mwishoni mwa wiki wakati wa kuwachagua viongozi wa chama.
Mvutano wao ulitishia kugawika kwa chama kutokana na utaratibu wa uchaguzi na kuwepo na makundi mawili ya viongozi walotafautiana kabisa juu ya mustakbal wa chama. Uchaguzi haukuweza kufanyika na umeahirishwa hadi mwakani.
0 Toa maoni yako.

Urusi yatetea hatua ya kijeshi Ukraine


Hali ya taharuki bado imelikumba jimbo la Crimea.
Urusi imetetea uamuzi wake kutuma wanajeshi nchini Ukraine, katika kikao cha dharura cha baraza la usalama la Umoja wa mataifa.
Balozi wa Urusi katika umoja wa mataifa, Vitaliy Churkin, amesema kuwa rais wa Ukraine aliyeng'olewa madarakani Viktor Yanukovych alikuwa ameiomba Moscow kutuma wanajeshi ili kuwalinda raia na kuzuia vita vya wenyewe kwa wenyewe.
0 Toa maoni yako.

Zitto aungana na CCM kutaka kura ya wazi

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), ameunga mkono msimamo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa kuwataka wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kupiga kura ya wazi katika kufanya uamuzi.

Zitto ameweka wazi msimamo wake jana kwenye kurasa zake za mitandao ya Facebook na Twitter akiwashauri wajumbe wa Bunge hilo kutoendelea na malumbano ya namna ya kupiga kura kati ya zile za siri au za wazi na badala yake kura ya wazi ipewe nafasi.

Alisema: “Nasikia kampeni zinaendelea Dodoma kuhusu uamuzi huo. Siasa zetu tunazifanya ni ‘zero-sum game’, kwamba anayepata anapata vyote, na anayekosa anakosa vyote, haipaswi kuwa hivyo hata kidogo.”

0 Toa maoni yako.

Pandu Kificho akalia kuti kavu, Aandaliwa mashtaka, kutimuliwa Siri za kumchukia zaanza kuvuja

SIKU chache baada ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kubaini kuwa kina wakati mgumu katika mijadala na upitishaji wa vifungu vya rasimu ya katiba, kimeanza kutafuta mchawi.

Tayari chama hicho kimeshamshika uchawi Mwenyekiti wa Muda wa Bunge la Katiba na Spika wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho, kwa kuwasilisha waraka wa maoni ya baraza hilo kwenye Tume ya Mabadiliko ya Katiba yanayotaka serikali tatu, tofauti na msimamo wa chama chake kinachoamini katika serikali mbili.
0 Toa maoni yako.

Katuni ya Kuza za Siri za Bunge Malumu a Katiba Tanzania

0 Toa maoni yako.

TEC: Bunge lisikashifu mapendekezo ya Serikali tatu


“Katiba yetu isiruhusu wachache wenye nguvu ya kisiasa, kiuchumi na kiutawala kutumia vibaya uwezo wao na kusababisha utengano kitabaka,”
Dodoma. Tume ya Haki na Amani ya Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), imetoa tamko ikitaka Bunge Maalumu la Katiba kuepuka kukashifu mapendekezo ya muundo wa Serikali tatu.

TEC imesema muundo wa Serikali mbili haukutatua matatizo ya msingi na badala yake ulilimbikiza kero zilizosababisha Zanzibar kujiundia Katiba yake mwaka 2010 bila kushauriana na Tanzania Bara.
0 Toa maoni yako.

Posho juu bungeni Ikulu, Bunge wazunguka mbuyu

WAKATI Ikulu ikitangaza kuwa posho kwa wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba haijaongezeka, Tanzania Daima imebaini kuwa imeongezeka kwa sh 140,000 kwa siku za Jumamosi na Jumapili tofauti na ilivyokuwa siku za nyuma.
Kuongezeka kwa posho hiyo ingawa kihesabu imebaki vilevile sh 300,000 kwa siku kunatokana na Ikulu kubariki pendekezo la uongozi wa Bunge Maalum la Katiba kutaka posho ya kujikimu ambayo ilikuwa sh 80,000 iwe posho ya kikao na ile ya kazi maalumu ya sh 220,000 iwe posho ya kujikimu.
0 Toa maoni yako.

Maandamano ya kuipinga Urusi, Ukraine.
Kundi la mataifa saba yaliyostawi zaidi kiviwanda almaarufu kama G7 limelaani vikali hatua za kijeshi zilizochukuliwa na Urusi nchini Ukraine-viongozi kundi hilo wakitaja hatua ya Urusi kama ukiukaji wa uhuru wa Ukraine.
Katika taarifa ya pamoja iliyotiwa pia saini na Umoja wa Ulaya EU-Urusi imetakiwa kushughulia wasiwasi wake kuihusu Ukraini kupitia mashauri au upatanishi.
0 Toa maoni yako.

Lupita Nyon'go ashinda tuzo ya Oscar


Lupita Nyong'o,ameshinda tuzo ya muigizaji bora msaidizi katika filam aliyoshiriki "12 Years a Slave", akizungumza katika tuzo za 86 za Oscar huko Hollywood, California March 2, 2014. REUTERS/Lucy Nicholson (UNITED STATES TAGS: ENTERTAINMENT) (OSCARS-SHOW) - RTR3FY5W
Mcheza sinema maarufu Lupita Nyong’o ambaye ni raia wa Kenya, Jumapili ameshinda tuzo la kifahari la Oscar huko Hollywood California.
0 Toa maoni yako.
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company